Siku ya tarehe 13/12/2008 Jumamosi itakuwa siku ya kumbukumbu kubwa kwa Doreen, familia yake, ndugu na majamaa wakati alipotunukiwa shahada ya Uzamivu (PhD) katika tiba. Pichani kushoto Dr. Doreen ndani ya joho la Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUCHS) katika hisia kali. Kulia ni Professor Nuhunoli (naomba nisahihishwe jina sahihi) aliyetunukiwa shahada ya Udaktari wa Sayansi. Kutokana na maelezo niliyoyapata kutoka kwa wasomi, hii ni tuzo ya juu kabisa.
Wednesday, December 17, 2008
Friday, December 5, 2008
Shibuda atagombeaje urais katika mlango mmoja ?
Conges Mramba katika makala yake kwenye gazeti la Rai (Mraba wa Mramba) tarehe 4-10 Desemba amekuja na kichwa cha habari CCM: Damu ya kijani au geresha? Ndani ya makala hiyo ameandika mambo mengi ya kutafakari kuhusu CCM na mambo yanavyokwenda kwenye chama hicho tawala.
Binafsi nimefurahishwa na hili. Nanukuu- " Shibuda atagombeaje urais katika mlango mmoja unaoandaliwa kwa rais aliyepo madarakani? Tafakari.
Binafsi nimefurahishwa na hili. Nanukuu- " Shibuda atagombeaje urais katika mlango mmoja unaoandaliwa kwa rais aliyepo madarakani? Tafakari.
Mfumuko wa bei ni aslimia milioni 230- Siamini!
Hivi kweli mfumuko wa bei Zimbabwe ni asilimia milioni 230! Mbona siamini, nashindwa kupata picha. Mimi ni mchumi, hiyo asilimia milioni 230 nashindwa kuipresent kwa kweli. Hivi Wazimbabwe wanaishije huko? Kuna tatizo na si dogo. Tuwasaidie ndugu zetu Wazimbabwe.
"Utaratibu tuliojiwekea" maana yake nini?
Siku hizi mambo yanapokiukwa utasikia kwa "utaratibu tuliojiwekea."
Kama kanuni, sheria na taratibu zipo kwanini tuwe na kitu mbadala- "Utaratibu tuliojiwekea" hapa ndipo tunapoanza kuharibu mambo. Na ndipo haki inapopindwa.
Kama kanuni, sheria na taratibu zipo kwanini tuwe na kitu mbadala- "Utaratibu tuliojiwekea" hapa ndipo tunapoanza kuharibu mambo. Na ndipo haki inapopindwa.
Hivi unafahamu kiswahili cha "White Elephant?"
Usipoteze wakati wako utauumiza kichwa bure! White elephant ni - Geresha (Gheresha).
Quote from Rio Ferdinand
Rio Ferdinand is a dependable centrehalf of the Manchester United Football Club of England.
I was moved with his words from the article published on the Daily News of last Friday 27/11/2008.
I quote - "Outside of Sport it would be Nelson Mandela for all he's achieved. He's devoted his life to his nation."
"It would be great if Nelson Mandela was the person who handed us a cup. There's no better man in the world to do that and tha's something to work towards, but there is a very long way to go yet."
Aliyasema haya alipokuwa akiuulizwa anafikiriaje kuhusu klabu bingwa ya dunia?
I was moved with his words from the article published on the Daily News of last Friday 27/11/2008.
I quote - "Outside of Sport it would be Nelson Mandela for all he's achieved. He's devoted his life to his nation."
"It would be great if Nelson Mandela was the person who handed us a cup. There's no better man in the world to do that and tha's something to work towards, but there is a very long way to go yet."
Aliyasema haya alipokuwa akiuulizwa anafikiriaje kuhusu klabu bingwa ya dunia?
Dereva Taxi wa aina hii ni wachache
Si rahisi ukasahau kitu kwenye Taxi na hatimaye akakipata. Lakini wako madereva taxi wanaoheshimu kazi zao na wanaopedna kulinda soko.
Dereva Taxi aliyanipeleka Jomo Kenyatta International Airport hivi karibuni ni muungwana kwani baada ya kushusha mkoba wangu kumbe nilidondosha "highlighter" (kalamu kubwa ya rangi ya kuweka msisitizo) ndani ya gari. Alipoiona alisimamisha gari na kunipatia kalamu hiyo. Dereva wa aina yake ni wa chache. Nakushukuru na umependisha chati madereva Taxi wa Kenya ingawa si wote. Asante sana.
