Monday, July 29, 2013

Karanga, maharagwe bwerere -Songea

Vyakula ni vingi sana mkoani Ruvuma. Karanga,maharagwe vinapatikana kwa wingi katika soko la Songea.
(Picha kwa hisani ya Dkt. Louis Kasuga wa ARI-Naliendele, Mtwara)

Matunda na viungo bila madawa

Mapapai, vitunguu na nyanya zikiwa sokoni Songea. Asilimia ya mazao haya hayajazalishwa kwa kutmia mbolea wala madawa.

Mama mfanyabiashara sokoni Songea

Akina mama wa Tanzania wamechangamka katika ujasiriamali. Mtafiti Dr. Louis Kasuga kutoka kituo cha Utafiti Naliendele, Mtwara alinasa picha ya mwanamama huyu akiwa katika soko la mjini Songea akifanya biashara ya mazao mbalimbali.

Dagaa sokoni Songea

Dagaa sokoni Songea.Nafikiri hawa ni dagaa kutoka ziwa Nyasa (Picha kwa hisani ya Dr. Louis Kasuga wa ARI-Naliendele)

Thursday, July 25, 2013

Baada ya msiba maisha yanaendelea

Baada ya msiba wadogo zangu walinipitisha katika eneo la mashamba ya baba zetu na kunionyesha mipaka. Inabidi tutunze raslimali zetu kwanza kwa kuzitambua na pili kuweka mikakati ya kuzitunza na kuziendeleza.Hii ni sehemu ya mashamba yetu yaliyopo katika kijiji cha Nige, Kariakoo-Matombo, Morogoro.

Usafi wa mazingira ndani na nje baada ya mazishi mila ya Kiluguru

Usafi wa ndani na nje ya mahali pa msiba unafanywa baada ya kuzika. Hii ni moja ya mila na desturi za Waluguru ambayo wengi hatuifahamu na pia hatuizingatii. Tulipomzika mama mkubwa Fortunata pale kijijini kwetu Nige, Kariakoo, Matombo-Morogoro nilishuhudia kinadada wakifanya shughuli hii ya usafi. Mgawawanyo wa kazi unazingatiwa hata kwenye misiba. Baba mdogo alionekana kuchoma kuku (Gender issue!)

Tukishazika siku inayofuata tuna choma kuku na kula

Waluguru siku moja baada ya kuzika kuna kitu kinachoitwa moto ndugu. Moja ya vitu vinavyofanyika asubuhi ni kubanika kuku kwenye moto na kisha wanandugu kugawa nyama kidogo kidogo na kuzila bila kutafuna mfupa.Tunaamini kuwa kwa kufanya hivyo tunafukuza kifo kwenye familia.

KARIBU MKOA WA MOROGORO

Mkoa wenye watu wapole, wanawake na wanaume wazuri,wenye heshima, wavumilivu na wachapakazi,wapenda michezo hasa mpira wa miguu pamoja na muziki. Moro kwenye mabonde na milima,mbuga, na maji yanayotiririka mwaka mzima,Bwawa la Mindu, Chuo Kikuu cha Kilimo, Chuo Kikuu cha Waislamu, Chuo Kikuu Mzumbe, Kituo cha Utafiti wa Kilimo Cholima Dakawa,Kituo cha Utafiti Kilimo Ilonga, Kituo cha Utafiti wa Kilimo KATRIN Ifakara, Taasisi ya Utafiti wa Malaria-Ifakara, Bwawa la kuzalisha umeme-Kidatu,Chuo cha wakulima Mkindo,Chuo cha Ualimu Ilonga, Chuo cha Ualimu Mhonda, Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Taasisi ya Utafiti wa Misitu (TAFORI), TV ABOOD, ABOOD BUS SERVICED, HOOD BUS SERVICES. Vyakula vingi kama mpunga,mahindi,mtama,muhogo,maboga,viazi vikuu,magimbi. Mboga za mwidu,derega,mchunga,bwasali, bamia,nyanya chungu,tunguja,nyanya maji,mwage,matango Matunda ya machungwa,ndizi,maembe,pasion,mafenesi,mashelisheli,tikitimaji. MORO SAFI SANAAA! KARIBU

Tuesday, July 23, 2013

Nilikabidhi msiba kwa baba zangu

Nilipofika nyumbani kijijini Nige, Kariakoo, Matombo, Morogoro nilikabidhi msiba kwa baba zangu Emil Bongwa na Kassian Mabwe (Pichani kutoka kushoto kwenda kulia) ni taratibu za familia ya baba zangu nasi tunaziheshimu na tunawaheshimu sana.

Dada zetu wakiomboleza msibani

Akina dada msibani ilikuwa ni kulia kulia kulia!

Renatus Banzi katika Pilika za msiba

Mtoto wa marehemu Renatus Banzi akiwa katika hekaheka za maandalizi ya msiba.

