Monday, October 3, 2011

Maji ya Baraka

Paroko Sowa wa Parokia ya Matombo ndiye aliyeendesha ibada takatifu. Pichani anaonekana akinyunyiza maji ya baraka.

Binti akimlilia baba yake

Ndiyo kwanza amewasili kutoka Songea anakoishi. Felista, mtoto wa nne wa marehemu Jerome Hugo akimlilia baba yake mbele ya jeneza. Majonzi, majonzi, majonzi.

Jeneza linasubiri kuingizwa kanisani

Kanisa la mtakatifu Paul-Parokia ya Matombo, jimbo la Morogoro ndimo ilimofanyika ibada ya misa takatifu ya marehemu Jerome Hugo. Kanisa hili ndilo marehemu alilolitumikia kwa miaka mingi katika maisha yake. Amebatizwa ndani ya kanisa hili, amepata ekaristi takatifu ndani ya kanisa hili na Kipaimara pia. Amefunga ndoa yake ndani ya kanisa hili na kuagwa ndani ya kanisa hili. TUMSIFU YESU KRISTU.

Mwili unawasili kanisani

Maandamano kuelekea kanisani.

Jeneza ndani ya gari

Jeneza likiwa ndani ya gari tuliusindikiza mwili kwenda kanisani kwa ajili ya ibada takatifu.

Waombolezaji nyumbani kwa marehemu Babu Jerome

Mwezi Septemba mwaka huu familia ilipata msiba wa kuondokewa na mzee wetu Jerome Huggo a.k.a Babu Jerome. Huyu ndiye mzee ambaye alikuwa na kumbukumbu nyingi za familia na hata kanisa Katoliki lilivyoingia Matombo. Nilibahatika kuhudhuria mazishi yake. Pichani mpwa wake Dr. Gregory akiwa msibani.

Walimu mabingwa wa hesabu katika mchakato

Let us Talk Mathematics



Bright Angels wamepania kukuza vipaji vya hesabu. Kila mwaka huandaa tamasha la kuwahamasisha wanafunzi kuelewa, kujifunza na kupenda hesabu. Huwakutanisha wanafunzi kutoka shule za jirani hasa wa sekondari. Ukifanya mazoezi na ukipenda hesabu siyo ngumu.

Ninawakumbusha Africana


Wanachama wa 'Africana Group' mnakumbushwa kuwa kikao kitafanyika tarehe 09 Oktoba 2011 siku ya Jumapili saa 6.00 mchana huko kijijini Kisemvule, wilaya Mkuranga, mkoa wa Pwani (Kwa Inno Banzi). Kuwahi ni jambo la muhimu sana. Ubwabwa wa nazi utakwepo.

Mnakaribishwa

I.J.Banzi
Mwenyeji/Mkiti wa Kikao

Baadaye ilibidi tupige picha ya ukumbusho


Kade na Banzi nyumbani Ksemvule, Mkuranga, mkoa wa Pwani

Kutoka Matombo hadi Kisemvule


Tulizungumza sana tukikumbuka enzi zetu kule nyumbani Matombo. Mashindano ya sabasaba ambapo yeye alikuwa bingwa wa kukimbia mita 100 nafikiri ingekuwa kwa wenzetu hivi sasa angefananishwa na H.BOIT.Stori za 'solono' (kupiga mbizi) mtoni mfizigo hazikukosekana pia. Tuliwakumbuka wazee maarufu, walimu waliotufundisha hata, wanafunzi watukutu walevi wa kijijini waliokuwa wanawasumbua, sikukuu za kanisa hasa ekaristi kuzunguka kijiji cha Kiswira na hata wasichana watanashati waliotetemesha pale kijijini enzi hizo wengine hawapo tena nasi duniani.

Kade ndani ya Kisemvule


Siku bro Kade alipopiga hodi Kisemvule. Tulimpokea kwenye msonge. Pichani anamemkumbatia mjomba Maria

September haikuwa nzuri kwangu


Majukumu ya kikazi, familia pamoja na mgao wa umeme umeiathiri sana blog hii. Mwezi Septemba sikuwatendea haki wapenzi wa Banzi wa Moro. Nina mengi ya kuwajuza kupitia blog hii. Poleni sana. Tuko pamoja.

Friday, August 19, 2011

Banzi wa Moro


Chini kulia miaka 37 iliyopita nikiwa Njombe Secondary School - FORM ONE. Nyuma yangu ni Library ya shule!Juu kushoto mwaka huu nalishwa keki na Mamaa- nyumbani Kisemvule, Mkuranga, Pwani.Taja tofauti 5 za picha hizo.SHUKRANI KWA MUNGU


Tuesday, August 16, 2011

Lugaluga wanalima na kuuza




Kama tunataka wakulima wetu wasinyonywe na wakione kilimo kinalipa wazalishe na kuuza wenyewe huku wakimiliki zana za usalishaji na ikiwezekana na miundo mbinu. Lugaluga wameshaanza kufanya hivyo. Kinachowakwimisha ni miundo mbinu ya umwagiliaji na barabara safi za mashambani. Hilo linatakiwa kufanyiwa kazi.

Viongozi na wanachama wa Lugaluga



Namimi nimo ni mwanachama mwanzilishi wa Lugaluga.

Lugaluga walikuwepo 8/8




LugaLuga Agricultural Marketing and Cooperative Society kulikuwepo kwenye maonyesho ya wakulima ya mwaka 2011 kwenye uwanja wa maonyesho-Morogoro. Walioneysha zana wanazotumia (matrekta madogo na makubwa) ambayo wanamiliki wanachama kupitia Ushirika wao. Bidhaa wanazozalisha- Mpunga, alizeti na mahindi. Hao ndiyo Lugaluga waliojizatiti kuondoa umaskini kupatia Ushirika.

Wakorea wanataka kuibadilisha Pangawe






Katika muda wa miaka mitano ijayo, Wakorea wanataka kukibadilisha kijiji cha Pangawe kilichopo wilaya ya Morogoro vijijini kuoenakana cha kisasa zaidi kikiwa na miundombinu ya umwagiliaji, barabara za mashambani, shule bora ya msingi, maji safi huduma ya afya, umeme na huduma nyingine. Tusubiri tuone. Kazi hiyo inafanywa na KOICA-Korea Interanational Cooperation Agency.