Monday, November 10, 2014

Violet keki kwa wakwe

Nitawahudumia hivi. Ndivyo Violet anavyosema wakati alipokabidhi keki kwa familia ya Mbetwa siku ya tarehe 8 Novemba 2014 kwenye ukumbi wa Marantha-Msimbazi, Dar.

Ndivyo Mpoki na Violet walivyoingia Marantha Hall






Mwenyekiti Pilla na keki ya Kamati

Mwenyeki wa Kamati  Bw. Phillip Pilla akifurahi keki ya Kamati ya Maandalizi ya Harusi ya Bw  & Bi Mpoki Mbetwa siku ya tarehe 8/11/2014

Keki ya Kamati

Hii ndiyo keki ya Kamati aliyokabidhiwa mwenyekiti wetu Bw. Phillip Pilla wa Kamati ya Maandalizi ya harusi ya Bw & Bibi Mpoki Mbetwa.

Mpoki-Ukarimu kwa wakwe


Kutoa keki kwa wakwe ni kuonyesha ukarimu wakati wote na kuwahakikishia wakwe kuwa uko tayari kuwakaribisha nyumbani kwako wakati wowote na kuwa chakula kipo kwani chakula ni UHAI.

Keki ya ukweli

Yes, hii keki si ya kitapeli ni keki ya ukweli. Nilipoila imeivaa lainii kama pamba! Keki ya Bw & Bi.Mpoki Mbetwa.

Special kwa Bw & Bibi Mpoki Mbetwa


Wasindikiza maharusi waliingia hivi


Wasindikizaji maharusi waliwaingiza Bw & Bi Mpoki Mbetwa ndani ya Marantha Hall-Msimbazi jijini Dar siku ya tarehe 8 Novemba 2014  katika style hii. Check wanavyojimwaga!

Wakwe ukumbini



Tuliwapokea ndani ya ukumbi wa Marantha-Msimbazi wakwe zetu kutoka Iringa kusheherekea harusi ya Bw Mpoki Mbetwa na mtoto wao Violet siku ya tarehe 8 Novemba 2014

Huwezi kuwakataza watoto wa familia

Watanzania tumekuwa na tabia mbaya ya kuandika kwenye kadi kuwa watoto hawaruhusiwi kwenye hafla za harusi na sendoffs. Lakini huwezi kuwakataza watoto wa familia. Watajifunzaje kushughulikia matukio haya muhimu wakati tunawakataza? Pichani watoto wa Familia ya Mbetwa wakiwa ukumbini siku ya harusi ya baba yao mdogo Mpoki. Angalia jinsi wanavyoburudika na soda!

Full kuwajibika

Mmoja wa wahudumu akiwajibika ndani ya Marantha Hall - Msimbazi jijini Dar wakati wa sherehe ya reception ya wanandoa Bw & Bi Mpoki Mbetwa siku ya tarehe 8 Novemba 2014.

Violet msanii mwenye sauti nyororo


Kama ungeisikia sauti ya Violet(aliyeshika microphone) akiimba moja ya wimbo wa marehem Whitney Houston ungeamini kuwa Whitney amefufuka! La hasha huyo ni Violet mtoto wa Kinyakyusa aliyekuwa akiwatumbuiza wageni waalikwa na maharusi wakati wa reception ya Bw & Bi Mpoki Mbetwa ndani ya Marantha Hall- Msimbazi jiji Dar. Msichana huyu ana kipaji kikubwa cha uimbaji nangojeea single yake ya kwanza!

Wageni waalikwa harusi ya Mpoki Mbetwa



Hawa ni baadhi ya wageni waalikwa waliofurika katika ukumbi wa Marantha-Msimbazi  jijini Dar wakati wa kusheherekea harusi ya Bw & Bibi Mpoki Mbetwa siku ya tarehe 8 Novemba 2014

Hospitali ya Magomeni

Hospitali ya Magomeni jijini Dar bado ni ileile miaka nenda rudi. Idadi ya watu inaongezeka lakini hali ni ileile.

Wameshindikana?

Hapa ni Jangwani jijini Dar. Nyumba bado zipo. Sehemu hii ya jiji inahistoria ya kukumbwa na mafuriko lakini inaonekana imeshindikana kuwaondoa wakazi wa eneo hili. Tahadhari mvua zinakuja na mafuriko hayako mbali nasi.

'Walk Over' yetu

Wakati wenzetu wanaangolea fly overs, sisi tunajivunia 'walkover' yetu ya Manzese!

Ni wapi hapa?

Kama wewe ni mwana Dar. Nina maana kama wewe ni born city wa Dar tambua mahali hapa.

Barabara ya Kawawa inaandaliwa kwa mabus ya kwenda kasi

Hapa ni Magomeni QTR jijini Dar. Ujenzi wa barabara ya Kawawa kwa matumizi ya mabus ya kwenda kasi unaendelea. Kituo cha mabus hayo kimeshajengwa. Mbele yake linaonekana jengo la Kanisa Katoliki Parokia ya Magomeni lililokarabatiwa.Ndani ya jengo hili  Bw na Bibi Innocent J.Banzi walifunga ndoa yao mwaka 1997.

Vituo vya mabus ya kwenda kasi Dar


Asilimia 90 ya vituo vya mabus ya kwenda kasi jijini Dar imekamilika. Jana nilishuhudia wafanyakazi wa kampuni ya STRABAG inayojenga barabara ya Morogoro wakifanyia marekebisho ya mwisho kabla ya kuanza kutumia vituo hivyo mara barabara itakapofunguliwa rasmi.

Magomeni Mapipa jana

Magomeni Mapipa nilivyoikuta jana jioni baada ya ujenzi wa barabara ya mabus ya kwenda kasi. Wakati ule sisi tunaishi pale Magomeni Qtrs hapa Mapipa hakukuwa na ghorofa hata moja. Wakati tunakwenda Jangwani kuangalia mazoezi ya Simba na Yanga tulikuwa tunakatiza hapo juu. Dar Es Salaam na vitongoji vyake inabadilika kwa kasi ya ajabu!