Monday, April 8, 2013

Mradi wa WEMA: Maelezo kwa Rais

Dr. Kullaya kutoka ARI-Mikocheni akitoa maelezo wa mradi wa WEMA kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea kituo hicho tarehe 19/3/2013

Saturday, April 6, 2013

Fotoa ufotolewe

Dr. Janet Kaaya Mkuu wa Kitengo cha 'Information and Documentation' Idara ya Utafiti na Maendeleo, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika akiwa kazini. Hakufahamu kuwa kulikuwa na wengine waliomlenga. Kweli ''fotoa ufotolewe!

Watafiti na Rais Kikwete

Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na watafiti wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Mikocheni alipotembelea kituo hicho tarehe 19/3/2013

Mdudu chonga wa minazi

Rais Kikwete akimchunguza mdudu msumbufu wa minazi - Chonga

Picha na Rais Kikwete

picha yangu na Rais wangu hii hapa.

Thursday, April 4, 2013

Rais Kikwete akizindua Maabara ya Uhandisi Jeni

Tarehe 19 Machi 2013, Mhe. Rais Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete alitembelea kituo cha Utafiti wa Kilimo Mikocheni na kuzindua maabara ya Uhandisi Jeni (Biotechnology Laboratory)

Rais Jakaya alipotembelea ARI-Mikocheni

Rais Mhe.Jakaya Mrisho Kikwete akipokelewa katika kituo cha Utafiti wa Kilimo Mikocheni.

Wednesday, April 3, 2013

Mkuu wa nyumba ya Masista wa Vicent wa Paulo

Mkuu wa Masista wa Shirika la Mt.Vicent wa Paulo (mbele) akiwa kwenye maandamano siku ya Sikukuu ya matawi, parokiani Vikindu.

Wanakwaya wa Vikindu

Wanakwaya wa Vikindu walipaza na kupiga ngoma wakiimba Hosana juu Mbinguni!

Maandamano kuelekea Kanisani

Hosana! Hosana juu mbinguni.

Sista na tawi lake

Kila mmoja alipata tawi na kuimba Hosana mwana wa Daudi.

Wanafunzi kwenye Ibada ya Matawi

Ndivyo ibada ya Matawi ilivyoanza Parokiani - Vikindu, nje ya jengo la Masista wa Shirika la Mt. Vicent wa Paulo.

Vikindu Dispensary

Zahanati hii inamilikiwa na masista wa Shirika la Mt. Vincent wa Paulo-Parokia ya Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam, kilomita takribani 35 kutoka katikati ya Jiji la Dar Es Salaam kuelekea wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani.Zahanati hii hutoa huduma za 'maternity' watoto, ushauri nasaha kwa waathirika wa HIV pamoja na huduma nyingine za Afya. Huduma zake ni bora sana hupokea pia bima ya NHIF.

Upanuzi wa Bandari ya Dar Es Salaam

Bandari ya Dar Es Salaam inaendelea kuboreshwa minudo mbinu yake.Kazi hiyo inafanyika usiku na mchana. Banzi wa Moro aliweza kushuhudia jengo moja likisukwa nondo.

Wapo 'Bongo'

Wageni hawa wapo jijini Dar hapa wanachukua usafiri wa Taxi kuelekea mahali watakapofikia.Tanzania ni nchi ya amani na binadamu wote ni ndugu zangu hakuna ubaguzi.

Chuo cha Mabaharia

Watzanzania wengi hawafahamu kilipo chuo cha mabaharia. Vijana wengi hupenda kuwa mabaharia, je wanakifahamu chuo hiki? Ni chuo na zamani lakini kimesomesha mabaharia wengi, kipo kando ya bahari ya Hindi jijini Dar Es Salaam barabara ya Sokoine.

Azam Ferries

Hapa ndipo ofisi za Azam Ferries zilipo jijini Dar. Ukitaka kwenda Zanziba na Unguja hapa ndipo pakuondokea. Pamoja na kuwa na timu ya Soka ya Azam, Mohamed Bakhresa anamiliki boats za kusafiria zenye ubora wa hali ya juu kama vile MV.Kilimanjaro.

Kanisa Kuu la Mt.Joseph - Dar es Salaam

Hili ndilo Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jijini Dar Es Salaam, Tanzania.

Nimerudi

Majukumu ya kazi,kuumia kidole na matatizo ya mtandao yamenifanya kuwa kimya kuanzia mwezi February tarehe 14 hadi leo. Wapenzi wa Banzi wa Moro najua mmesumbuka sana na kujiuliza kilichotokea. Hayo niliyoyataja ni sababu kuu ya kutoning'iniza. Kuna watu walioniuliza vipi Banzi. Poleni sana. Sasa nimerudi.Pichani jiji la Dar na tatizo sugu la traffic jam.

Kempsiki 'perhaps'

Wakati mwingine tunapata shida ya kupata mahali pakujipatia makulaji. Wengi tunafikiri kuwa sehemu nzuri za kupata msosi ni hotelini. Hapa Dar sehemu za kupata chakula ni nyingi zinazojulikana kama mama lishe. Hapa ni 'Kempsiki' ya Temeke Veternary unaweza kunipata hapa muda wa 'lunch'.