
Idara ya utafiti na Maendeleo iliyoko Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeweka utaratibu mzuri wa kupelemba na kutathmini shughuli za utafiti katika kanda zake saba za utafiti ili kuweza kufahamu utekelezaji wa mipango ya utafiti ufanisi, changamoto na kuweka mikakati ya kupambana na changamoto zinazojitokeza. Pichani wanaonekana wapelembaji waliotumwa kanda ya kaskazini mwezi Juni 2010.