Wednesday, September 28, 2016

Hili ni group langu nililosoma nalo nchini Urusi

Hili ni group langu la masomo nilipokuwa nchini Urusi kwa masomo yangu.Katika Group hili nawakumbuka wachache kwa majina hasa hao waafrika kutoka kushoto Mamadu (Mali) Mohamed Barrie (Sierra Leone), Mansary (Sierra Leone) na Alex Konte (Siera Leone). Mimi niko mkono wa kushoto wa Mamadu. Hapa ilikuwa ni Crimea, Simferopol mwaka 1989. Nadhani wa kwanza kushoto ni Kutryova na kushoto kwangu ni Svetlana.

Huyu ndiye Ibrahim Ajibu wa Simba

Ibrahim Ajibu wa Simba Sports Club (Nyekundu) akiruka kiunzi wakati wa mpamboa wa klabu yake na AFC-Leopards kutoka Kenya-Tarehe 8/8/2016 katika uwanja wa Taifa, Dar Es Salam. Leopards ilala 4-0. Ni katika kuadhimisha miaka 80 tangu kuanzishwa kwa klabu ya Simba ninayoipenda mimi!

Bright Angels-High School ziara ya mafunzo-Mafia

Wanafunzi wa Bright Angels High School iliyopo wilayani Mkuranga, Mkoa wa Pwani wakiwa katika ziara ya mafunzo huko Mafia wakiangalia mabwawa ya kutengeneza chumvi.

Miaka 80 ya Simba Sports Club nilikuwepo uwanjani

Nilikuwepo uwanjani pamoja na mashabiki lukuki wa Simba nikimshuhudia mnyama akimrarua AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 kwenye uwanja wa Taifa, Jijini Dar Es Salaam. Wote tukiimba kila mtu 'Mavugooo'. Mchezaji huyu wa Kimataifa kutoka Burundi,  Laudit Mavugo alitupia bao katika mechi yake ya kwanza akiichezea SSC. Ilikuwa raha sana. Nimeweka kumbukumbu ya kuhudhuria mechi ndani ya uwanja wa Taifa wakati Simba inatimiza miaka 80 tangu ianzishwe.

Thursday, September 22, 2016

Milima ya Nyingwa-Matombo-Morogoro

Hii ni milima ya Nyingwa, Matombo-Morogoro

Matombo-Lanzi

Mandhari mazuri ya kijiji cha Lanzi,Kibungo, Matombo, Morogoro. Angalia mgahawa kando ya barabara. Kwetu kuzuri.

Hii ndiyo Kamati ya Harusi

Ukisikia kamati ndiyo hii. Hongera!

Maharusi wamechagua kibanda wazi

Hawa ni wadogo zetu Waluguru kutoka Matombo Kiswira waliofunga ndoa hivi karibuni. MC alikuwa Richie Paschal. Kwa mujibu wa Richie harusi ilifana sana.

MC. Mluguru Richie Paschal Solaga

Kwa Waluguru wanaotaka shughuli zao ziendeshwe kwa lugha ya Kiluguru basi itabidi umtafute MC. Richie Paschal Solaga. Ana  kipaji cha hali juu na anajua kuchangamsha shughuli. Hata kama si kwa Kiluguru yupo vizuri sana kwani anajua vikorombwezo. 

Kunywa maziwa kutoka Meatu

Nadhani somo limeeleweka na limekubalika. Mkuu wa Mkoa wa Shimiyu Mhe. Anthony Mtaka akionyesha  maziwa ya Meatu. Hakika inafurahisha na inapendeza. Cha kufurahisha Maziwa hayo yanatengenezwa na mradi wa vijana. Hivyo ni moja ya vyanzo vya ajira na mapato kwa vijana.(Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

Tutumie vya kwetu- Chaki kutoka Maswa

Mkoa wa Simiyu umeanza kutengeneza chaki kutoka Maswa. Tupende na kutumia vya kwetu. Inakuwawaje hata chaki tuagize kutoka nje? Pichani Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  Mhe. Anthony Mtakwa akishangaa Chaki kutoka Maswa mali ya Tanzania.

