Tuesday, July 5, 2011

Wapambe hawakosi



Dada Batsheba, Meab,kaka Inno,Frank, shangazi Mbwala na Bw wote walikuwepo.Umewaona?

Kwa furaha Ana aliimba wimbo




Baada ya kuvikwa pete ya uchumba, dada Ana kwa furaha aliwaimbia wageni akishirikiana na rafiki yake. Baadaye akina mama, shangazi, dada na wadogo walijimwaga. Mzee Crispin Mangengesa Mdimi (Baba mzazi) na Dkt. Gregory Paul Mluge (Mjomba) wote walifurahi baada ya tukio hilo.

Kilichofuata ni hafla ya 'engagement'



Nikueleze?Baada ya kupata mkwanja wa kutoka ..... Kuna nini tena! Ilikuwa ni hafla fupi ya 'engagement'Wahusika walijitokeza hadharani. Kulia ni dada Anna na kushoto ni shem wetu Mlaki. Aliyeshika microphone ni Banzi wa Moro.Hapa sasa ni mshereheshaji.Wakati wa kutoa mahali nilikabidhiwa jukumu na familia kuendesha mchakato wa kutoa na kupokea posa.Waandishi wa habari wa vyombo vyote hapa nchini walishuhudia tukio hili.

Tunapokea mahali



Baba alipokea chake, mama alipata mkaja wake, babu alipata kichana ndevu, shoka na panga pia ni baadhi ya vitu vya posa. Dada Vicky Mdimi alipokea fedha kwa niaba ya familia na kaka mtu Kamsopi Mdimi alipokea shoka na panga na baadaye kukabidhiwa wahusika. Akina Ngowi walilijizatiti kweliwkeli. Kilichofuata .........

Karibuni!



Siku ya Jumapili tarehe 3/7/2011. Familia ilipokea posa ya dada yetu Ana Mdimi anayeolewa na Bw. Pichani shangazi anagalagala chini kwa mila na taratibu za kimanda mpaka afichuliwe na wakwe ndipo wakaribishwe!

Paroko Tomy alisimamia maandamano



Maandamano ya kuabudu Ekaristi Takatifu Parokia ya Vikindu.Father Tomy mbele ya Watoto wa Utatu,waimbaji waliimba kwa shangwe.Watoto walishiriki kikamilifu katika maandamano.

Maandamano Parokiani-Vikindu Jimbo kuu la Dar Es Salaam



Sakaramenti hiyo twaiabudu kifudifudi na sheria za zamani zikomeshwe na hiyooo. Yafichaikayo machoni imani huyaona. Wimbo huu ni maarufu sana siku ya Sikukuu ya Ekaristi Takatifu nilianza kuiimba nikiwa katika Parokia ya Mt.Paulo Matombo,Morogoro.

EKARISTI TAKATIFU

Tarehe 26/6/2011 Wakatoliki waliazimisha sikukuu ya Ekaristi Takatifu. Pichani chombo kinachong'aa ni 'MONSTRANCE' kule kwetu Matombo tunaiita 'Monstrandi'

Friday, July 1, 2011

Taasisi ya Utafiti Kizimbani -Zanzibar




Hapa ndipo Makao makuu.Utafiti wa Mpunga - NERICA unaendelea.Na mahojiano yalifanyika pia ofisini kwa Mkurugenzi wa Taasisi - Dr. Salehe Haji

Mwanakwerekwe


Na hapa ndipo Mwanakwerekwe. Ni mahali maarufu Zanzibar.

Na hizi amejenga mtoto wa Karume


Mhe. Amani Abeid Karume alifuata nyayo za baba yake na kujenga flats hizi.

Makutano ya Legezamwendo na Bubu


Hapa barabara mbili zinakutana. Moja ni Legezamwendo na nyingine ni Bububu. Ukienda Kizimbani sharti upite hapa.

Bahari imetulia


Bahari ikitulia unaweza hata kufanya kazi na Laptop!

Bahari ikichafuka!



Bahari ikchafuka. Abiria chomboni ni kama uonavyo.

Flats alizojenga Sheikh Abeid Amani Karume

Majengo haya ni kumbukumbu ya Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume. Mwenyekiti wa Kwanza wa Baraza la mapinduzi Zanzibar hapa ni Michenzani-Unguja.

Wanafurahia boat

Kama hakuna mawambi ni raha kusafiri na boat.

Hiyo ndiyo bahari ya Hindi

Bahari ya hindi imetulia tuli!

Ndani ya boat

Nje ya boat juu kwa mbele.

Nje ya Boat Je?

Azam Marine


Unaposafiri kwenda Unguja kwa kutumia boat. Boat yenye uhakika na raha na Azam Marine na hii ndiyo ofisi yao - Dar