Friday, February 26, 2010

Tunaita kudandia


Haya ndiyo watoto wetu wanayoweza.
Kijana huyu ni umri wa wanafunzi wa shule za msingi. Sasa tujiulize anadandia bus ili iweje? Hana sare za shule pengine tungesema kuwa anataka kuwahi kwenda shule. Hapa ni Dar hiyo ndiyo Taswira ya Taifa. Picha kutoka Gazeti la Mwananchi la Tarehe 26/2/10

Ushindi ni mazoezi


Asikudanganye mtu, ushindi ni mazoezi tu. Angalia jinsi mlinda mlango wa Twiga Queens (Timu ya Taifa ya Soka ya Wanawake)- Zena Juma anavyojifua kwenye mazoezi. Hii inampa stamina, uzoefu pamoja na mbinu. Hivyo vyote vikikamilika ushindi ni dhahiri. MUNGU IBARIKI TWIGA QUEENS

Mjibu Kipanya basi


Kama wewe mjuzi wa kujibu maswali mjibu kipanya tukate mzizi wa fitina wa rushwa.

Kuna nini UWT



UWT kuna fukuto kali. Vijembe na mambo kadha wa kadha. Wengine hatufahamu chochote. Lakini jinsi nilivyomsikia Makamu wa Mwenyekiti wa chama hicho Bi Asha Makame kwa kipitia TBC 1 jana jioni na leo hii kusoma kwenye gazeti la Mwananchi lenye kichwa cha Habari "Mwilima ajiandaa kujibu mapigo UWT." Gazeti hilo lilimnukuu Mwilima akisema "Mmhh! Napata utata kulijibu hilo, lakini nisema tu kwamba kwa mujibu wa katiba ya UWT, kikao cha Kamati ya Utendaji ndicho kinachoweza kuniondoa," alisema Mwilima.

Tuesday, February 23, 2010

Anauza mikate!


Leo asubuhi nimeinyaka picha hii kutoka kwenye blog ya ndugu yangu Mjengwa. Picha hii imepigwa Zanzibar. Mfanyabiashara huyu raha mustarehe anauza mikate kwenye tenga huku akiitangaza waziwazi bila kufunikwa. Usalama wa afya za walaji je. Hata huku Tanzania Bara tabia hii ya wafanyabiashara kutojali usalama wa afya za walaji ni tatizo sugu. Utaona samaki wa kukaanga wanauzwa barabarani bila kuhifadhiwa, korosho zimewekwa kwenye mafungu na kuguswaguswa na wanunuzi. Hii kwa kweli si tabia nzuri. Wafanyabiashara wajifunze utaratibu mzuri wa kuuza bidhaa zao hasa vyakula.

Monday, February 22, 2010

Kumbe Ulaya nako barabara mbovu kama bongo!


Unaulizwa, kama msichana huyu alikupita wakati ukimuomba lift. Ukimkuta kwenye hali hii utamsaidia?

Hee mizigo mitano kwenye pikipiki!


Mzee anaendesha, huku akipakia binti, nyumba ndogo na mama pamoja na tenga. Wakipata ajali ni kazi ya Mungu? Pikipiki hii haikutengenezwa kwa madhumuni hayo.

Hii ndiyo JWTZ


Kwa mazoezi haya na mengine ambayo hayawezi kuonyeshwa ovyo ovyo. Jeshi letu si mchezo. Mtu akija kicha kichwa ataumizwa vibaya sana oh! Safi sana JWTZ!

Anayesema hakuna chochote kwenye sekta ya KILIMO mwongo


Angalia kwenye picha wataalamu wakiwa kwenye viatu vya kazi (boots) mwangalie Mhe. Dkt Ali Mohamed Shein Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akifurahia shamba zuri la mahindi kwa ajili ya kuzalisha mbegu linalomilikiwa na JKT Mlale wilaya ya Mbinga.