Wamejiandaa kwa safari kuelekea Matombo Morogoro

Mama Cathy na Macarios Banzi tayari kwa safari ya Matombo msibani.

Mazishi ya mama mkubwa Fortunata Epimark

Jumatatu ya tarehe 17/6/2013 ni siku ya msiba kwa familia ya akina Banzi wakati mama mkubwa Fortunata Epimark mke wa baba yetu mkubwa Mwl. Ephrem Ephrem Mbiki alipofariki jijini Dar na kuzikwa kijijini Matombo, Morogoro. Pichani jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa kwenye kanisa Katoliki, Parokia ya Mavurunza, Kimara Dar Es Salaam kwa Ibada ya kumuombea kabla ya kusafirisha mwili kwenda kijijini.

Nakagua bustani ya vijana Kisemvule

Mwanzo mgumu. Miche ya matikitimaji imeanza kuota kwenye bustani ya vijana iliyopo kijijini Kisemvule.Nitawasaidia vijana hawa ili wasonge mbele na kutimiza ndoto zao. Vijana wengine tuige mfano wa vijana hawa watatu.

Kisima kitakachotumika kumwagilia bustani ya mbogamboga Kisemvule

Maji mengi yaliyopo kijijini Kisemvule yamewahamasisha vijana kuja na wazo la kulima bustani ya mbogamboga.Hawa watafanikiwa.

Wameamua kulima bustani ya mboga kijijini Kisemvule

Bw. Peter  Linus Mkude (Mwenye shati jekundu) na rafiki zake wawili (mmojawapo mwenye shati jeupe) wameaumua kulima bustani ya mboga mboga. Kwa kuanza tayari wameshaandaa eneo lipatalo nusu eka na kupanda matikiti maji. Ni wazo walilokuja nalo kujikwamua kiuchumi. Tarehe 21/7/2013 nilipata kutembelea sehemu hiyo iliyopo kijijini Kisemvule wilaya ya Mkuranga mwanangu Maria pichani kushoto na rafiki yake nao walikuwa na shauku ya kuona shamba hilo.

Kisima cha 'mdundiko' kijijini Kisemvule

Kisima hiki kiko katika kijiji cha Kisemvule wilayani Mkuranga. Kimetengenezwa na mwanakijiji anayejulikana kwa jina la Kite.Maji ya kisima hiki hayana chumvi, ni baridi hakika yana ladha nzuri.Hivi majuzi nilipata kumtembelea Bw. Kite na kujaribu kusukuma maji kutoka kisimani.

Kiwanda cha Cement ya Rhino-Kisemvule, Mkuranga

Hiki ndicho kiwanda cha cement ya Rhino kilichopo kwenye kijiji cha Kisemvule, wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani.

Mapadri wapya Kanisa Katoliki nchini Tanzania

Zamani ilikuwa si rahisi kuwapata mapadre kama ilivyokuwa vigumu kuwapata wasomi ngazi ya PhD, Madaktari wa binadamu pamoja na wahandisi. Hivi sasa jimbo linaweza kutoa mapadri saba kwa wakati mmoja kama ilivyotokea hivi karibuni kwa jimbo kuu la Dar Es Salaam. (Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi)

Thursday, July 18, 2013

Furaha ya watoto kwenye shughuli ni wali!

Furaha ya watoto kwenye shughuli ni kula wali. Shughuli isiyokuwa na wali haina furaha kwa watoto!

Mwali amepanda 'bodaboda'

Baada ya shughuli mwali anasafirishwa kwa kutumia pikipiki kurudi nyumbani. Gharama yake ni ndogo na pia unatumia muda mfupi bila ya kumchosha abiria. Pamoja na matatizo yanayojitokeza hasa ajali za mara kwa mara, bado pikipiki zimerahisha usafiri wa vijijini.

Hawa ndio wali wa kiume wa Kizaramo

Zamani wali wa kiume wa Kizaramo walikuwa wakivalishwa kanzu wakati wanapochezwa (tafrija). Wali hawa wametia fora angalia walivyopendeza wakiwa ndani ya suti kali!

Wali wa kike wa Kizaramo

Kama kuna kabila linaloendeleza utamaduni wao basi Wazaramo ni mojawapo hasa inapokuwa masuala ya unyago kwa wasichana waliovunja ungo. Mara wanapopoata mafunzo wanayostahili hufanyiwa tafrija na hapa motto anazawadiwa zawadi mbalimbali na hasa nguo. Pichani wali waliochezwa kijijini Kisemvule hivi karibuni.

Tathmini ya pamoja ya Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo

Wakulima, wagani na watafiti ni muhimu wakafanya kazi kwa pamoja kuanzia kupanga, kutekeleza na kutathmini shughuli. Pichani wataalamu wa kilimo wakiwa ndani ya ofisi ya Afisa kilimo wa Wilaya ya Kilosa mapema mwezi Julai, 2013.

