Thursday, August 2, 2012

Uwanja wa Taifa

Manispaa ya Temeke imebahatika kuwa na viwanja vikuu viwili vya michezo. Uwanja wa Taifa na Uwanja wa UHURU. Vyote vimejengwa katika sehemu moja.Picha inaonyesha lango kuu la Uwanja wa Taifa (NATIONA STADIUM).

Wednesday, August 1, 2012

Mazingira ya mkoa wa Morogoro

Mkoa wa Morogoro una mazingira tofauti tofauti.Kuna sehemu za vilima vilima na sehemu za mabonde. Kuna sehemu za baridi kali na sehemu za joto kali.Pichani ni sehemu ya bonde na mlima unaoonekana kwa mbali.

Sekondari ya Magereza Ubena

Sekondari ya Magereza Ubena imejengwa katika maeneo haya, miti mingi imeoteshwa hivyo kutoa mazingira mazuri ya kujisomea.

Chai kwa magimbi

Siku hizi migahawa mingi na mahoteli mjini Morogoro huuza vitafunwa vya magimbi kwa kifungua kinywaji. Pichani wateja wakipata chai kwa magimbi na mihogo bila kusahau supu!

Ghala la mchele - Moro

Hili ni moja ya maghala mengi binfasi ya mchele yaliyotapakaa mjini Morogoro. Mwezi Julai mwaka huu kilo moja ya mchele iliuzwa kwa sh1500/= wafanyabiashara wanabashiri kuwa hali ya upatikanaji wa mchele haitokuwa nzuri kwa mwaka ujao huenda bei ikapanda sana.

Ametoka Bungeni

Mmoja wa wataalamu wa Wizara ya Kilimo Bw. Sarema wa Idara ya Uendelezaji Mazao akitokea Bungeni Dodoma mwezi Julai 2012 akifanya mazoezi pale Dumila akiwa njiani kuelekea Dar.

Tuesday, July 31, 2012

Maini ya NjiaPanda ya Mbande

Kama unasafiri kuelekea Dodoma njiapanda ya kwenda Kongwa na Mpwapwa sehemu inayoitwa Njiapanda ya Mbande ni maarufu kwa biashara za nyama ya kuchoma. Hata asubuhi hapa unaweza kupata maini na figo za moto!

Speaker za S90-Nimezikuta Dodoma

Speaker za kirusi S90 (Sto divnosta) nimezikuta kwenye ukumbi mmoja mjini Dodoma na zinatwanga ile mbaya!Speaker hizi ni toleo la miaka ya themanini!

Hapa ndipo KILIMO IV

Hili ndilo jengo la Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika lilipo mjini Dodoma al maarufu kama KILIMO IV. Ukiwa ndani ya jengo hili ni kwa kazi maalum na hakuna kulala. Wizara hulitumia jengo hili kwa mikutano mbalimbali inayofanyika mjini Dodoma. Lakini hutumika kikamilifu wakati wa vikao vya Bunge hasa Bunge la kuwasilisha Bajeti.

Hali ngumu wazee

Wakati vijana wenzake wakiwa katika pilika za kuuza biashara zao za nyanya na maboga na wengine kuuza matenga,kijana huyu(pichani)alitulalamikia kwa kusema hali ni ngumu wazee. Sijui tungemsaidiaje.Atazidi kulalamika sana wakati wenzake wakiendelea endapo hatabadilika.

Wanawake nao wamo

Banzi wa Moro aliinyaka picha hii wakati mwanamke huyu akiwa katika harakati za kupanga matenga kwenye lori. Miaka 20 iliyopita, mwanamke asingweza kudandia lori na kupanga matenga.Sina shaka mwanamke huyu ni mfanyabiashara wa nyanya.

Biashara huria

Baada ya kununua bidhaa inabidi kukaa chemba kujadili bei na mchuuzi kwani unaweza kupunguziwa bei kutokana na ushawishi wako kwani biashara ni huria! Usishangae boga la sh 1000 likauuzwa kwa sh 500!

Nitakutumia nikifika Kisemvule

Huduma za M-Pesa, Tigo-Pesa na Airtel Money zimeingia kwa kasi kijijini kwetu Kisemvule-Mkuranga.Usiwe na wasiwasi ninaweza kukutumia ngawira au kupokea ngawira nikiwa Kisemvule!

Boga kwa futari

Tulipofika Wami Dakawa njiapanda ya kwenda Turiani, tulishindwa kujizuia kununua maboga. Wakati huu wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani, futari ya maboga ni moja ya vikoromwezo vya chakula vinavyotumika kwa futuru.Hapa tulinunua boga moja kwa kiasi cha shilingi 1000/=. Pichani Bi Ishika Mshaguley akichagua boga analolipenda!

Na baadaye safarini DAR

Ndivyo tunavyotumia magari ya serikali. Ni kwa safari za kikazi na si vinginevyo. Toyota Landcruiser S/W nafikiri siyo gari la kifahari eti jamani. Pichani dereva wetu Lems Nyagawa akiwa maeneo ya Dumila mkoani Morogoro tukiwa njiani kuelekea Dar tarehe 22/7/2012 baada ya kikao cha Bunge.

Tunapokuwa Bungeni Dodoma

Tunapowakilisha Bajeti zetu Bungeni- Dodoma si lele mama. Kazi kubwa ni kujibu hoja za wabunge. Mwezi Julai 2012 Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika iliwasilisha Bajeti yake na hivi ndivyo wataalamu walivyojitayarisha kujibu hoja zilizoibuliwa na wabunge.
Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo Dkt. F.Myaka (mwenye laptop)akiwa katika ukumbi wa Kilimo IV Dodoma
Wataalamu wa kilimo wakifuatilia kwa makini mawasilisho ya Bajeti ya Wizara kupitia luninga wakiwa ndani ya jengo la Kilimo IV Dodoma
Kuna hoja zilizoumiza vichwa lakini zilijibiwa na hatimaye bajeti ikapita.

Mtoto anaposaidiwa kukamilisha 'homework'

Hapa nampa big-UP my nanihii.... kwa kutenga muda kumsaidia binti yetu Maria kukamilisha homework yake!

Watoto hupenda kuzima mishumaa ya birthday

Siyo birthday yake lakini uncle Jordan Kirita alizima mishumaa ya aunt wake Dr. Doreen Moshi (aliyemshikilia).

Umoja unaanzia kwenye familia

Kikundi cha Africana kikiwa kwenye mkutano wa mwezi Julai huko Chang'ombe karibu kabisa na uwanja wa TCC nyumbani kwa Bw. na Bi. J.Kirita

Ukishuka ulizia Kisemvule gengeni!

Hapa ndipo bus la Mbagala Rangi Tatu-Mwandege-Vikindu-Kisenvule linapogezia. Ni Kisemvule magengeni.