Dada Irine Kibena tunamuandaa kuwa mlimbwemde wa Tanzania miaka michache ijayo. Angalia pozi yake akiwa kwao Kola, Morogoro.
Friday, July 1, 2011
Tunamuandaa kuwa Miss Tanzania
Dada Irine Kibena tunamuandaa kuwa mlimbwemde wa Tanzania miaka michache ijayo. Angalia pozi yake akiwa kwao Kola, Morogoro.
Kwetu sisi ndizi ni kitafunwa tu
Kwa wenyeji wa Morogoro kawaida ndizi huliwa zikiwa mbivu au kama vitafunwa (kwa kunywea na chai). Huwezi ukapikiwa ndizi halafua ukasema kuwa leo nimekula chakula. Hata kama watachanganya na nyama bado ni vitafunwa tu. Chakula cha heshima kwetu ni wali! Angalia mikungu ya ndizi nyuma ya nyumba - Kola, Morogoro mjini.
Pikipiki inapovaa 'helmet'
Malongoza mtaalamu wa kuandaa chakula cha shughuli - Morogoro
Mpishi Malongoza wa Morogoro ni maarufu kwa kupika chakula cha shughuli. Hana papala na anajali muda. Anatayarisha chakula kwa umakini mkubwa hatua kwa hatua na ukimuuliza atakupa sababu. Nilishangaa nipoona anamwagia mafuta sufuria la kupikia. Akanieleza kuwa sababu yake iwe rahisi wakati wa kuosha. Lakini sikumuelewa pale aliponieleza kuwa anamwaga chumvi pembeni ya jiko ili chakula kiwe kitamu! Huyu ndiye Malangoza mtaalamu wa maakuli -Morogoro.
Kuna wazungu na Africana pia
Mkude wa Morogoro
Huyu ni ndugu 'mtoto' wangu anaitwa Mkude. Kwa kuzingatia taratibu za mila za Kiluguru mimi ni Baba Mkude. Lakini mimi ni Banzi au Jaka, Zinga na dada zangu wanaitwa akina Kimbiki ni watoto wa Wambiki. Watoto wangu wanastahili kuitwa akina Mkude, Mizambwa, Mdoti, Midahuli.. (wanaume) na ikiwa mwanamke anaitwa Mwenda au Mlamwenda. Kwa hiyo huyo ni ndugu yangu na ni mtoto wangu. Morogoro akina Mkude,Banzi, Mloka, Mwenda, Mbiki,Mbena, Luanda, Mtonga tukiwa nyumbani tunatumia jina la kwanza kutotofautisha!
Familia ya Morogoro
Wednesday, June 29, 2011
Wednesday, June 22, 2011
Trekta letu
KATRIN kujengewa uwezo
Utafiti wa Mifugo Uyole - Mbeya
ASA-Mkataba wa Huduma kwa Mteja
Dakawa-Kituo cha usambazaji wa Teknolojia
SARO- Nyumbani kwake Cholima-Dakawa
Ni madaraja
Friday, June 17, 2011
Chini ya Daraja la Umoja
Nangurukuru
Nyama choma na supu ya mbuzi ok!
Subscribe to:
Posts (Atom)