Dereva Taxi aliyanipeleka Jomo Kenyatta International Airport hivi karibuni ni muungwana kwani baada ya kushusha mkoba wangu kumbe nilidondosha "highlighter" (kalamu kubwa ya rangi ya kuweka msisitizo) ndani ya gari. Alipoiona alisimamisha gari na kunipatia kalamu hiyo. Dereva wa aina yake ni wa chache. Nakushukuru na umependisha chati madereva Taxi wa Kenya ingawa si wote. Asante sana.
Ulemavu si hoja
Niko Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Jomo Kenyatta nikisubiri ndege yakunirudisha nyumbani Dar. Jirani yangu yuko mama mmoja wa kizungu (baadaye nakajakugundua kuwa ni Mswede) yuko "busy" na laptop yake na kifaa kingine (sikijui). Nashangaa nagundua kuwa ni kipofu lakini ana jamaa zake wawili alioandamana nao.
Baadaye nagundua kuwa naye anasafiri kuelekea Tanzania tena Morogoro. Nilifahamu hivyo baada ya kusikia mazungumzo yao na yule Mmasai kutoka Twatwatwa, Kilosa na mama mmoja kutoka Sudan. Mama huyu licha ya kutoona alikuwa na vifaa vya kisasa vinavyomsaidia kuendesha shughuli zake kama vile kutumia kompyuta. Na wakati akizungumza huwezi kugundua kama ni kipofu, ufahamu wake ulikuwa ni wa hali ya juu. Ama kweli Ulemavu si hoja.
Baadaye nagundua kuwa naye anasafiri kuelekea Tanzania tena Morogoro. Nilifahamu hivyo baada ya kusikia mazungumzo yao na yule Mmasai kutoka Twatwatwa, Kilosa na mama mmoja kutoka Sudan. Mama huyu licha ya kutoona alikuwa na vifaa vya kisasa vinavyomsaidia kuendesha shughuli zake kama vile kutumia kompyuta. Na wakati akizungumza huwezi kugundua kama ni kipofu, ufahamu wake ulikuwa ni wa hali ya juu. Ama kweli Ulemavu si hoja.
Vijana wakiafrika sasa hufanya biashara nchi mbalimbali
Kuchelewa kuondoka uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyata siku ya tarehe 26 Novemba 2008 kumenifanya nijifunze mengi.
Wakati nilipokuwa napata chakula cha mchana cha kuponi pale uwanjani (kutokana na kucheleweshwa) niliwaona vijana wengi wake kwa waume. Nilibahatika kumuuliza mmoja wao anatokea wapi alinijibu anatoka Nigeria na anelekea Bangkok kwa shughuli ya biashara. Kwenye meza nilizunguukwa na vijana wanne waliokuwa wakizungumza kifaransa nao wako kwenye pilika ya safari za kibiashara. Nilishindwa kudodosa zaidi nijue ni biashara ya aina gani wanayofuata huko Bangkok. Sote tulikuwa tunasubiri chakula!
Wakati nilipokuwa napata chakula cha mchana cha kuponi pale uwanjani (kutokana na kucheleweshwa) niliwaona vijana wengi wake kwa waume. Nilibahatika kumuuliza mmoja wao anatokea wapi alinijibu anatoka Nigeria na anelekea Bangkok kwa shughuli ya biashara. Kwenye meza nilizunguukwa na vijana wanne waliokuwa wakizungumza kifaransa nao wako kwenye pilika ya safari za kibiashara. Nilishindwa kudodosa zaidi nijue ni biashara ya aina gani wanayofuata huko Bangkok. Sote tulikuwa tunasubiri chakula!
Kenya Airways huchelewa pia
Ndege KQ 482 kutoka Nairobi kuelekea Dar Es Salaam ilikuwa iondoke saa 6:45 mchana Jumatano tarehe 26/11/2008. Lakini haikuweza kuondoka hadi saa 12.30 jioni. Lo! Kumbe hata KA nayo huchelewa?
Unapokutana na mfugaji kutoka Twatwatwa ukiwa Nairobi
Adam Ole Mwarabu ni mfugaji kutoka kijiji cha Twatwa, Kilosa, Morogoro. Kijiji hiki ni maarufu kwa mapigano kati ya Wafugaji (Wamasai) na wakulima. Adam ni Mmasai. Hivi karibuni nilikutana na Adamu uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JomoKenyatta Jijini Nairobi wakati tukisubiri ndege ya kurudi nyumbani Tanzania (Dar Es Salaam). Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukutana na Adam. Huku akivalia lubega na kubeba "laptop" yake ni lazima utajiuliza kimoyomoyo hivi Mmasai anaweza kutumia Laptop?