Thursday, September 15, 2016

Unapoitaja Matombo unagusa matunda na machenza

Machungwa na machenza ya Matombo, Morogoro ni matamu sana. Tatizo wafanyabiashara wameingilia kati biashara hii na kuyauza machenza na machungwa wakati bado hayajafikia kukomaa kibailojia (Yanakomaa yakiwa mtini). Kibaya zaidi huchanganya machungwa au machenza mazuri na mabaya. Mlaji akibahatika hula chenza tamu na ikiwa hana bahati unaweza kula chenza chungu. Hii ni kuharibu biashara na umaarufu wa machungwa au machenza ya nyumbani Matombo. Kwa kawaida machungwa huanza kuvunwa kuanzia mwezi machi hadi Juni.

Athari ya Tetemeko la Ardhi Bukoba

Tetemeko la Ardhi lililotokea Bukoba.Baadhi ya nyumba za Ibada zimeathirika.Kanisa Katoliki Ihungo limeharibiwa vibaya. Poleni sana wenzetu wa Bukoba.(Picha kwa hisani ya ukurasa wa fb. Askofu Method Kilaini).

Tuangalie ugonjwa wa nyanya kuoza kitako (Blossom endrot)


Baadhi ya wakulima wa nyanya wamekuwa wakipata tatizo la nyanya zao kuungua chini ya kitako na kuharibu kabisa ubora wa nyanya hizo. Wanataalamu wanatueleza kuwa ugonjwa huo unaitwa kuoza kitako (Blossom endrot). Hii husababishwa na mmea kukosa maji ya kutosha au kutofuata ratiba ya umwagiliaji kwa zao hilo.Unakuta siku nyingine unamwagilia asubuhi siku nyingine mchana au unamwagilia Jumamosi halafu unarudia tena kumwagilia siku ya Jumanne huko ndiko kutozingatia ratiba ya umwagiliaji. Hiki ndicho chanzo kikuu cha ugonjwa huo wa kuoza kitako.
 
 TIBA

Ondoa matunda yote yaliyo athirika halafu anza kufuata na kuzingatia ratiba ya umwagiliaji wa shamba lako.
(Hii nimeinyaka kutoka fb wafanyakazi wa kilimo Mifugo na uvuvi na kuikarabati kidogo na kuirusha kwani ni wengi wanalima nyanya na hasa na kuwaona wanamwagilia maji kiubabaishaji tu).

Wednesday, September 14, 2016

Bus la Yutong la Wachina

Hili ni bus la Yutong la kutoka Uchina. Utawapenda tu. Wachina ni wazuri kwa teknolojia.  Hutengeza kuteka matakwa ya mdau. Hapa Tanzania kwa sasa naweza kusema kuwa asilimia 80 ya mabus ni  ya Kichina. Inasemekana ni bei poa ukilinganisha na mabus aina ya Scania au Marcopolo. Kingine wanachofanya  Wachina ni kuongeza thamani ya bidhaa. Ukipanda mabus yao yalivyorembwa na kuwekewa vikorombwezo vingine hakika hutoacha kulipanda tena. Sisi tutaanza lini kuunda mabus yetu?

Nani Zaidi?


Haya ni machenza kutoka Matombo - Morogoro

Machungwa na machenza ya Matombo, Morogoro ni matamu sana. Tatizo wafanyabiashara wameingilia kati biashara hii na kuyauza machenza na machungwa wakati bado hayajafikia kukomaa kibailojia (Yanakomaa yakiwa mtini). Kibaya zaidi huchanganya machungwa au machenza mazuri na mabaya. Mlaji akibahatika hula chenza tamu na ikiwa hana bahati unaweza kula chenza chungu. Hii ni kuharibu biashara na umaarufu wa machungwa au machenza ya nyumbani Matombo. Kwa kawaida machungwa huanza kuvunwa kuanzia mwezi wa Machi hadi Mei.

Kumbukumbu harusi ya uncle Sophy Mluge

Ushiriki wa madada na makaka kwenye harusi hii iliyofanyika mjini Morogoro  ulikuwa wa hali ya juu. Hii ni kumbukumbu ya zaidi ya miaka miwili iliyopita.

Nimeikumbuka shule yangu ya Msingi Matombo

Nimeikumbuka shule yangu ya Msingi Matombo. Hivi sasa ni shule ya Sekondari Matombo. Kuna mchakato unaoendelea kuifanya iwe High School (Form I-VI) haya ni mabadiliko makubwa.Kitu kimoja nakumbuka nilikuwa mpiga kengele.