Friday, August 10, 2012

Nilifurahishwa na huduma za TTCL

TTCL ni kampuni kongwe ya mawasiliano nchini Tanzania. Kwenye maonyesho ya wakulima ya mwaka 2012 kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Temi Jijini Arusha nilifurahishwa na huduma zao. Hapa niliweza kununua simu ndogo safi kwa bei ya sh 20,000/- na kusajiliwa hapohapo. Niliweza kununua betry charger kwa shilingi 5,000/- kwa simu yangu ya zamani ambao charger yake ilipotea. Pia niligawiwa vipeperushi pamoja na mfuko wa TTCL!

Hai ni zaidi ya bidhaa za shambani

Wilaya ya Hai walijipanga kisawasawa kwenye maonyesho ya Nanenane 2012 kanda ya Kaskazini yaliyofanyika kwenye viwanja vya Temi Arusha. Wakulima kwenye makundi yao ya uzalishaji walionyesha bidhaa nyingine zaidi ya mazao ya kilimo.

Ngogwe na parachichi

Kwenye banda la Halmashauri ya wilaya ya Hai niliweza kujionea nyanya chungu (ngogwe)na parachichi na mazao mengine haya ni maonyesho ya wakulima mwaka 2012 Kanda ya Kaskazini

Bilinganya la Nanenane 2012 Kanda ya Kaskazini

Kwenye banda la maonyesho Manispaa ya Jiji Arusha moja ya kivutio ni bilinganya kubwa!

Friday, August 3, 2012

Ukiuliza nyodo utajibiwa nyodo

Eti yamepimwa angaza!

Na baadaye kukagua mipaka ya shule

Baada ya kukagua vyoo na kukuta viko katika hali mbaya sana. Ilibidi pia kukagua mipaka ya shule kwani tayari uvamizi wa eneo la shule umeshaanza.

Wajumbe walikagua vyoo

Kazi ilianza mara moja. Baada ya kikao wajumbe wa Bodi wakiongozwa na Mwenyekiti Bw. Bakari Chande walikagua vyoo.

Bodi ya VSS-Kikao cha I

Tarehe 30/6/2012 Bodi ya Vikindu Secondary School ilikaa kikao chake cha I na kumchagua Bw. Bakari Chande kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi. Mambo makuu yaliyozungumzwa katika kikao hicho ni kuhusu miundo mbinu ya shule hasa ubovu wa vyoo, upungufu wa viti na madawati kwa wanafunzi,mimba kwa wasichana na utoro sugu. Kuhusu tatizo la ubovu wa vyoo, wajumbe kwa pamoja waliamua kuchangia sh. 20,000/- kila mmoja na kuazimia kuitisha kikao na watendaji wa vijiji wa Kata ya Vikindu kuzungumzia matatizo yanayoikabili shule ya Sekondari Vikindu.

Wajumbe wa Bodi ya Vikindu Secondary School (VSS)

Hawa ni baadhi ya Wajumbe wapya wa Bodi ya VSS wakiwa katikam picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao cha I cha Bodi

Vikindu Secondary School

Hii ndiyo shule ya Sekondari Vikindu iliyoko wilyani Mkuranga katika kijiji cha Kisemvule

Kiatu cha harusi

Kiatu cha harusi bado kipo, koti la suti ipo, shati bado lipo isipokuwa suruali inabana sana. Samahani, watoto wameniibia gidamu za kufungia viatu ndiyo maana nimefunga kwa gidamu nyeusi!

Chakula cha miaka 15 ya ndoa

Wali, nyama, mchicha,njegere pamoja na bia kidogo

Banzi-Miaka 15 ya Ndoa

Jana tarehe 2/8/2012 ni kumbukumbu ya kubariki ndoa yetu mimi na mkewe wangu Nancy Ireneus Mbawala
.Ni miaka 15 imepita sasa.Kumbukumbu zinaonyesha bajeti ya sherehe za harusi yetu mwaka 1997 ilikuwa ni Tsh 830,000/-. Nawashukuru wote walioshughulika kwa ajili yetu. Tunamshukuru Mungu.

Matukio-Kipaimara cha Linda Lwezaura

Bi Linda Deogatias Lwezaura (kushoto) akiwa na mpambe wake
Watoto walikaribishwa.
Masista walialikwa.
Msosi wanguvu.
Miondoko ya mshehereshaji (mc)
Msosi kwa Linda na mpambe wake.
Dr. Julius Mwanandota akiserebuka.

Thursday, August 2, 2012

Raha ya vijijini

Mkutano unafanyika chini ya kivuli cha mti. Hapa ni wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa

Chips zinaanzia hapa

Huwezi kupata chips bila kulima viazi mviringo. Chips zinaanzia kwenye kilimo.

Kilimo cha umwagiliaji - Mtazamo

Mbuzi wadogo

Mbuzi wakiwa wadogo wanapendeza sana. Hukimbia huko na huko. Kwa kifupi ni watundu. Mbuzi wakifugwa kitaalamu hutoa nyama choma nzuri na hata maziwa, hivyo kuboresha lishe na kipato.Pale inapowezekana fuga mbuzi.

Wanasubiri mafunzo ya ziada

Elimu popote. Banzi wa Moro aliwanyaka wanafunzi hawa wa Kisemvule Shule ya Msingi wakisubiri mafunzo ya ziada a.k.a tuition

Na hii ndiyo Mbagala Rangi 3

Mbagala Rangi 3- Picha imechukuliwa kutoka kwenye kighorfa cha Huduma Bar (Kwa wale wanaoifahamu Mbagala Rangi 3)