Monday, March 30, 2015

Bright Angels High School yazindua Bodi ya Shule

 Shule ya Sekondari ya Bright Angels iliyopo Kisemvule, wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani imezindua Bodi ya Shule mwezi Februari mwaka 2015. Bodi hiyo itasaidia menejimenti ya shule katika kupanga na kutekeleza mipango ya kuendeleza shule.




Monday, March 23, 2015

Tulipotembelea Kivule


Tupo Dar lakini wakati mwingine familia hazitembeleani. Jumamosi iliyopita familia yangu iliitembelea familia ya Dr. Julius Manandota  waliohamia Kivule hivi karibuni. Ni mara yangu ya kwanza kufika Kivule lakini familia ilifurahi kwa kweli ni sehemu nzuri na watu wa Dar wanajenga aiseh. Nilichokiana ni Jiji kuimarisha miundo mbinu hasa barabara pamoja na DAWASA  na TANESCO kupeleka huduma za maji na umeme.

Biashara matangazo

Hapa Tanzania  wanywaji wa bia laini wanaipenda sana bia iitwayo 'castle lite'  wanasema ni nzuri. Lakini kampuni ya bia inafanya prmotion babu kubwa ya bia hii kupitia njia mbalimbali kama gari hili la kusambaza bia linavyoonekana.

Peter Massawe - Daktari bingwa wa Vipando vya korosho

Sekta ya kilimo kuna madaktari bingwa waliobobea katika fani mbalimbali. Mmojawapo ni Dkt.Peter Massawe-Daktari Bingwa wa Vipando (Plant Breeder) aliyebobea katika zao la korosho. Massawe ni Mratibu wa Utafiti wa Taifa wa zao la korosho. Utafiti wa zao la korosho hapa nchini unaratibiwa katika kituo cha Utafiti cha Naliendele kilichopo mkoani Mtwara chini ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Idara ya Utafiti na Maendeleo. Mwaka huu  Kamati ya Taifa ya Mbegu imeidhinisha aina 24 za mbegu bora korosho chotara zilizotafitiwa na watafiti wa zao hilo chini ya uongozi wa Dkt.Massawe. Hongera Dkt. Massawe na timu yako.

Eti Linaitwa 'Zebra Rock'

Jiwe hili linavutia. Nimelipata kwenye ukurasa wa fb wa TANAP. Eti linaitwa 'Zebra Rock' linapatikana mkoani Kilimanjaro (waliokwisha panda mlima Kilimanjaro watanieleza ni wapi hasa jiwe hili liliko). Ni moja ya kivutio cha watilii. Hapa ukiwa mchoraji unaweza kuchora picha nyingi ukilitathmini kwa makini jiwe hili. Kinachonisikitisha ni kwamba limepewa jina eti 'Zebra Rock!'

Friday, March 13, 2015

Kilimo cha umwagiliaji-raha, tija

Jua linawaka si mchezo, mazao yamenyauka hasa mikoa ya Pwani. Kilimo cha kutegemea mvua si cha uhakika na hakina tija. Tukimwagilia, utakipenda kilimo na kitakupa tija.

Foleni ya Buguruni nayo!

Kinachokera ni dereva kama huyu mwenye haraka

Muonekano wa Buguruni

Jiji la Dar Es Salaam linajengeka kwa kasi ya kutisha. Hapa ni Buguruni. Hebu check kwa mbele hotel mpya ya NEW POPEX HOTEL.

Makeke ya uncle 'Junior'- The Davido

Leo asubuhi nimebahatika kumkuta uncle Junior nyumbani kwao Buguruni -Maghorofani akijiandaa kwenda shule . Makeke yake yalikuwa kama unavyoona pichani.
Alinionesha gari lake
Na hii ndiyo sare ya michezo shuleni kwako St Joseph Kindergarten

Alinionesha vidole vitatu sikufahamu maana yake

Umahiri wa kudaka mpira je? Huenda atakuwa goalkeeper wa Taifa Stars

Hakika mapenzi yake kwa football ni dhahiri na inawezekana anaipenda Barcelona!

Uliwadia wakati wa kwenda shule

Na hapa ndipo nilipomuelewa kuwa ni peace - Huenda ni CHADEMA!

Alinionyesha bag la shule lenye rangi ya njano! Kumechisha nini?

Inapotakiwa kwenda shule ni makeke mengi tu
Toys kibao kwa raha zake
Angekuwa na gari yake nadhani uncle Junior angeendesha kwenda shule!

