Tuesday, June 21, 2016

Kilimo cha bamia kama ufugaji wa kuku wa mayai!

Kitu ambacho nilikuwa sifahamu ni jinsi unavyoweza kuvuna bamia. Bamia linaweza kuvunwa mara mbili kwa siku, asubuhi na jioni. Kuna mtu ameninong'oneza. Bamia wakati wowote hukua, tena kwa haraka ukichelewa linakomaa na hivyo kuwa gumu na kutofaa kuliwa kama mboga labda kulitunza kwa mbegu.Hivi sasa navuna bamia katika sehemu ndogo niliyolima pale nyumbani kwangu Kisemvule. Kweli kilimo cha bamia ni kama ufugaji wa kuku wa mayai.