Kisu kimenolewa acha kabisa mchezo


Ndiyo, baada ya kukaa muda mrefu kwa maumivu, Ulimboka Mwakingwe 'Uli' amerudi na makali mapya dimbani kwenye kikosi cha Wekundu wa Msimbazi (SSC). Kasi imeongezeka na shabaha ya goli kama kawa! Kuna nini tena mbona kazi kwisha. Ubingwa ni dhahiri mwaka huu. Pichani Uli katika kasi yake akimtoka Stephen Mwasika wa Moro United katika mchezo wa ligi kuu uwanja wa UHURU hapo jana (21/02/2009). Simba ilishinda kwa magoli 4-1. Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi.

Friday, February 19, 2010

Kumbe chocolate kwa kiswahili ni kashata!


Hii nimeinyaka leo kutoka blog ya uncle Michuzi. Kuna chocolate inayotenngezwa kwa jina la Tanzania. Nasikia inapendwa sana huko majuu. Sasa uncle yeye ameiita ni kashata. Sikujua kama chocalate ndiyo kashata. Tuanze kutumia sasa mtoto akitaka chocolate dukani basi tunasema nipe kashata mbili za maziwa (milk chocolate)!

Vyakula dawa vinavyorefusha maisha



Leo katika pekuapekua yangu nimekuta kilichotayarishwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kinachoelezea vyakula dawa vinavyorefusha maisha kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

Vyakula hivyo ni Viungo (husaidia kutuliza au kutibu matatizo ya afya kama kutapika, kuharisha, mafua, kichefuchefu na kujaa gesi tumboni. Mboga na Matunda ni chanzo cha vitamini na madini muhimu mwilini husaidi kuongeza damu, uzito na vitamini A . Mimea kama ubuyu wenye vitamini C hutuliza mafua na kuongeza hamu ya kula, choya (rozela) husaidia pia kuongeza damu. Shubiri (alovera) husaidia kutibu magonjwa mbalimbali yakiwemo malaria na kisukari. Kipeperushi hicho kinapatiokana kupitia barua pepe: psk@kilimo.go.tz

Magufuli anatuambia nini kuhusu utafiti wa kuku wa asili?


Katika Taarifa ya mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya nne. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akielezea mafanikio yaliyopatikana kutoka utafiti wa kuku wa asili ni kwamba kuku wa asili anapopewa chakula cha ziada badala ya kujitafutia chakula wao wenyewe; utoaji wa mayai unaongezeka kutoka wastani wa mayai 10 hadi kufikia kati ya mayai 18 hadi 25 kwa mtago. Ukuaji wa vifaranga unaongezeka kutoka wastani wa gramu kati ya 3 hadi 5 hadi kufikia wastani wa gramu 8 na 10 kwa siku. Kiwango hiki cha ukuaji kinaonyesha kuwa kuku anaweza kufikia kati ya kilo 1.5 hadi kilo 2 kwa kipindi cha miezi 6 tu. Aidha kuachisha makinda/vifaranga ndani ya wiki 4 kunaongeza idadi ya mitago kutoka kwa wastani 2-3 kwa mwaka hadi wastani wa mitago 6 - kwa kolowa kwa mwaka na hivyo kuongeza idadi ya mayai kutoka wastani wa mayai 40-60 hadi 90-120 kwa kolowa kwa mwaka. Matokeo haya ni mazuri ni ni changamoto kwa wafugaji. Nyama ya kuku wa asili ni tamu sana tujitahidi kufuga.

Watoto na UKIMWI waambiwe kila kitu?


Ugonjwa wa UKIMWI ni balaa katika dunia. Bara la Afrika limepigika zaidi kwa ukimwi hakuna kaya isiyoathirika kwa UKIMWI.

Mikakati mingi imepangwa kupambana na ugonjwa huo ambao hadi sasa hauna tiba. Baya zaidi ni kwa watoto ambao ndiyo wanaojenga taifa la baadaye. Kuna swali je, WATOTO waambiwe kila kitu kuhusu UKIMWI? Ukizingatia uchumi, utamaduni na mazingira ya mwafrika? Tuelimishane.

Huyo ndiye ROONEY!