TAZARA Sokoni-Mahakama ya ndizi

Ukitokea kituo cha mabas cha TAZARA kama unaelekea Temeke, jijini Dar kituo kinachofuata kinaitwa SOKONI. Soko hili ni maarufu kwa biashara ya ndizi mbivu wengine mahali hapa hupaita 'mahakama ya ndizi.' Kituo hiki kiko karibu na Makao makuu ya TAZARA na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. Leo asubuhi nimebahatika kununua ndizi moja nzuri kwa bei ya shilingi 150/= unajua nilinunua ngapi? Kumi na mbili (12).

Azam - Tazara

Ni asubuhi, barabara ya Mandela jijini Dar. Kwa mbali nayaona majengo ya Azam, zamani National Milling Coorporation. Imenikumbusha mbali wakati huo serikali ilipokuwa inamiliki shirika hilo la umma la usagishaji na usindikaji wa nafaka. Hapo ndipo ilipokuwa ikisindikiwa mikate mizuri tuliyokuwa tukiikimbilia kila inapoonekana na kupanga foleni.

Tujikumbushe kwa Babu-Samunge


Kumbukumbu na Baba wa Taifa

Hii ni kumbukumbu nzuri Dada Petty ( wa kwanza kulia)  mstari wa nyuma ukiwa na Baba wa Taifa Mwl. J.K.Nyerere  (Marehemu)  Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na mkewe Maria Nyerere (wa kwanza kushoto mstari wa nyuma). (Picha kwa hisani ya fb - Petty Mloka)

Wanaendesha gari wakiwa wadogo!

Uncles! Wakiwa wadogo wana ndoto ya kuendesha gari. Watakapokuwa wakubwa ni lazima wataweka priority ya kumiliki gari. (Picha kwa hisani ya fb-Petty Mloka)

Ni rahisi kujifunza kichina

Kwa wanaoishi wilaya ya Mkuranga hasa kijiji cha Kisemvule inawapasa kujifunza Kichina kwa bidii. (Picha kwa hisani ya fb-Petty Mloka)

NEW SEATBELT DESIGN

design kama hii ni kuwatesa abiria. Mimi siitaki! (Picha kwa hisani ya fb-Petty Mloka)

Si wote wanaofahamu Kiingereza

Je, ujumbe umefika? Tusijidanganye. Si wote wanaofahamu lugha ya kiingereza. (Picha kwa hisani ya fb-Petty Mloka)

Kiatu kimefichwa 'strategically'

Viatu vingi pichani ni vya watoto. Lakini mmoja ni mjanja zaidi. Kwa kuogopa kuibiwa angalia jinsi sandal ya pink ilivyowekwa juu ya kiatu. Ni mkakati ili kisionekane kirahisi na kuibiwa. Nadhani ana kumbukumbu ya kupoteza kiatu katika mazingira kama haya! (picha kwa hisani ya fb -Petty Mloka)

TWO THINGS

Nadhani ujumbe umefika (picha kwa hisani ya fb-Petty Mloka)

Jamani harusi hii ni pendeza sana

'Open air' wedding reception. Inapendeza sana.

Kali kutoka Urusi

Hizi zote ni pombe kali aina ya Vodka kutoka Urusi. Hiyo ya Yanga inaitwa Moskovskaya (Moscow Vodka) na hiyo ya kushoto  'Simba' inaitwa Stolichnaya Vodka. Kwa kweli zote kali ni moto! Jaribu uone

Hotel kwenye beach yetu ya Bahari ya Hindi


Umeshawahi kutembelea hoteli zilizoko kwenye ufukwe wa bahari ya Hindi Jiji Dar? Pendeza sana. Tembelea wewe na familia yako halafu tuandikie.

Wednesday, March 11, 2015

Wadau wa EAAPP wanavyoridhishwa na njia za kupata teknolojia

 'Eastern Africa Agricultural Productivity Project' (EAAPP) ni mradi unaolenga kuongeza uzalishaji na Tija kwenye Kilimo kwa nchi za Mashariki ya Afrika. Maradi huu unatekelezwa katika nchi 4 nazo ni Tanzania (Mpunga);Kenya(Ng'ombe wa Maziwa;Uganda (Muhogo) na Ethiopia(Ngano). Mazao yaliyo kwenye mabano yanaonyesha zao kuu linaloshughulikiwa katika nchi hiyo ambapo vituo mahiri vya mazao hayo vinaimarishwa (Regional Centres Of Excellence). Hapa Tanzania, kituo mahiri cha zao la mpunga kiko katika kituo cha Utafiti wa Kilimo-KATRIN, Ifakara. Moja ya viashiria vya mradi huu ni kupima kiwango cha wadau kuridhika na upelekekaji wa teknolojia za kilimo kwa kutumia njia tofauti kama vile radio,TV, vipeperushi,mafunzo na maonyesho ya kilimo. Kwa kuzingatia chart hiyo hapo juu, inaonyesha kuwa wadau hadi kufikia mwaka huu (2015) wadau wameridhika kwa asilimia 67 ukilinganisha na asilimia 20 iliyokuwepo mwaka 2010.Haya ni mafanikio makubwa.

