Tuesday, July 5, 2011
EKARISTI TAKATIFU
Friday, July 1, 2011
Taasisi ya Utafiti Kizimbani -Zanzibar
Makutano ya Legezamwendo na Bubu
Flats alizojenga Sheikh Abeid Amani Karume
Azam Marine
Tunamuandaa kuwa Miss Tanzania
Kwetu sisi ndizi ni kitafunwa tu
Kwa wenyeji wa Morogoro kawaida ndizi huliwa zikiwa mbivu au kama vitafunwa (kwa kunywea na chai). Huwezi ukapikiwa ndizi halafua ukasema kuwa leo nimekula chakula. Hata kama watachanganya na nyama bado ni vitafunwa tu. Chakula cha heshima kwetu ni wali! Angalia mikungu ya ndizi nyuma ya nyumba - Kola, Morogoro mjini.
Pikipiki inapovaa 'helmet'
Malongoza mtaalamu wa kuandaa chakula cha shughuli - Morogoro
Mpishi Malongoza wa Morogoro ni maarufu kwa kupika chakula cha shughuli. Hana papala na anajali muda. Anatayarisha chakula kwa umakini mkubwa hatua kwa hatua na ukimuuliza atakupa sababu. Nilishangaa nipoona anamwagia mafuta sufuria la kupikia. Akanieleza kuwa sababu yake iwe rahisi wakati wa kuosha. Lakini sikumuelewa pale aliponieleza kuwa anamwaga chumvi pembeni ya jiko ili chakula kiwe kitamu! Huyu ndiye Malangoza mtaalamu wa maakuli -Morogoro.
Kuna wazungu na Africana pia
Mkude wa Morogoro
Huyu ni ndugu 'mtoto' wangu anaitwa Mkude. Kwa kuzingatia taratibu za mila za Kiluguru mimi ni Baba Mkude. Lakini mimi ni Banzi au Jaka, Zinga na dada zangu wanaitwa akina Kimbiki ni watoto wa Wambiki. Watoto wangu wanastahili kuitwa akina Mkude, Mizambwa, Mdoti, Midahuli.. (wanaume) na ikiwa mwanamke anaitwa Mwenda au Mlamwenda. Kwa hiyo huyo ni ndugu yangu na ni mtoto wangu. Morogoro akina Mkude,Banzi, Mloka, Mwenda, Mbiki,Mbena, Luanda, Mtonga tukiwa nyumbani tunatumia jina la kwanza kutotofautisha!
Familia ya Morogoro
Subscribe to:
Posts (Atom)