Wednesday, August 4, 2010

Huwezi kuamini kuwa hawa wamebwagwa!


Ndiyo, Shamasa Mwangunga, Dr.Mwamtumu Mahiza na Alfred Tibaigana wamebwagwa katika kinyang'anyiro cha kuwania ubunge kupitia CCM.

Hakuna sababu ya kuogopa HISABATI


WANAFUNZI walio wengi wanaogopa hesabu kwa sababu hawapati msingi mzuri. HISABATI si somo gumu kama mwanafunzi atafundishwa na mwalimu anayejua kufundisha na kulielewa somo la hesabu.Ili uweze kukotoa vizuri lazima ufahamu kanuni za hesabu. HESABU HUENDA NA KANUNI (FORMULAE)!

Utaratibu mzuri wa kupanda mabus ya wanafunzi unahitajiwa


NDIYO, Bank ya CRDB imetoa mabus machache kwa ajili ya wanafunzi wa jiji la Dar Es Salaam. Pamoja na kuwa na mabus hayo bado wanafunzi hugombania wakati wa kupanda mabus hayo. Kwanini kusiwepo utaratibu mzuri wa kuingia kwenye mabus hayo? Njia rahisi ni kwa wanafunzi kujipanga katika mstari. Aliyewahi ndiye atakuwa wa kwanza kupanda gari. Wanafunzi mkifanya hivi hata abiria wengine wataiga kwenye vituo vya mabus. Mnapogombania bus kuna hatari ya kuchana sare zenu za shule, kuchafuka, kuibiwa, kuchana vitabu na madaftari na wakati mwingine hata kuumia na kuzua ugomvi usio na sababu.

Nililipenda somo la Baiolojia


Somo la Baiolojia ndilo lililonipeleka kwenye sekta ya KILIMO.Nililifanya vizuri nikiwa "O" Level na kunipeleka "A" Level. Kutoka "A" nikaenda kusomea Crops Production (Diploma) kule Ukiriguru - MWANZA.Baadaye kwenye elimu ya juu nikabobea kwenye UCHUMI kilimo. Nilipokuwa "O" LEVEL nilizifahamu barabara sehemu kuu za ua.

Anajifunza biashara


Picha hii nimeipata kwa hisani ya gazeti la Daily News toleo la tarehe 4/8/2010. Nimeipenda kwa kumwona mtoto huyu akijifunza kupanga bidhaa zinazouzwa na mzazi wake. Angalia anavyopanga limau huku akielezwa na mzazi wake. Hakika mtoto huyu anajifunza biashara.

Rasimu ya Katiba Mpya majibu leo Kenya


KUNA makundi makubwa mawili nchini Kenya kuhusu mabadiliko ya Katiba ya KENYA kuna wale wanaosema NDIYO na wale wanaosema HAPANA. Makundi haya yanapigiwa debe na vigogo wakubwa wawili Kibaki kundi la NDIYO na lile linalosema "NO" linapigiwa debe na aliyewahi kuwa Rais wa Kenya Daniel Troitch Arap Moi. Makundi haya yanapigana vijembe kweli kweli kuna mawaziri wa Serikali ya Moi wanaoipinga Rasimu ya katiba hiyo pia.

Kocha Poulsen amrudisha Kaseja Taifa Stars


Kocha mpya wa Taifa Stars Mdenish Jan Poulsen amemrudisha Juma Kaseja katika kikosi cha Taifa Stars. Kaseja anaaminika kuwa ni golikipa nambari moja kwa sasa nchini Tanzania, hata kwa kipindi kirefu sasa hajaonekana langoni akiichezea Taifa Stars kwa kile kilichodaiwa na kocha wa zamani Maxio Maximo kuwa ni mtovu wa nidhamu.Hii ni nafasi pekee kwa Kaseja kuwadhihirishia Watanzania kuwa haikuwa kweli, na inampasa kujituma ili aweze kupata namba ya kudumu katika Taifa Stars.

John Waziri ashinda Kichangani


Habari za uhakika ambazo Banzi wa Moro imezipokea muda mfupi uliopita zinaeleza kuwa John Raphael Waziri ameshinda katika kura za maoni za kumpta mgombea wa kiti cha Udiwani kata ya Kichangani, Manispaa ya Morogoro. John ambaye ni mtoto wa mkulima kutoka Matombo, Morogoro na mkazi wa Kichangani katika manispaa hiyo amewabwaga wapinzani wake kwa tofauti ya kura nyingi.

Tuesday, August 3, 2010

Safari ya Dutumi


Bado kuna shida ya usafiri kutoka Morogoro kwenda Dutumi. Picha hii imepatikana kwenye gazeti la Mwananchi la leo likielezea kuwa wasafiri wakipanda lori kutoka Mtamba, Morogoro kwenda Dutumi. Mbunge atakayechaguliwa wa jimbo la Morogoro Kusini ana kazi ya kuhakikisha kuwa anaboresha miundombinu ya usafiri kwenye jimbo lake.

Huyu ndiye aliyemshinda Mzee Malecela


Kama ufahamu, Livingstone Lusinde ameweza kumbwaga mwanasiasa mkongwe na Mbunge wa Jimbo la Mtera Mhe. John Malecela kwenye kura za maoni zilizofanyika Jumapili iliyopita.Unatakiwa kuthubutu tu. Tusiogope.