Adam, ni Mmasai aliyendelea. Amesafiri nchi nyingi hapa duniani kuliko wengi wetu. Amehudhuria mikutano mingi ya kimataifa na wakati nilipokutana naye alikuwa anatokea Ubalozi wa Poland kuchukua Visa.
Adam ni Mratibu wa NGO inayooitwa PAKODEO (nitamuuliza kirefu chake). NGO hii hujishughulisha zaidi na masuala ya ardhi, mifugo, elimu, mazingira na jinsi ya kupambana na HIV-AIDS.
Adam hazungumzii zaidi kuhusu mapigano ya wakulima na wafugaji anasema ni ya kisiasa zaidi na viongozi hawako makini katika kutatua tatizo.
Adam, ni Mmasai aliyendelea. Amesafiri nchi nyingi hapa duniani kuliko wengi wetu. Amehudhuria mikutano mingi ya kimataifa na wakati nilipokutana naye alikuwa anatokea Ubalozi wa Poland kuchukua Visa.
Adam ni Mratibu wa NGO inayooitwa PAKODEO (nitamuuliza kirefu chake). NGO hii hujishughulisha zaidi na masuala ya ardhi, mifugo, elimu, mazingira na jinsi ya kupambana na HIV-AIDS.
Adam hazungumzii zaidi kuhusu mapigano ya wakulima na wafugaji anasema ni ya kisiasa zaidi na viongozi hawako makini katika kutatua tatizo.
Tuesday, November 25, 2008
Utekelezaji mbovu Afrika ndo unaotufanya tusifikie malengo
Jana katika hotel ya Intercontinental hapa Nairobi, Kenya tulikuwa tunajadili masuala ya "kupelemba na kutathmini" (Monitoring and Evaluation) kwenye utafiti wa Kilimo.
Imedhihirika kuwa tuna mipango mizuri yenye malengo mazuri. Na malengo yetu makuu kwnye nchi hizi za Afrika Mashariki na ya Kati kwa bahati nzuri ni ya muda mrefu sana kama vile kuondoa umaskini, ujinga, maradhi lakini hadi hii leo tunazungumzia hayo hayo tokea tupate UHURU. Korea ya Kusini walikuwa kwenye hali kama yetu miaka 40 iliyopita sasa wameshatoka. India sasa wanajitosheleza kwa chakula! Sisi misaada, misaada misaada!
Imedhihirika kuwa tuna mipango mizuri yenye malengo mazuri. Na malengo yetu makuu kwnye nchi hizi za Afrika Mashariki na ya Kati kwa bahati nzuri ni ya muda mrefu sana kama vile kuondoa umaskini, ujinga, maradhi lakini hadi hii leo tunazungumzia hayo hayo tokea tupate UHURU. Korea ya Kusini walikuwa kwenye hali kama yetu miaka 40 iliyopita sasa wameshatoka. India sasa wanajitosheleza kwa chakula! Sisi misaada, misaada misaada!
Eti sisi Waafrika ni wabaguzi zaidi kuliko wazungu?
Kuna baadhi ya watu wanasema kuwa Obama kuwa Rais Amerika ni rahisi zaidi kuliko Clinton kuwa Rais wa Kenya! Wanasema kuwa sisi Waafrika ni wabaguzi zaidi kuliko wazungu je ni kweli?
Monday, November 24, 2008
Huduma za Hotelini Kenya ni zaidi
Ukiwa Hotelini Nairobi Kenya, huduma nyingi zinapatikana ikiwamo hii ya Internet. Hapa nilipo nimeweza kuwasiliana nanyi kwa kutumia "Wireless internet connection" huna haja ya kuonana na mtu anayekupa hiyo huduma. Upo chumbani kwako unapiga simu na unapata huduma kwa maelekezo.Malipo baadaye na ni malipo nafuu.
Hee, hata kama mimi ni mtalii ningeweza kupendelea kwenda Kenya. Hivi vitu vinawezekana kwetu pia. Nafahamu huduma hizi zipo kwetu lakini hazijaenea kwa kiasi cha kutosha lakini inawezekana. Tunapoteza hela nyingi kwenye sekta ya mawasiliano tumeng'ang'ania simu za mkononi tu. Wenzetu wanahama taratibu!
