Friday, January 30, 2015

Batobato na Michirizi ya Njano unaangamiza muhogo

Michirizi ya njano (Kushoto) na Batobato (kulia) ni magonjwa yanayoteketeza mashamba ya muhogo hapa nchini. Mihogo iliyoathirika huoza. Ni ugonjwa yanayosumbua sana kwenye sehemu nyingi zinazozalisha muhogo hapa nchini na kuwapa hasara kubwa wakulima. Utafiti unaendelea kupambana na magonjwa  haya hasa unaolenga kupata aina bora za  mbegu zenye kuhimili magonjwa.

Utafiti wa Muhogo Chambezi kupitia mradi wa EAAPP

Ili kupata mbegu bora ya muhogo, utafiti hupitia hatua mbalimbali ikiwemo hii ya 'clonal evaluation trial' kama tulivyoelezwa na mtafiti Karoline Sichalwe(mwenye t-shirt ya mauamaua) kutoka kituo cha Utafiti wa Kilimo-Kibaha anayefanya utafiti wa kupata aina bora ya mbegu ya muhogo kwenye mashamba yaliyopo kituoni Chambezi-Bagamoyo. Utafiti unagharamiwa na mradi wa EAAPP.

Chambezi-Kituo kidogo cha Utafiti wa Kilimo

Hiki ni kituo kidogo cha Utafiti wa Kilimo  Chambezi wilayani Bagamoyo kinachosimamiwa na Kituo cha Utafiti Mikocheni kilichopo Dar Es Salaam. Kituo hiki kilianzishwa wakazi wa Mradi wa Taifa wa Kuendeleza  Zao la Mnazi kwa ufadhili wa Ujerumani. Kituo hiki kwa sasa hutumika zaidi kwa utafiti wa Muhogo ingawa tafiti za mazao mengine kama vile korosho na minazi unafanyika kwa kiasi kidogo. Kituo hiki kina eneo kubwa kwa shughuli za utafiti wa kilimo endapo kiyawezeshwa kupata raslimali za kutosha  kinaweza kuvutia shughuli nyingi za utafiti wa mazao  kanda ya mashariki.

Tukiwa Modiporum-India kwenye Taasisi ya Utafiti ya Mifumo ya Kilimo

Tulipokuwa kwenye ziara ya mafunzo nchini India mwaka 2014, timu yetu ilipata fursa ya kutembelea Taasisi ya Utafiti wa Mifumo ya Kilimo nchini India huko Modiporum. Hapa tulikutana na watafiti nguli wa Taasisi hiyo na kuongea nao jinsi wanavyoendesha utafiti wa aina hiyo ambapo hapa kwetu ni sehemu ndogo tu. Tulipata fursa ya kutembelea tafiti zinazoendelea hapo hapo kituoni zinazohusu mifumo ya kilimo. Baada ya hapo tulipata picha ya pamoja.Mwenye vazi la Kihindi ni Dr. Mohamed Bahari aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye alikuwa ndiye kiongozi wa msafara kutoka Tanzania.

Utafiti wa Nyati wa maziwa nchini India

Utafiti wa kupata aina ya nyati bora kwa utoaji wa maziwa ni endelevu nchini India. Taasisi ya Utafiti wa Ng'ombe wa Maziwa wanaendelea na tafiti mbalimbali kufikia lengo hili. Huku utafiti ikiendelea ng'ombe na nyati wanaozalishwa hupewa chakula kinachohitajiwa na kutunzwa kwenye mabanda ya kisasa.

Kutunza kumbukumbu ni muhimu

Nilipokuwa kwenye ziara ya mafunzo nchini India  nilikumbushwa umuhimu wa kutunza kumbukumbu ya mifugo kama inavyoonekana pichani. Kumbukumbu hizi ni za aina ya ng'ombe . Hiki ni kituo cha Utafiti kinatafiti aina bora ya ng'ombe wa maziwa anayewaza kupatikana kwa sifa wanazozihitaji ili aweze kusambazwa kwa wafugaji.

Kijiwe cha fundi baiskeli

Mafundi  baiskeli bado wapo ingawa kuingia kwa bodaboda kumemomonyoa umaarufu wao

Benny Morandi kijana anayejituma kuishi maisha bora



Benedict Morandi a.k.a. Bene ni kijana anayeishi kijijini Kiswira, Matombo Morogoro. Kijana huyu ni fundi seremala, mpiga picha, mkulima na mwanakwaya wa Parokia ya Mt. Paulo - Matombo. Ni kijana Mzalendo anayependa kijiji chake. Akiwa mdogo tu Bene tayari alishanunua sehemu yake ya makazi kwa  shilingi 30,000/= tu na hivi sasa amejenga nyumba ya kuishi yeye na familia yake(picha ya juu). Bene anapenda ndugu zake wa upande wa mkewe na wa kwake (picha ya chini). Anaisihi maisha ya kuvutia huku nyumba yake ikizungukwa na madhari mazuri.

