Thursday, October 31, 2013

Gari la maharusi

Gari lililowachukua Bw & Bibi Joe Mutahangrwa mara baada ya kufunga ndoa Kanisani Vikindu- Tarehe 26/10/2013.

Kampa amapofurahia utamaduni wa kwao

Ukimuona mtu mzima anaingia ndani ya uwanja basi tambua kwamba imemkuna. Pichani Mkurugenzi wa TANDAN FARMS ya Vikindu-Kisemvule Bw. Kampa ambaye ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya sherehe ya kuwapongeza Bw & Bi Joe Mutahangarwa baada ya kufunga ndoa yao akicheza ngoma ya asili ya  Kihaya.

Bw & Bibi Joe Mutahangarwa wakitoka kanisani

Bw & Bibi Joe Mutahangarwa wakitoka kanisani mara baada ya kufunga ndoa tarehe 26/10/2013 kanisani Vikindu.

Mr & Mrs Joe Mutahangarwa vyeti vya ndoa

Mambo yamekuwa mambo. Bw na Bibi Joe Mutahngarwa wakionyesha vyeti vyao vya ndoa siku ya tarehe 26/10/2013

Wazazi wa Daphrosa

Bw. na Bibi Nangeda wazazi wa Bi Daphrosa wakishudia ndoa ya mtoto wao kanisani Vikindu. Tarehe 26/10/2013.

Sir George Kahama Kanisani

Bibi Josephina Mutahangarwa, Bi. Janet Kahama na Sir Clement George Kahama wakiwa Kanisani Vikindu wakifuatilia Ibada ya ndoa ya Bw. na Bibi Joe Mutahangarwa iliyofanyika tarehe 26/10/2013.

Joe Mutahangarwa akifurahia Ibada

Bw. Joe Mutahangarwa na Mkewe Daphrosa wakiwa na furaha wakati wa Ibada ya ndoa yao Kanisani Vikindu.

Dada Kanisani

Dada zake Joe wakifutialia kwa makini Ibada ya ndoa ya Bw. na Bibi Joe Mutahangarwa iliyofanyika tarehe 26/10/2013 kanisani Vikindu.

Joe naye alimvisha pete mkewe

Bw. Joe Mutahangarwa akimvisha mkewe Daphrosa Nangeda pete ya ndoa alama ya uaminifu na kitu kimoja sasa anakuwa Mrs. Mutahangarwa! Tukio lililofanyika katika Kanisa la Mt. Vinsenti wa Paulo-Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Tarehe 26/10/2013

Kwaya ya Mt. Vinsenti wa Paulo ikitumbuiza kanisani

Kwaya ya Mt. Vinsenti wa Paulo - Parokia ya Vikindu, ilitoa burudani ya kutosha katika ibada takatifu ya misa ya ndoa ya Bw & Bi. Joe Mutahangarwa iliyofungwa tarehe 26/10/2013.

Siku Joe Mutahangarwa alipovishwa pete kanisani

Tarehe 26/10/2013 ndani ya Kanisa la Mt. Vinsenti wa Paulo-Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Bw. Joe Mutahangarwa  alivishwa pete ya  ndoa na mkewe Daphrosa Nangeda (Pichani) na baadaye tafrija ya nguvu ilifanyika huko Jesus Town Vikindu, TANDAN Restaurant.

Thursday, October 24, 2013

Mwanamke mlemavu mjasiriamali

Wengi wetu tumekamilika kimwili lakini hatupendi kufanya kazi ili tuweze kujipatia mkate wetu wa kila siku.
Lakini mama huyu, licha ya ulemavu wake ameamua kufanya biashara ya ndizi akiwa katika baiskeli yake. Hivi ndivyo inavyotakiwa.

Papa Francis upendo kwa watoto

Tangu  kuteuliwa kwake Papa Francis ameonyesha mapendo makubwa kwa watoto na watu fukara

Ajali pikipiki yangu

Pikipiki chni ya uvungu wa gari iliyogonga

Pikipiki baada ya ajali
Tarehe  29/8/2013 pikipiki yangu SANLG ilipata ajali mbaya lakini kijana aliyekuwa akiiendesha alinusurika hata hivyo alivunjika mguu. Hivi sasa ameshatoka hospitalini (Muhimbili) anajiuguza nyumbani kwake. Ukiziona picha hizi huwezi kuamini kuwa mwendesha pikipiki alinusurika katika ajali hii.

Tuesday, October 22, 2013

Gari moshi la Tanzania- Tija Je?

Gari moshi (Train) la Tanzania. Tanzania tumebahatika kuwa na njia mbili za reli. Reli ya kati na Tanzania-Zambia. Lakini nina mashaka kama matumizi ya reli hizi zinaleta tija nchini.