Hee, hata kama mimi ni mtalii ningeweza kupendelea kwenda Kenya. Hivi vitu vinawezekana kwetu pia. Nafahamu huduma hizi zipo kwetu lakini hazijaenea kwa kiasi cha kutosha lakini inawezekana. Tunapoteza hela nyingi kwenye sekta ya mawasiliano tumeng'ang'ania simu za mkononi tu. Wenzetu wanahama taratibu!
Nikiwa Kenya niko Nyumbani
Nairobi, watu wake, miti yake na udongo wake ni kama Arusha tu. Isitoshe Wakenya wanaongea na kukipenda Kiswahili tofauti na jinsi Watanzania wengi wanavyohisi kuhusu Wakenya. Kwa kweli ukiwa Kenya unajisikia nyumbani. Utasikia watu wanakusalimia habari mzee. Wanasema yule "demu" ameondoka. Wanakuambia bia baridi ndiyo yenyewe. Wageni wengi wangependa kufahamu na kuzungumza Kiswahili wakiwa Kenya. Watanzania mpo?
Nairobi nayo inatatizo ya “traffic jam”
Mara baada ya kutua Jomo Kenyata International Airport na kuelekea Intercontinental Hotel, katikati ya jiji la Nairobi, tunapambana na Traffic jam kubwa. Pamoja na kuwa na barabara nyingi na zile zinazokatisha juu, lakini bado jiji la Nairobi lina tatizo la Traffic jams!
Kumbe si Dar tu. Kama hakuna utaratibu mzuri, kuwa na barabara nyingi na pana hakuwezi kumaliza tatizo la "traffic jam" katika miji yetu.
Kumbe si Dar tu. Kama hakuna utaratibu mzuri, kuwa na barabara nyingi na pana hakuwezi kumaliza tatizo la "traffic jam" katika miji yetu.
Kweli inawezekana watoto wasiwe wa kwako
Nipo hapa Intercontinental Hotel Nairobi, Kenya. Nimekutana na wasomi kutoka Kenya, Uganda, Eriteria, Burundi na Rwanda. Siku ya leo tumezungumzia sana kuhusu kilichotuleta hapa Kenya hasa kuhusu masuala ya "Kupelemba na Kutathmini "( Monitoring and Evaluation)shughuli za Utafiti, Ugani na Mafunzo katika eneo hili la Afrika ya Mashariki na ya Kati.
Mazungumzo nje ya hilo yanagusa masuala mbalimbali.Lakini kwa kuwa ni watu wazima na tupo jinsi mbili tunazungumza yanayotuhusu katika maisha yetu ya kila siku. Katika hilo lililochukua muda mwingi ni mahusiano ya ndoa. Imebainika kuwa mwanamke anaweza kubeba siri kubwa kuhusu baba halisi wa watoto. Je hili mnalionaje wana mtandao?
Mazungumzo nje ya hilo yanagusa masuala mbalimbali.Lakini kwa kuwa ni watu wazima na tupo jinsi mbili tunazungumza yanayotuhusu katika maisha yetu ya kila siku. Katika hilo lililochukua muda mwingi ni mahusiano ya ndoa. Imebainika kuwa mwanamke anaweza kubeba siri kubwa kuhusu baba halisi wa watoto. Je hili mnalionaje wana mtandao?
Taxi za njano
Ukitua uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi utakutana na magari mengi sana ya aina mbalimbali na mazuri kwa kusema ukweli. Hata hivyo magari madogo ya abiria yaliyopakwa rangi ya njano yanavutia zaidi hapo uwanjani (Lakini si magari ya Dar Young Africans). Magari hayo ni utambulisho kuwa ni zile Taxi zinazo park uwanjani hapo na ubavuni kuandikwa JKIA. Magari hayo ni masafi yanavutia na yana utaratibu mzuri kwa abiria. Ni vizuri kwa Taxi za zinazo park Dar- Mwl. Julius Nyerere International Airport zikaiga utaratibu huu na kuwa na nauli zakuridhisha kwa wateja na si kuwatega watejawaingizwe king! Kipato hakipatikani kwa ujanja ujanja! Tuwe wastaarabu na tuvute wateja kwa mambo mazuri.
Watanzania tulishapita hatua ya Waamerika
Niko hapa Nairobi Kenya, nimetoka kwenye "reception dinner" iliyoandaliwa na wenyeji wetu ASARECA kwenye warsha hii ya "Kupelemba na Kutathmini" miradi ya ASARECA.