Wayne Rooney ni mpachika magoli maarufu kwa sasa wa timu ya soka ya Manchester United ya Uingereza ni mchezaji anayependa soka na kulicheza kwa kiwango cha juu kabisa. Awapo uwanjani Rooney hujituma sana katika kupachika magoli si mtu wa kumwacha pekee hata kidogo ni hatari kwa timu pinzani.

Akitolewa nje na kocha wake huwa anakuwa na ghadhabu isiyosemeka. Rooney anawea kupiga ngumi ukuta, anaweza kuvua gloves na kuzibwaga chini au kufanya lolote lile. Lakini utampenda akifunga goli. Husheherekea kwa mbwembwe zote unazozifahamu anaweza kuserereka kwa magoti bila kujali kuchubuka. Pichani Rooney (mwenye glovu nyeusi) akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga goli.

Tuesday, February 16, 2010

Woman=problems

Tafakari

Tutaukumbuka Mradi wa Minazi


Tanzania tuna bahati kubwa sana ya kustawisha mazao ya aina mbalimbali katika ekolojia tofauti. Kwa kuwa tuna bahari kuna mazao yanayostawi ukanda wa pwani. Kwa kuwa tuna sehemu za nyanda za juu tuna mazao yanayostawi huko kama vile ngano pamoja na matunda ya nchi zenye baridi za ulaya.

Nazi ni zao linalostawi sehemu nyingi hapa nchini lakini kwa miaka ya hivi karibuni upatikanaji wake umekuwa ni wa shida sana hata kusababisha bei ya nazi pamoja na madafu kupanda kwa haraka sana. Uzalishaji wake umeshuka kwa kuwa minazi mingi hukatwa kupisha makazi ya watu hasa sehemu za Pwani. Vilevile magonjwa yamesababisha minazi mingi kusinyaa hivyo kushusha uzalishaji.

Zao la nazi miaka ya 80 hadi 90 lilikuwa likishughulikiwa sana na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi (National Coconut Development Project-NCDP). Mradi huu ulifanya kazi kubwa licha ya dosari ndogo ndogo zilizojitokeza baada ya kumalizika kwa mradi hasa kwa mbegu fupi kutokubaliwa na wakulima wengi baada ya kuona kuwa huchakaa baada ya muda mfupi.

Hali ikiendelea hivi bila kuchukua hatua madhubuti uzalishaji wa nazi utashuka mwaka hadi mwaka na madafu nayo yataadimika na be itapanda sana.

Thursday, February 11, 2010

Wakati Wamisri wakiomba dua muone huyo mchezaji wa Ivory Coast!


Hivi kweli huu ni ustaarabu au imani za kishirikina. Bila aibu mchezaji huyu wa Ivory Coast anakojoa uwanjani. Lakini mpiga picha makini aliinyaka hii na sasa imevuja kwenye mtandao. Pamoja na hayo yote Ivory Coast walibamizwa na Misri

ATHARI ZA KUPUNGUZA WAFANYAKAZI


Hebu soma hiyo taswira hapo juu. Wazungu wanarudi nyuma na kung'amua kuwa kupunguza wafanyakazi kuna athari kwa wafanyakazi wanaopunguzwa, uchumi pamoja na mambo mengine. Hili ni fundisho kwetu. Tulibeba kwa haraka sera ya kupunguza wafanyakazi bila kuangalia madhara yake sekta nyingi hivi sasa hapa nchini zina uhaba wa wataalamu. Wataalamu waliopo sasa wanastaafu hivyo kulazimika kuwaajiri kwa mkataba. Tutakujakung'amua hapo baaye kuwa hata ajira za mkataba zina madhara yake

Madega-Hivi Yanga wanaweza kutupa raha au kutuaibisha?

Madega, Young Africans haina historia nzuri kwenye mashindano ya kimataifa. Hivi hatutegemei kuwa itatupa raha uliyoisema. kwa mpira gani? Wanaweza kufurukuta tu hapa nyumbani kwa ushindi wa kupangwa! Hivyo mimi sina mpango wa kuja uwanja wa Taifa kuiona Yanga ikituaibisha.