Ukiwa na baskeli hukosi kuziba pancha

Unatakiwa kuwa na viraka vya mpira, gundi, spanners, kopo na maji ili uweze kuziba pancha ya gurudumu la baiskeli!

J.M.Kikwete ndani ya shati la mbio za mwenge 2013

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ndani ya sare ya mbio za Mwenge 2013. Amependeza kwa kuwa imeshonwa vizuri. Kila kitu 'Made in Tanzania.' Watanzania tuna vingi vizuri tupende vya kwetu!

Unga wa Muhogo kwenye viroba


Bidhaa yoyote inayoandaliwa vizuri inavutia walaji. Angalia jinsi unga wa muhogo ulivyowekwa vizuri kwenye viroba tayari kwa kuuzwa. Unga wa muhogo ni mzuri na unapendwa na walaji wa sehemu nyingi nchini Tanzania. Kilimo hiki hakina budi kupewa kipaumbele hapa nchini si kwa njaa tu bali kwa kuongeza kipato cha wakulima wetu.  (Picha kwa hisani ya IITA).

Viazi mviringo chakula wanachopenda watoto

Ukitaka kuwafurahisha watoto basi wananulie chips hata kama ni chips kavu wataweka tomato sauce na siku ikawa nzuri kwao. Tanzania imebahatika kuwa na mazingira yanayoweza kustawisha aina mbalimbali ya mazao. Kwa mfano mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya ni maarufu kwa kilimo cha viazi mviringo (Picha kwa hisani ya IITA).

Mbegu bora za muhogo

Usiokote pingili ovyo za muhogo na kwenda kuzipanda shambani. Unaweza kueneza magonjwa kwenye shamba lako la muhogo, unaweza kupanda aina ya muhogo ambao ni mchungu. Pata mbegu bora kutoka kwenye vituo vya kilimo vinavyotambulika au wazalishaji wa mbegu wanaotambulika. (Picha kwa hisani ya kijarida cha IITA).

Mashine ya kupandia muhogo

Si  mahindi tu yanayoweza kupandwa na mashine bali hata muhogo  unaweza kutumia mashine kwa kupandia ikiwa una shamba lenye eneo kubwa. Pichani trekta ikivuta mashine ya kupandia muhogo. (Picha kwa hisani ja kijarida cha IITA)

Tengeneza fedha kwa kulima muhogo

Muhogo umekuwa mali. Licha ya kutumiwa kama chakula pia muhogo ni zao la biashara tembelea masoko ya Tandale, Buguruni, Tandika na Mbagala biashara ilivyoshamiri. Muhogo umekuwa mkombozi kwa akina mama katika jiji la Dar Es Salaam. Akina mama hao huuza muhogo mbichi (mtamu) kwa kutafuna, huchemsha na hutengeneza chips za muhogo (chips dume!)

Aflatoxin

What is aflatoxin?

  • Aflatoxin is a poison produced by a fungus called Aspegillus flavus
  • This fungus reside in soil and dead/decaying matter in the field
  • It is very dangerous to humans and animals
  • Aflatoxins affects many aother crops such as cassava, yam and rice
    How does aflatoxin harm us?

    • Aflatoxin causes liver cancer, suppresses the immune system, and retards the growth and development of children
    • Aflatoxin-infected crops are forced into low value markets or destroyed
    • Aflatoxin damages our health and business opportunities 

    Can we see aflatoxin?

    • Aflatoxin cannot be seen - it is colorless chemical
    • Aspergillus flavus is green in colour (right on the maize cob)
    • Grains without visible signs of A. flavus may also have high amounts of aflatoxin.
    • Laboratory tests determine contamination levels
    (Picture and information by IITA courtesy)

Monday, October 21, 2013

Familia ya Madenge - Matukio siku ya kupanda msalaba

Tarehe 12/10/2013. Familia ya Mzee Madenge wa Sinza ilihitimisha msiba wa Mama yao mzazi kwa Ibada ya Misa takatifu iliyofanyika katika Parokia ya Sinza baadaye kusimika msalaba huko Sinza Makaburini. Haya ni baadhi tu ya matukio muhimu ya siku hiyo.