Nyumba ya Kisasa ya wageni mjini Kilosa

Kilosa sasa kumekucha  hakuna shida ya nyumba za wageni kama ilivyokuwepo miaka 10 iliyopita.Nyumba nyingi mpya na za kisasa zimejengwa mjini Kilosa.

DJ katika tamasha la Vijana Katoliki -Dekania ya Kigamboni

Inapokwa suala la muziki hakuna swali vijana ndo mahali pao.

Wanauza pepeta kwenye kivuko cha mto Kilombero

Akina dada wa Ifakara wakiuza pepeta (Rice flakes) katika kivuko cha mto Kilombero.Mpunga si kwa ajili ya wali tu. Mpunga unaweza kutumika kwa matumizi mengine kama vile pepeta, vitumbua pumba zake kama mbolea pamoja na kutengeneza kinywaji haya ni baadhi tu ya faida ya kulima mpunga.

Utafiti wa mpunga klituoni KATRIN-Ifakara

Wataalamu wa kilimo wakipata maalezo ya utafiti wa mpunga kutoka kwa mtafiti wa KATRIN-Ifakara walipotembelea shamba la majaribio la kituo lililopo katika mto Lumemo-Ifakara mapema mwezi Julai 2013.

Wednesday, July 17, 2013

Ufunguzi wa Kituo cha Utafiti KATRIN -Ifakara

Kituo cha Utafiti wa Kilimo KATRIN kilichopo Ifakara kimefunguliwa rasmi tarehe 22/3/1970  na Baba wa Taifa Mwl. J.K.Nyerere saini yake inapatikana katika kitabu cha wageni cha kituo hicho. Hakika ni kumbukumbu nzuri.

Vifaa vya umwagiliaji katika shamba la utafiti Ilonga

Mhasibu Mwandamizi Christopher Gibbson wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika akishangaa mabomba ya umwagiliaji katika shamba la utafiti Ilonga.

Shambani Lumemo - Ifakara

Toyota-Landcruiser, gari hili linafaa sana kwa shughuli za shambani kama vile za utafiti kilimo. Bw . Omari Kizito na Shuhu Jr wamekuwa wakiendesha gari la aina hii wakiambatana na watafiti vijijini. Hapa wapo kwenye shamba la Utafiti KATRIN katika mto Lumemo-Ifakara.

Dr. Chaboba Mkangwa-Zonal Director Research and Development-Eastern Zone

Utafiti wa zao la mtama na alizeti kituo cha Utafiti Ilonga

Utafiti wa alizeti na mtama umeandelea kufanywa kwa miaka mingi katika kituo cha utafiti Ilonga. Matokeo mazuri yamepatikana kama vile mbegu bora zinazozaa kwa wingi zinazovumilia ukame na magonjwa.


Ushindi ARI-Ilonga

Vikombe vilivyonyakuliwa na kituo cha Utafiti Ilonga ndani ya ofisi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki.

Friday, July 12, 2013

ARI-Ilonga Tanzania


Utafiti wa mtama kituoni Ilonga

Utafiti wa zao la mtama unafanyika katika kituo cha Utafiti Ilonga. Aina za mtama hutafitiwa ili kupata aina inayopendwa kwa matumizi mbalimbali.

Dr. Kasuga - Veteran researcher!

Dr. Louis Kasuga mtafiti wa korosho kutoka Naliendele akiwa kaziniwilayani Kilombero.

Maelezo kutoka kwa watafiti wa mpunga Cholima-Dakawa

Utafiti wa zao la mpunga umeendelea kufanyika nchini Tanzania kwa miaka mingi. Kituo cha Utafiti wa Kilimo Cholima -Dakawa ndiyo waliozalisha mbegu ya mpunga ijulikanoyo kwa jina la SARO 5 ambayo sasa imeanza kusambaa kwa haraka hapa nchini kutokana za sifa zake.

Teknolojia za kilimo cha Kichina kituo cha Dakawa

Mtaalamu wa Kichina wa kituo cha teknolojia za kilimo za Kichina akiwaonyesha wajumbe wa timu A ya kupelemba na kutathmini kanda ya Mashariki mwaka 2013 plot ya maonyesho ya vitunguu.
 

Pepeta za Ifakara!

Pepeta nazo ni tamu - kwa kiingereza zingeweza kuitwa 'Rice flakes' ni sawa kabisa na corn 'flakes'Nilipofika kwenye kivuko cha mto Kilombero nilinunua pepeta kiasi cha kilo tatu kwa gharama ya Tshs 4,500/=.

Trekta ni kila kitu

Huu ni wakati wa mavuno wilayani Kilombero. Pichani trekta likisafirisha mpunga kutoka shambani.