Friday, November 23, 2012

Na hii ni harusi ya Kihaya

Hivi ndivyo ilivyokuwa reception ya Bw. Dianus Mutta iliyofanyika kwenye ukumbi wa Equator Grill Temeke tarehe 27/10/2012.

Safari yenye bahati

Dada Appia alibahatika kushuhudia zoezi hili la kutoa mahari kwa kaka yake Macarios kabla ya kusafiri usiku wa tarehe 11/11/2012 kurudi Norway anakoishi hivi sasa

Mzee Mdimi alifurahi

Ujumbe kwenda Gongolamboto kwa lengo lakutoa mahari ya Bw.Macarios Banzi ilikuwa chini ya ushauri wa Mzee Mangengesa Mdimi. Wakati wote wa shughuli yeye alifurahi sana kwani shughuli zilikwenda kama tulivyopanga.

Vinywaji vilikuwepo

Waluguru wanasema shughuli 'mbwali.' Ndivyo ilivyokuwa wakati wakutoa mahari ya Bw. Macarios ilikuwa nipe nikupe pande zote zilifurahi na kupongezana kwa chakula na vinywaji!

Thursday, November 22, 2012

Kilichofuata baada ya kutoa mahari

Mama Cathy a.k.a Mrs Banzi wa Moro akizirudi na shemjie Dikupatile!
Renatus Banzi a.k.a bepari akifurahia tukio na kujimwaga uwanjani
Mshenga Bw. Lawrence Mkude akicheza kwa furaha baada ya kukamilisha shughuli.

Vimbwanga vya kwenye mahari

Kwenye kutoa mahari kulikuwa na vituko vya aina yake lakini hivi vyote vilifanywa kwa nia nzuri tu ya kusherehesha shughuli. Dada wa Macarios (Helmina Mwenda na Eddy Daulinge)walijitokeza na kumuonyesha Martina kuwa wao ndiyo wanawake zake Macarios na hawana habari yoyote ya kuchumbuiwa kwake.Fuatilia picha hizi kwa makini upate uhondo.
'Mke mkubwa' Helmina Mwenda akimlalia 'mumewe' Macarios Banzi akionyesha yeye ndiye zaidi
Ilibidi shangazi P.Mloka na kaka Inno waokoe jahazi, la sivyo shughuli 'ingeharibika'!

Ndiye Martina Jeremias

Huyu ndiye shemeji yangu Martina Jeremias. Usiulize maswali mengine!

Kaka furaha!

Mratibu wa shughuli ya kutoa mahari ya Bw. Macarios Banzi alikuwa ni Banzi wa Moro! (pichani)

Wanajiandaa kuwasilisha mahari

Shangazi P.Mloka na Mshenga Bw. L.Mkude wakijiandaa kuwasilisha mahari ya Bw. Macarios Banzi mapema mwezi Novemba 2012 huko Gongolamboto.
Mmoja wa negotiatiors tuliokuwa nao kwenye msafara huo ni Baba yetu Mangengesa Mdimi (mwenye T-shirt nyeupe)mmmoja wa wandishi wakongwe hapa nchini.

Ufuta Je?

Hapa tuliambiwa kuleta ufuta pia uhusiano wake katika mahari mimi sijui lakini nafaikiri una maana yake. (Nitauliza baada ya mdogo wangu kufunga ndoa!)

Kukabidhi mablanketi

Moja ya vifaa tulivyotakiwa kutoa kwenye mahari ni mablanketi pichani shangazi wa Bw. Macarios Banzi Mama P.Mloka anakabidhi mablanketi.

Shughuli ya kutoa mahari

Akina dada rukhsa

Akina dada wanaruhusiwa kuwa kwenye timu ya majadiliano wakati wa kutoa mahari. Pichani kutoka kushoto Eddy Daulinge na Suzy Banzi wakifuatilia kwa makini shughuli ya utoaji mahari kwa kaka yao Macarios Banzi huko Gongolamboto tarehe 11/11/2012

Timu yetu

Timu yetu ya majadiliano kwenye mahari ya Bw. Macarios Banzi iliongozwa na Bw. Lawrence Mkude wa Mbezi (Mwenye shati nyekundu)

Tunajipanga

Kabla ya kwenda kutoa mahari ya Macarios Banzi, kikao kilifanyika kwenye baa ya Mgaereza iitwayo 'Recreation' pale Gongolamboto ili tuweze kujipanga vizuri.

Tuesday, November 13, 2012

Chereko- Baba kapata Mama!

Baada ya shughuli ya mahari kwenye shughuli ya Macarios ilibidi ndugu waserebuke pichani kutoka kushoto dada Mwenda na Dada Appia wakicheza kwa furaha