Royal Pub ni mahali pa zuri pa kupata chakula na kinywaji ukiwa wilayani Ruangwa mkoa wa Lindi. Ilibidi nipige picha. Ruangwa bomba sana!
Friday, June 3, 2011
Na hapa ni Ruangwa
Royal Pub ni mahali pa zuri pa kupata chakula na kinywaji ukiwa wilayani Ruangwa mkoa wa Lindi. Ilibidi nipige picha. Ruangwa bomba sana!
Wachaga kwa nyama!
Hii siyo gari yetu.
Maelezo ya ziada kutoka kwa mtafiti
Mwache mkulima ajieleze
Utafiti shambani kwa wakulima. Huko Mtama, Lindi kikundi cha wakulima kinafanya utafiti wa zao la embe. Pichani mkulima mwanamama akijieleza.Tulimsikiliza na kumuuliza maswali na alitujibu barabara. Kijiji hiki kimo ndani ya jimbo la Mh. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Huyo ni nani?
Watafiti wanasubiri kwenda Kilwa vijijini
Taxi za Kilwa babu kubwa
Ukiambiwa kwenda kufanya kazi Kilwa Masoko utafikiri kama umepewa adhabu. Huo ni mtazamo wa zamani. Mwisho wa mwezi huu nilikuwa Kilwa Masoko kikazi. Kilwa mambo ni kama hivi:-
-hakuna kukatika umeme (umeme wa songas)
-magari aina ya Noah niyo Taxi zao (Kilwa- Nangurukuru)
-Samaki ndo usiseme (wa kukaanga,supu au wa kuungwa)
-wali kwa nazi
-kuku wa kienyeji!
-Guest bei poa na ni self contained
-beach safi
-Ulabu kama Dar tu
Baiskeli Kilwa
Tufunge zawadi
Hongera Banzi
Vituo vya Radio vilikuwa hewani
Mapadri walitoa Baraka
Subscribe to:
Posts (Atom)