Wednesday, July 17, 2013

Ufunguzi wa Kituo cha Utafiti KATRIN -Ifakara

Kituo cha Utafiti wa Kilimo KATRIN kilichopo Ifakara kimefunguliwa rasmi tarehe 22/3/1970  na Baba wa Taifa Mwl. J.K.Nyerere saini yake inapatikana katika kitabu cha wageni cha kituo hicho. Hakika ni kumbukumbu nzuri.

Vifaa vya umwagiliaji katika shamba la utafiti Ilonga

Mhasibu Mwandamizi Christopher Gibbson wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika akishangaa mabomba ya umwagiliaji katika shamba la utafiti Ilonga.

Shambani Lumemo - Ifakara

Toyota-Landcruiser, gari hili linafaa sana kwa shughuli za shambani kama vile za utafiti kilimo. Bw . Omari Kizito na Shuhu Jr wamekuwa wakiendesha gari la aina hii wakiambatana na watafiti vijijini. Hapa wapo kwenye shamba la Utafiti KATRIN katika mto Lumemo-Ifakara.

Dr. Chaboba Mkangwa-Zonal Director Research and Development-Eastern Zone

Utafiti wa zao la mtama na alizeti kituo cha Utafiti Ilonga

Utafiti wa alizeti na mtama umeandelea kufanywa kwa miaka mingi katika kituo cha utafiti Ilonga. Matokeo mazuri yamepatikana kama vile mbegu bora zinazozaa kwa wingi zinazovumilia ukame na magonjwa.


Ushindi ARI-Ilonga

Vikombe vilivyonyakuliwa na kituo cha Utafiti Ilonga ndani ya ofisi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki.

Friday, July 12, 2013

ARI-Ilonga Tanzania


Utafiti wa mtama kituoni Ilonga

Utafiti wa zao la mtama unafanyika katika kituo cha Utafiti Ilonga. Aina za mtama hutafitiwa ili kupata aina inayopendwa kwa matumizi mbalimbali.

Dr. Kasuga - Veteran researcher!

Dr. Louis Kasuga mtafiti wa korosho kutoka Naliendele akiwa kaziniwilayani Kilombero.

Maelezo kutoka kwa watafiti wa mpunga Cholima-Dakawa

Utafiti wa zao la mpunga umeendelea kufanyika nchini Tanzania kwa miaka mingi. Kituo cha Utafiti wa Kilimo Cholima -Dakawa ndiyo waliozalisha mbegu ya mpunga ijulikanoyo kwa jina la SARO 5 ambayo sasa imeanza kusambaa kwa haraka hapa nchini kutokana za sifa zake.

Teknolojia za kilimo cha Kichina kituo cha Dakawa

Mtaalamu wa Kichina wa kituo cha teknolojia za kilimo za Kichina akiwaonyesha wajumbe wa timu A ya kupelemba na kutathmini kanda ya Mashariki mwaka 2013 plot ya maonyesho ya vitunguu.
 

Pepeta za Ifakara!

Pepeta nazo ni tamu - kwa kiingereza zingeweza kuitwa 'Rice flakes' ni sawa kabisa na corn 'flakes'Nilipofika kwenye kivuko cha mto Kilombero nilinunua pepeta kiasi cha kilo tatu kwa gharama ya Tshs 4,500/=.

Trekta ni kila kitu

Huu ni wakati wa mavuno wilayani Kilombero. Pichani trekta likisafirisha mpunga kutoka shambani.

Samaki wa mto Kilombero

Moja ya sifa ya mto Kilombero na samaki wa aina mbalimbali wakiwemo Kitoga, Kambare na Perege.

Monday, July 8, 2013

Daraja la mto Ruaha

Hapa ni Kidatu lilipo daraja la mto Ruaha si mbali sana na mahali panapozalishwa umeme kwa nguvu ya maji. Tegemeo la nishati hapa nchini.

Sunday, July 7, 2013

Mtafiti kijana wa Ilonga

Tanzania imeanza kuajiri watafiti wapya wa Kilimo takribani miaka mitano iliyopita. Pichani mtafiti kijana akitoa maelezo ya utafiti anaoufanya kwenye zao la mahindi kituoni Ilonga.

Mtafiti kijana mwanamke

Mtafiti kijana mwanamke akitoa maelezo ya utafiti kwenye kijishamba cha majaribio katika kituo cha Utafiti Ilonga. Hii ni njia nzuri ya kuwajengea uwezo watafiti vijana na hasa wanawake.

Watumishi wa misa

Hawa wamenikumbusha enzi zangu takribani miaka 40 iliyopita nilipokuwa nikitumikia katika Kanisa la Parokia ya Matombo.Watumishi hawa walitumikia misa takatifu kwenye tamasha la vijana wa Dekania ya Kigamboni.

Masista wakipata msosi

Masista waliohudhuria tamasha la vijana wa Dekania ya Kigamboni wakipata chakula cha pamoja. Masista hawa walionyesha ushirikiano na upendo mkubwa kwa vijana. Walishiriki kwenye ibada hadi kwenye maonyesho ya michezo mbalimbali iliyoonyeshwa na vijana.

Manjonjo ya ngongoti

Kwa kweli ngongoti alileta buradani ya pekee wakati wa tamasha la Vijana wa Dekania ya Kigamboni lilofanyika parokiani Vikindu tarehe 30/6/2013(Picha na John Banzi)