Masista wa Parokia ya Sinza walihudhuria ibada ya  asubuhi
Dada Julieth Madenge na ndugu wengine wakiwa kanisani
Bus maalum liliwaleta wanandugu kanisani
Bw. Henry Elias Henrish Kobelo akielekeza jambo
shughuli ziliendelea makaburini
Dada Julietha Madenge akilia mbele ya kaburi la Baba yake Mzee Elias Henrish Madenge

St. Vincent Dispensary-Vikindu - Masaa 24

Zahanati ya Kanisa Katoliki St. Vincent iliyopo Vikindu mkoa wa Pwani sasa inafanya kazi masaa 24 na inapoke Bima ya NHSF. Zahanati hii iko pembezoni mwa barabara iendayo Mtwara karibu kabisa na Kanisa Katoliki Parokia ya Vikindu- St. Vincent de Paul

Maandalizi ya harusi ya Joe Mutahangarwa

Maandalizi ya harusi ya Bw. Joseph Mutahangarwa a.k.a Joe yanaendelea huku Vikindu- TANDAN FARMS - RESTAURANT. Harusi itafanyika  tarehe 19/10/2013 kwenye kanisa la Mt. Vinsenti wa Paulo Vikindu siku ya Jumamosi kuanzia saa 9.00 jioni. Pichani mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi Bw. Kampa akihesabu fedha za michango iliyotolewa na wadau wa sherehe hiyo huku Bw.harusi mtarajiwa (kulia) akiangalia kwa makini.

Serikali ya Kijiji Kisemvule wafurahi mahafali ya watoto wao

Serikali ya Kijiji cha Kisemvule ilijihusisha kwa asilimia 100 kwenye mahafali ya wanafunzi wa Darasa la Saba shule yao ya Msingi Kisemvule 2013 kama inavyoonekana pichani.

Himili Mbawala - Pongezi kwa kupata CPA

Tarehe 5/10/2013. Bw. Himili Mbawala alitunukiwa shahada ya Juu ya Uhasibu inayojulikana kama CPA. Mahafali hayo yaliyoandaliwa na Bodi ya Wahasibu (NBAA) yalifanyika Jijini Dar Katika Ukumbi wa Mlimani City.

Hongera Elizabeth Banzi

Elizabeth Banzi amehitimu Elimu ya Msingi mwaka huu katika shule ya Msingi Kisemvule.HONGERA

Wajumbe wa Africana kikaoni - Chang'ombe

Siku ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa - Mwl. J.K.Nyerere (14/10/2013) Kikundi cha Africana kilifanya kikao chake cha Mwezi huko Chang'ombe jijini Dar. Kikao cha mwezi Novemba kitanyika Ursino Estate, Dar Es Salaam. Wanachama mtatarifiwa tarehe kamili.
Madadaz-Ceasar Mloka, Slyvia Daulinge na Ghana Kunambi
Silyvester Jakka na Anthony Kunambi
Christian Mkoba,Suzy Kobelo na Maria Mkoba
Dada Ghana Kunambi
Dada Suzy Banzi

Mapambo kwa raha zako!

Wakati mwingine tunakuwa na gharama zisizo za lazima kwa ajili ya mapambo. Utasiki mapambo Tzs 1,600,000/=. Ona mapambo haya yalitengenzwa kwa ajili ya harusi moja kijijini Kisemvule- Mapambo maputo, makuti, vitambaa na mkeka mambo kwisha na harusi imefanyika  na ndoa inaendelea kwa mapenzi ya bashasha hadi leo!

Rhino Cement inatoka hapa

Hiki ndicho kiwanda cha Cement aina ya Rhino inayotengenezwa kijijini Kisemvule- Mkuranga mkoa wa Pwani. Cement ni nzuri, kiwanda kimeleta ajira kwa Watanzania. Je, kinasaidia nini jamii inayokizunguuka mazingira je? Hili liangaliwe ili wananchi wanafuike.

Vijana wa Kise Kids

Vijana hawa wa Timu ya soka ya kijijini Kisemvule  iitwayo kwa  'Kise Kids  Soccer Club' wamepania kuleta mabadiliko katika soka la Tanzania.

Punje linaliwa!

Utaitaka shughuli isiyokuwa na wali? Hapa vijana wawili wameachiwa sinia lao la punje!

Matunda - Fahari ya Tanzania

Tanzania imebarikiwa kuwa na hali ya hewa na udongo mzuri unaoweza kustawisha mazao ya aina mbalimbali yakiwemo machungwa na ndizi. Angalia ndizi na machungwa yakiuzwa Mabagala Rangi tatu jijini Dar Es Salaam.

Vijana wajenzi wa nyumba Kisemvule


Kijiji cha Kisemvule mkoa wa Pwani  kinakua kwa haraka sana. Karibu kila siku nyumba mpya zisizopungua 10 zinajengwa hapo kijijini. Hii imewafanya vijana wengi wa kijijini hapo kujifunza kazi ya ujenzi wa nyumba.