Thursday, January 22, 2015

Mboga 'kilobani' inawezekana


Tutangaze korosho kutoka Tanzania



Miaka ya 80 mpaka 90 zao la korosho lilikuwa hoi bin taabani. Wakulima wengi waliyaacha mashamba yao ya korosho na kuangalia shughuli nyingine zinazolipa. Jitihada zilizofanywa na serikali kupitia wadau mbalimbali zimenyanyua uzalishaji wa zao hilo. Korosho sasa bei yake imepanda si chini ya shilingi 1000 kwa kilo kwa korosho ambazo hazijabanguliwa. Sasa wajasiriamali wengi wamejitokeza na kuanza kuziandaa korosho na kuzifunga kwenye muonekano mzuri. Katika mkoa wa Mtwara, wilaya ya Tandahimba inaongoza kwa uzalishaji wa korosho na mabadiliko unayoona dhahiri kupitia maisha ya wananchi wa Tandahimba. Wanavijiji wana makazi bora, huduma za shule ni nzuri hata upatikanaji wa maji safi na salama zimeboreshwa kupitia ruzuku kutoka Halmashauri inayopatikana kutokana zaidi na kipato kutoka zao la korosho.Hebu angalia korosho zilizofungashwa vizuri kutoka IMANI. Korosho hizi zilikuwa kwenye maonyesho ya NaneNane 2014 mkoani Lindi viwanja vya Ngongo.Mimi ni mmoja ya watu wanaopenda kutafuna korosho hazinikinaishi. Korosho ni tamu. Hivi ni kwanini unaposafiri kwa usafiri wa anga, mashirika ya ndege hapa nchini hawatangazi korosho zetu za Tanzania kwa kuwapatia abiria watafune kama snacks? Ukipanda Air Botswana au Swazi utatafuna nyama zilizokaushwa mpaka meno yaume na kutambua kweli unaelekea nchi ya wafugaji!

Wednesday, January 21, 2015

Mbegu za muhogo katika kiganja cha mtafiti

Hizi ndizo mbegu za muhogo. Wasio wakulima na wataalamu wa kilimo wanaweza kubisha kuwa muhogo hauna mbegu kwa kuwa wamezoea kuona muhogo ukipandikizwa kwa kutumia pingili. Nilipokuwa kwenye kituo kidogo cha majaribio ya utafiti kilichopo Chambezi, Bagamoyo, mtafiti alituonyesha mbegu za muhogo ambazo zinatumika katika mchakato wa kupata aina mbalimbali za muhogo.

Tuwe makini kwenye kuandika mabango

Hebu soma vizuri bango lililosimikwa kwenye nyumba hii ya wageni. Hivi umeelewa nini kuhusu 'Full AC with TV rooms?" MOTEL CROPS inapatikana mjini Bagamoyo.

Je ulishawahi kuomba 'lift' kwa Rais na kukubaliwa?

Rais wa Uruguay Jose Mujica na mkewe Lucia Topolansky (pichani)  hivi karibuni wamemshangaza kijana Gerhard Acosta  baada ya kumpa 'lift' kwenye gari yao ya serikali. Baadaye Gerhald alisema hivi " Nilipoteremka, nilishukuru na kufurahi sana kwa sababau si kila mtu mwenye moyo wa kumsaidia mtu asiyemjua barabarani, achilia mbali ni Rais wa nchi." Chanzo gazeti la Raia Mwema 21/01/2015.

Thursday, January 15, 2015

Tumeamua kufanya kazi kuendeleza kilimo nchini

Kutoka kulia - Prisca Massoro (Afisa Ugavi-MAFC), Hamza (Afisa Ugazi  Bagamoyo DC), Carolini Sichalwe (Afisa Utafiti Kilimo-MAFC-DRD, Kibaha) na John Banzi (Mchumi-MAFC-DRD HQ).
Tukiwa Chambezi, Bagaomoyo kituo kidogo cha Utafiti wa Kilimo

Mwaka mpya - Barabara ya Tunduma - Sumbawanga yakamilika