Hawa waling'ara tarehe 8/3/2015

Kutoka kushoto Ajibu, Okwi na Ndemla. Wachezaji hawa wasimba waling'ara siku ya mechi ya Simba na Yanga tarehe 8/3/2015 ambapo Simba iliibuka na ushindi wa goli 1-0 lililofungwa na Emmanuel Okwi. Kwa ushindi huo Simba sasa iko nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi 2015 wakiwa na pointi 26 huku Young Africans ikiongoza kwa point 31.

Kuponivic-Yametimia

Kocha wa Simba Goran Kopunivic akimshukuru Mungu baada ya mchezo wa Simba na Yanga kumalizika na Simba kuibuka kidedea siku ya tarehe 8/3/2015 kwa ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Emmanuel Okwi ndani ya uwanja wa Taifa.

Kelvin Yondani hamuwezi Okwi

Tarehe 8 Machi 2015 siku ya Wanawake duniani, wapenzi wa soka nchini walishehrekea ki aina yake. Ndiyo siku ambayo mchezo wa DAR DERBY (Simba Vs Yanga). Matokeo Simba iliiadhibu Yanga kwa bao 1-0.Pichani Emmanuel Okwi akimpita kirahisi beki wa Yanga Kelvin Yondan.

Hapa ni Morogoro-Msamvu

Ni zaidi ya wiki moja tangu mvua kali inyeshe mjini Morogoro na kuzua tafrani. Majani yameanza kuchipua vizuri na kuupendezesha mji wa Morogoro. Hapa ni Msamvu kuelekea keepleft cha Msamvu kwenye kituo kikubwa cha mabus ya abiria kwenda mikoa ya nje ya Morogoro.

Monday, March 9, 2015

Hotel Mpya -Morogoro

Hotel hii mpya iko kando ya barabara ya Morogoro eneo la Viwanja vya NANENANE

Hiki ni kituo cha mabus ya kwenda Mikoani cha Msamvu-Morogoro


Jahazi Taarabu inajua kujitangaza

Sikukuu ya Wanawake  ( 8 Machi) mwaka huu ilifanyika kitaifa  mjini Morogoro. Jahazi walikuwepo huko. Angalia wanavyojitangaza. Hawa ndiyo Jahazi. Hapa ni Masika mjini Morogoro. Wengi watalisoma tangazo na nafikiri wengi walikwenda kuwaona wanajahazi wakitumbuiza.

Miwa ya kutafuna

Hapa ni Kingolwira, Morogoro. Miwa inauzwa. Hii ni miwa ya kutafuna. Kuna aina mbili za miwa.Moja ni ile ya kutafuna na ile inayotumika kutengeneza sukari. Kwa kawaida miwa ya kutengeneza sukari ni miyembamba na migumu. Miwa ya kutafuna ni laini. Hii imenikumbusha wakati nikisoma shule ya msingi nyumbani Matombo wakati wa mapumziko wanafunzi tulikuwa tukitafuna miwa kwa sana tu hadi matumbo kujaa maji mengi ukikimbia yanalia-kubwakubwkubwakubwa. Ha Moro ina kila kitu.

Tulipishana na trekta

Wakati tulipokuwa tukielekea Moro tulipofika Kingolwira, tulipishana na trekta. Hii inaashiria tunaingia mkoa wa kilimo na pia wenye kutumia zana bora za kilimo yakiwemo matrekta. Morogoro ghala la mazao la Taifa.

Iliyokuwa Abood Soap Industries-Moro


Hapa ni Msamvu Morogoro, ndipo kilipokuwa kiwanda cha kutengeneza sabuni za 'Abood Soap'. Sabuni hizi zilikuwa maarufu si kwa Moro tu bali nchi nzima. Utengenezaji wa sabuni hizi umesitishwa miaka mingi iliyopita. Kilichobaki ni majengo na sidhani kama mitambo bado ipo (sijaingia ndani ya kiwanda). Abood mwenyewe sijui anasema nini kuhusu kiwanda chake. Wakazi wa Moro waliokuwa wakifanya kazi kwenye kiwanda hiki sasa hawana ajira kwa hiyo familia zilizokuwa zikitegemea kiwanda hiki kwa kipato zimeathirika sana.