Phiri arejea Msimbazi


Kazi kwisha mwanangu, Phiri ametua Msimbazi ili aje awauwe watu. Si unaujua mchakamchaka wake ni pointi tatu kutoka mwanzo! Je, watani watatoka tarehe 14 Agosti. Hebu muone mzee wa mipango Nyange a.k.a Kaburu. Si ndo amekwenda kumpokea Phiri kule Ukonga.

Shule Je?


Mvulana huyu alitakuwa kuwa shuleni kama si Sekondari basi Msingi lakini amekuwa mmachinga wa karanga za kukaanga. Je, biashara hii ni ya kwake au ametumwa? Kweli biashara hii itamkwamua. Sidhani. Na kama ndivyo basi biashara hii iboreshwe zaidi, angalia karanga zilivyotungwa kweli hazivutii kuzinunua. Elimu ya biashara ni muhimu pia.

Friday, July 30, 2010

Hii ndiyo timu ya wapelembaji


Idara ya utafiti na Maendeleo iliyoko Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeweka utaratibu mzuri wa kupelemba na kutathmini shughuli za utafiti katika kanda zake saba za utafiti ili kuweza kufahamu utekelezaji wa mipango ya utafiti ufanisi, changamoto na kuweka mikakati ya kupambana na changamoto zinazojitokeza. Pichani wanaonekana wapelembaji waliotumwa kanda ya kaskazini mwezi Juni 2010.

Mwanamke Power Tiller


HATA wanawake wanastahili kuwa na mashine zitakazo rahisisha kazi za shambani kwa ufanisi zaidi. Power tiller inaweza kufanya shughuli nyingi za shambani. Pichani mwanamke akifurahia power tiller.

Yapo maharage yaliyotafitiwa


KAMA ilivyo kwa mahindi.Kaya nyingi hapa nchini hutumia maharage kwa mboga. Ni ukweli usiofichika kuwa kama unampata mpishi mzuri akakupikia maharage kwa nazi na akaunga wali kwa nazi hakika hutaacha kula chakula hicho. Watafiti wetu wameshafanya utafiti na wanaendelea kufanya utafiti wa aina mbalimbali za maharage. Kuna maharage ya rojorojo kuna maharage yanayopendwa kwa rangi yake na hata yale yanayostawishwa kwa ajili ya kusindika au kula yakiwa machanga. Waulize watafiti wa kutoka Selian Arusha na Uyole Mbeya utapata jibu na kuanza kustawisha maharage au kula maharage au kufanya biashara ya maharage.

Watafiti wanapojikita na utafiti wa Mahindi


HAKUNA ubishi watanzania wengi wanakula ugali.Sehemu nyingi za nchi hii zinastawisha mahindi. Utafiti wa mahindi katika nchi hii umeanza muda mrefu na umepata mafanikio makubwa pia umekutana na changamoto nyingi. Utafiti wa mahindi hasa hufanywa na kituo cha utafiti Uyole Mbeya,Selian Arusha na Ilonga Kilosa. Hebu angalia picha ya mahindi yanayofanyiwa utafiti na watafiti kutoka Selian. Hapa lazima uvune tu.

Si mpunga ni ngano


Watu wengi wa pwani hawaufahamu mmea wa ngano ingawa ni hodari sana wa kula chapati mikate na maandazi. Nchi yetu imebahatika kuwa na sehemu zinazozalisha ngano hasa kanda ya kaskazni na Nyanda za Juu Kusini. Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Selian kina jukumu la kutafiti uzalishaji wa ngano. Pichani ngano aina ya JUHUDI kwenye mashamba ya majaribio.

Hata viazi vitamu vinafanyiwa utafiti pia


Si viazi vyote unaweza kutumia majani yake kama mboga ya matembele! Aidha si viazi vyote vinaweza kuwa na unga mwingi. Vile vile viazi vinaweza kuwa na rangi aina tofauti njano, nyeupe hata zambarau. Kazi ya utafiti ni kuzalisha viazi kutokana na matakwa ya wadau na soko

Kilimo mseto wa mahindi na mbaazi


WATAFITI wa kilimo kanda ya Kaskazini wanaendelea na utafiti wa kilimo mseto cha mahindi na mbaazi katika mashamba ya wakulima ili wakulima wenyewe waweze kujionea faida ya kilimo hicho. Moja ya faida ni kurutubisha ardhi. Lakini pia mkulima kwa eneo hilo hilo mkulima anapata mboga na nafaka. Hapa ana uhakika wa chakula na pia kuongeza kipato kwenye familia.

Mkurugenzi anapojishughulisha na utafiti


Ndivyo afanyavyo Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti wa Kilimo kanda ya Kaskazini Dkt. Mbuyi Mugendi aliponaswa na blog hii bila kufahamu akiielezea timu ya kitaifa iliyotumwa kupelemba na kutathmini shughuli za utafiti katika kanda yake. Ni wangapi wanaendelea kufanya kazi za taalama zao ingawa wanajukumu pia ya kusaini hundi?