Kwa faida ya wale ambao hawaifahamu ASARECA. Huu ni chombo cha Afrika mashariki na Kati kinachoangalia masuala ya Utafiti, Ugani na Mafunzo Katika Kilimo.
Ndugu zangu wa Kenya wamekiri kuwa hakuna cha kushangaza kuhusu Obama kuwa Rais wa Amerika. Watanzania wameshapita hatua hiyo siku nyingi. Wanaeleza wenyewe kuwa kwa Tanzania hawakuwa na sababu ya kufahamu kuwa Mkapa alikuwa anatoka wapi. Walichotaka ni kuwa na Rais atakayeweza kuisimamia nchi ya Tanzania. Watanzania tupige makofi basi kuwa tunawazidi hata Waamerika kwa hilo. Lakini kwa nini hatupigi hatu kwenye Maendeleo?
Kwa faida ya wale ambao hawaifahamu ASARECA. Huu ni chombo cha Afrika mashariki na Kati kinachoangalia masuala ya Utafiti, Ugani na Mafunzo Katika Kilimo.
Ndugu zangu wa Kenya wamekiri kuwa hakuna cha kushangaza kuhusu Obama kuwa Rais wa Amerika. Watanzania wameshapita hatua hiyo siku nyingi. Wanaeleza wenyewe kuwa kwa Tanzania hawakuwa na sababu ya kufahamu kuwa Mkapa alikuwa anatoka wapi. Walichotaka ni kuwa na Rais atakayeweza kuisimamia nchi ya Tanzania. Watanzania tupige makofi basi kuwa tunawazidi hata Waamerika kwa hilo. Lakini kwa nini hatupigi hatu kwenye Maendeleo?
Friday, November 14, 2008
Habari na Mawasiliano ni nyenzo muhimu katika Kilimo
Mwezi Septemba mwaka 2008 nilibahatika kuhudhuria warsha ya wadau wa habari na mawasiliano katika sekta ya Kilimo kutoka nchi za SADC iliyofanyika nchini Botswana, jijini Gaborone.
Nchi 14 ukiondoa Afrika ya Kusini zilishiriki warsha hiyo iliyokuwa na dhumuni la kuona jinsi gani nchi za SADC zinavyoweza kuwasiliana na kutumia tekenoljia ya habari, katika
masuala mbalimbali ya kilimo kwa kutumia vyombo mbalimbali kwa kuzingatia wadau.
Wakati umefika sasa wa kukitangaza kilimo kama vile inavyotangazwa " cocacola" lakini mawasiliano hayo ni vyema yakawaongezea maarifa wadau wetu wa kilimo. Tunataka kilimo chenye kumnufaisha mkulima.
Kuna mambo mazuri yanayofanyika katika nchi hizi ambazo yanawezwa kuigwa na nchi nyingine lakini hayafahamiki. Kuna matukio muhimu yanayotokea katika sekta ya kilimo lakini yanabakia palepale. Basi ilionekana kuwa kuna umuhimu wa kila nchi kuangalia jinsi ya kutumia taarifa, mawasiliano na teknolojia ya habari katika kuboresha sekta hii.
Wakati viongozi wetu wanapiga kelele na kuhamasisha uzalishaji katika kilimo, habari na mawasiliano ni nyenzo muhimu itakayosaidia kuboresha kilimo chetu. Pichani wanaonekana washiriki wa warasha hiyo.
Nchi 14 ukiondoa Afrika ya Kusini zilishiriki warsha hiyo iliyokuwa na dhumuni la kuona jinsi gani nchi za SADC zinavyoweza kuwasiliana na kutumia tekenoljia ya habari, katika
Wakati umefika sasa wa kukitangaza kilimo kama vile inavyotangazwa " cocacola" lakini mawasiliano hayo ni vyema yakawaongezea maarifa wadau wetu wa kilimo. Tunataka kilimo chenye kumnufaisha mkulima.
Kuna mambo mazuri yanayofanyika katika nchi hizi ambazo yanawezwa kuigwa na nchi nyingine lakini hayafahamiki. Kuna matukio muhimu yanayotokea katika sekta ya kilimo lakini yanabakia palepale. Basi ilionekana kuwa kuna umuhimu wa kila nchi kuangalia jinsi ya kutumia taarifa, mawasiliano na teknolojia ya habari katika kuboresha sekta hii.
Wakati viongozi wetu wanapiga kelele na kuhamasisha uzalishaji katika kilimo, habari na mawasiliano ni nyenzo muhimu itakayosaidia kuboresha kilimo chetu. Pichani wanaonekana washiriki wa warasha hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)