Wednesday, May 30, 2012
Binti yetu atimiza miaka 14
Jana tarehe 29/5/2012 binti yetu Catherine Banzi (kulia) ametimiza umri wa miaka 14. Hongera sana Catherine Mungu akubariki sana uwe na maisha marefu.
Tuesday, May 29, 2012
MC alimuona mtoto huyu
Kati ya watoto walioshughulika sana katika kupiga picha za send off ya Adela alikuwa ni huyu mwenye T-shirt ya pink na suruali ya jeans ilibidi MC amtambulishe mbele ya wageni waalikwa na kumpongeza.
Ni wakati wa Kwaito!
Kama umepata msosi na vinywaji bwelele hakuna wa kukukataza kuyarudi magoma kwa raha zako. Hapa ni Moro,Magadu Leaders Club siku ya Send off ya Adela, mzee wetu huyu akionyesha umahiri wake katika kuirudi miondoko ya 'Kwaito'. Kwa kweli Moro oyee!
'Vikuku vinanukia ahaa."
Enzi zangu niliipenda sana nyimbo tuliyoibatiza 'vikuku vinanukia ....' Lakini hii ni picha hali ya msosi tulioukamata siku ya send off ya dada yetu Adela Ng'atigwa (kuku wa kienyeji kutoka Nyandila-mgeta, bamia, njegere, kisamvu, derega, vhimoka, magimbi, samaki, mbumundu, bwasali, ng'udende, uhunga, ng'andulo....). Kilikuwa kitamu sana!
Fuga nguruwe ujiongezee kipato
Nguruwe ni mnyama rahisi kumfuga kwani hashambuliwi sana na maradhi na pia hutumia aina mbalimbali za vyakula ambavyo hupatikana kirahisi katika mazingira yoyote.Jijini Dar Es Salaam nguruwe wa uzito wa kilo 80 anaweza kukupata kiasi cha Tshs 400,000/=. Nilipotembbelea mikoa ya Iringa na Mbeya nilikuta wakulima wengi wakifuga nguruwe hasa wilaya ya Kilolo kijiji cha Kidabaga.
Radio pembeni
Inawezekana vijana hawapendi tena kusikiliza radio. Lakini wazee wengi hupenda kusikiliza radio kama inavyoonekana pichani Mama Hasbon Makishe akiwa karibu sana na radio wakati alipowatembelea wajukuu zake nyumbani kwao Kisemvule mkoa wa Pwani.
Mtu na wifi yake
Dada Julieth Madenge kushoto akiwa na wifi yake Nancy Banzi kwenye bustani za Magadu Leaders' Club-Morogoro
Tuchague miti ya kupanda karibu na nyumba zetu
Tunashauriwa kupanda miti yenye manufaa kama vile ya matunda kando ya nyumba zetu kamavile mpera (pichani)
Monday, May 28, 2012
Mjengo wa Masaki
Pitapita zangu jijini Dar kando ya bahari ya Hindi nilinyaka mjengo huu wa Masaki.Nikwambie kitu, Masaki mwanangu asikwambie mtu kuna mijengo ya nguvu na kumetulia, na kusafi!
Bw na Bibi Kavia
Watu wengi wamnekuwa wakiniomba nining'inize picha ya Bw.na Bibi Kavia. Pichani MC.akiwatambulisha maharusi watarajiwa Bw.na Bibi Kavia
Sunday, May 13, 2012
Kilimo kinavyobadili maisha ya wakulima
Niko kikazi mikoa ya Iringa na Mbeya kwa madhumuni ya kukagua miradi inayotekelezwa na Programu ya kuendeleza Sekta ya Kilimo Tanzania (ASDP).Mpaka sasa nilichokiona kinatia moyo pale miradi ilipotekelezwa vizuri.Vijiji ambavyo havikutekeleza vizuri mambo ni 'business as usual' Wakulima wetu wanafanya kazi katika mazingira magumu. Wanazalisha ili kutulisha sisi. Kuna wengine kilimo kimebadilisha maisha yao. Kwa mfano wakulima wa kijiji cha Magozi Iringa vijijini kutokana na kilimo cha mpunga sasa wana uhakika wa chakula mwaka mzima, wengi wameweza kujenga nyumba bora pia wamejinunulia jenereta ya kufua umeme!
Mpunga ndani ya viroba
'Satelitte dish' kijijini Magozi wilaya ya Iringa Vijijini
Nyumba bora za kisasa.
Saturday, May 5, 2012
Meza zilifurika vinywaji
Hakuna aliyelalamika kukosa kinywaji, kila meza ilifurika kinywaji siku ya Sendoff ya Da Adela Ng'atigwa. Waluguru wanasema 'lusona na mbwali' - Sherehe na pombe (tafsiri yangu).
Meza ya akina Kobelo
Familia ya Kobelo kutoka Dar Es Salaam na Morogoro ilikuwa na meza yao kwenye sendoff ya Adela. Waluguru wanamsemo wao 'Lusona lwao'
Ndugu na marafiki walikutana
Sendoff ya Adela imekutanisha wengi
Dada Rest wa Kilakala-Morogoro
Dada Mbiki wa Morogoro
Dada Kibena wa Morogoro
Wafanyakazi wa MAFC-Dar
Subscribe to:
Posts (Atom)
