Friday, August 10, 2012
Nilifurahishwa na huduma za TTCL
TTCL ni kampuni kongwe ya mawasiliano nchini Tanzania. Kwenye maonyesho ya wakulima ya mwaka 2012 kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Temi Jijini Arusha nilifurahishwa na huduma zao. Hapa niliweza kununua simu ndogo safi kwa bei ya sh 20,000/- na kusajiliwa hapohapo. Niliweza kununua betry charger kwa shilingi 5,000/- kwa simu yangu ya zamani ambao charger yake ilipotea. Pia niligawiwa vipeperushi pamoja na mfuko wa TTCL!
Hai ni zaidi ya bidhaa za shambani
Wilaya ya Hai walijipanga kisawasawa kwenye maonyesho ya Nanenane 2012 kanda ya Kaskazini yaliyofanyika kwenye viwanja vya Temi Arusha. Wakulima kwenye makundi yao ya uzalishaji walionyesha bidhaa nyingine zaidi ya mazao ya kilimo.
Ngogwe na parachichi
Kwenye banda la Halmashauri ya wilaya ya Hai niliweza kujionea nyanya chungu (ngogwe)na parachichi na mazao mengine haya ni maonyesho ya wakulima mwaka 2012 Kanda ya Kaskazini
Friday, August 3, 2012
Na baadaye kukagua mipaka ya shule
Baada ya kukagua vyoo na kukuta viko katika hali mbaya sana. Ilibidi pia kukagua mipaka ya shule kwani tayari uvamizi wa eneo la shule umeshaanza.
Wajumbe walikagua vyoo
Kazi ilianza mara moja. Baada ya kikao wajumbe wa Bodi wakiongozwa na Mwenyekiti Bw. Bakari Chande walikagua vyoo.
Bodi ya VSS-Kikao cha I
Tarehe 30/6/2012 Bodi ya Vikindu Secondary School ilikaa kikao chake cha I na kumchagua Bw. Bakari Chande kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi. Mambo makuu yaliyozungumzwa katika kikao hicho ni kuhusu miundo mbinu ya shule hasa ubovu wa vyoo, upungufu wa viti na madawati kwa wanafunzi,mimba kwa wasichana na utoro sugu. Kuhusu tatizo la ubovu wa vyoo, wajumbe kwa pamoja waliamua kuchangia sh. 20,000/- kila mmoja na kuazimia kuitisha kikao na watendaji wa vijiji wa Kata ya Vikindu kuzungumzia matatizo yanayoikabili shule ya Sekondari Vikindu.
Wajumbe wa Bodi ya Vikindu Secondary School (VSS)
Hawa ni baadhi ya Wajumbe wapya wa Bodi ya VSS wakiwa katikam picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao cha I cha Bodi
Kiatu cha harusi
Kiatu cha harusi bado kipo, koti la suti ipo, shati bado lipo isipokuwa suruali inabana sana. Samahani, watoto wameniibia gidamu za kufungia viatu ndiyo maana nimefunga kwa gidamu nyeusi!
Banzi-Miaka 15 ya Ndoa
Jana tarehe 2/8/2012 ni kumbukumbu ya kubariki ndoa yetu mimi na mkewe wangu Nancy Ireneus Mbawala.Ni miaka 15 imepita sasa.Kumbukumbu zinaonyesha bajeti ya sherehe za harusi yetu mwaka 1997 ilikuwa ni Tsh 830,000/-. Nawashukuru wote walioshughulika kwa ajili yetu.
Tunamshukuru Mungu.
Matukio-Kipaimara cha Linda Lwezaura
Bi Linda Deogatias Lwezaura (kushoto) akiwa na mpambe wakeWatoto walikaribishwa.
Masista walialikwa.Msosi wanguvu.Miondoko ya mshehereshaji (mc)Msosi kwa Linda na mpambe wake.Dr. Julius Mwanandota akiserebuka.
Thursday, August 2, 2012
Mbuzi wadogo
Mbuzi wakiwa wadogo wanapendeza sana. Hukimbia huko na huko. Kwa kifupi ni watundu. Mbuzi wakifugwa kitaalamu hutoa nyama choma nzuri na hata maziwa, hivyo kuboresha lishe na kipato.Pale inapowezekana fuga mbuzi.
Wanasubiri mafunzo ya ziada
Elimu popote. Banzi wa Moro aliwanyaka wanafunzi hawa wa Kisemvule Shule ya Msingi wakisubiri mafunzo ya ziada a.k.a tuition
Na hii ndiyo Mbagala Rangi 3
Mbagala Rangi 3- Picha imechukuliwa kutoka kwenye kighorfa cha Huduma Bar (Kwa wale wanaoifahamu Mbagala Rangi 3)
Subscribe to:
Posts (Atom)



