Friday, August 3, 2012
Wajumbe walikagua vyoo
Kazi ilianza mara moja. Baada ya kikao wajumbe wa Bodi wakiongozwa na Mwenyekiti Bw. Bakari Chande walikagua vyoo.
Bodi ya VSS-Kikao cha I
Tarehe 30/6/2012 Bodi ya Vikindu Secondary School ilikaa kikao chake cha I na kumchagua Bw. Bakari Chande kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi. Mambo makuu yaliyozungumzwa katika kikao hicho ni kuhusu miundo mbinu ya shule hasa ubovu wa vyoo, upungufu wa viti na madawati kwa wanafunzi,mimba kwa wasichana na utoro sugu. Kuhusu tatizo la ubovu wa vyoo, wajumbe kwa pamoja waliamua kuchangia sh. 20,000/- kila mmoja na kuazimia kuitisha kikao na watendaji wa vijiji wa Kata ya Vikindu kuzungumzia matatizo yanayoikabili shule ya Sekondari Vikindu.
Wajumbe wa Bodi ya Vikindu Secondary School (VSS)
Hawa ni baadhi ya Wajumbe wapya wa Bodi ya VSS wakiwa katikam picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao cha I cha Bodi
Kiatu cha harusi
Kiatu cha harusi bado kipo, koti la suti ipo, shati bado lipo isipokuwa suruali inabana sana. Samahani, watoto wameniibia gidamu za kufungia viatu ndiyo maana nimefunga kwa gidamu nyeusi!
Banzi-Miaka 15 ya Ndoa
Jana tarehe 2/8/2012 ni kumbukumbu ya kubariki ndoa yetu mimi na mkewe wangu Nancy Ireneus Mbawala.Ni miaka 15 imepita sasa.Kumbukumbu zinaonyesha bajeti ya sherehe za harusi yetu mwaka 1997 ilikuwa ni Tsh 830,000/-. Nawashukuru wote walioshughulika kwa ajili yetu.
Tunamshukuru Mungu.
Matukio-Kipaimara cha Linda Lwezaura
Bi Linda Deogatias Lwezaura (kushoto) akiwa na mpambe wakeWatoto walikaribishwa.
Masista walialikwa.Msosi wanguvu.Miondoko ya mshehereshaji (mc)Msosi kwa Linda na mpambe wake.Dr. Julius Mwanandota akiserebuka.
Thursday, August 2, 2012
Mbuzi wadogo
Mbuzi wakiwa wadogo wanapendeza sana. Hukimbia huko na huko. Kwa kifupi ni watundu. Mbuzi wakifugwa kitaalamu hutoa nyama choma nzuri na hata maziwa, hivyo kuboresha lishe na kipato.Pale inapowezekana fuga mbuzi.
Wanasubiri mafunzo ya ziada
Elimu popote. Banzi wa Moro aliwanyaka wanafunzi hawa wa Kisemvule Shule ya Msingi wakisubiri mafunzo ya ziada a.k.a tuition
Na hii ndiyo Mbagala Rangi 3
Mbagala Rangi 3- Picha imechukuliwa kutoka kwenye kighorfa cha Huduma Bar (Kwa wale wanaoifahamu Mbagala Rangi 3)
Uwanja wa Taifa
Manispaa ya Temeke imebahatika kuwa na viwanja vikuu viwili vya michezo. Uwanja wa Taifa na Uwanja wa UHURU. Vyote vimejengwa katika sehemu moja.Picha inaonyesha lango kuu la Uwanja wa Taifa (NATIONA STADIUM).
Wednesday, August 1, 2012
Mazingira ya mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro una mazingira tofauti tofauti.Kuna sehemu za vilima vilima na sehemu za mabonde. Kuna sehemu za baridi kali na sehemu za joto kali.Pichani ni sehemu ya bonde na mlima unaoonekana kwa mbali.
Sekondari ya Magereza Ubena
Sekondari ya Magereza Ubena imejengwa katika maeneo haya, miti mingi imeoteshwa hivyo kutoa mazingira mazuri ya kujisomea.
Chai kwa magimbi
Siku hizi migahawa mingi na mahoteli mjini Morogoro huuza vitafunwa vya magimbi kwa kifungua kinywaji. Pichani wateja wakipata chai kwa magimbi na mihogo bila kusahau supu!
Ghala la mchele - Moro
Hili ni moja ya maghala mengi binfasi ya mchele yaliyotapakaa mjini Morogoro. Mwezi Julai mwaka huu kilo moja ya mchele iliuzwa kwa sh1500/= wafanyabiashara wanabashiri kuwa hali ya upatikanaji wa mchele haitokuwa nzuri kwa mwaka ujao huenda bei ikapanda sana.
Ametoka Bungeni
Mmoja wa wataalamu wa Wizara ya Kilimo Bw. Sarema wa Idara ya Uendelezaji Mazao akitokea Bungeni Dodoma mwezi Julai 2012 akifanya mazoezi pale Dumila akiwa njiani kuelekea Dar.
Subscribe to:
Posts (Atom)


