Friday, July 1, 2011

Tunamuandaa kuwa Miss Tanzania


Dada Irine Kibena tunamuandaa kuwa mlimbwemde wa Tanzania miaka michache ijayo. Angalia pozi yake akiwa kwao Kola, Morogoro.

Kwetu sisi ndizi ni kitafunwa tu


Kwa wenyeji wa Morogoro kawaida ndizi huliwa zikiwa mbivu au kama vitafunwa (kwa kunywea na chai). Huwezi ukapikiwa ndizi halafua ukasema kuwa leo nimekula chakula. Hata kama watachanganya na nyama bado ni vitafunwa tu. Chakula cha heshima kwetu ni wali! Angalia mikungu ya ndizi nyuma ya nyumba - Kola, Morogoro mjini.

Pikipiki inapovaa 'helmet'



Kwa kawaida waendesha pikipiki wanatakiwa kuvaa helmet (kofia za kujikinga na kichwa) waendeshapo vyombo hivyo. Banzi wa Moro ilinyaka scene hii pale Kola-Morogoro wakati mwendesha pikipiki alipodondosha helmet na baadaye kuifunga nyuma ya pikipiki. Angalia picha pmbili ya juu na kushoto.

Malongoza mtaalamu wa kuandaa chakula cha shughuli - Morogoro






Mpishi Malongoza wa Morogoro ni maarufu kwa kupika chakula cha shughuli. Hana papala na anajali muda. Anatayarisha chakula kwa umakini mkubwa hatua kwa hatua na ukimuuliza atakupa sababu. Nilishangaa nipoona anamwagia mafuta sufuria la kupikia. Akanieleza kuwa sababu yake iwe rahisi wakati wa kuosha. Lakini sikumuelewa pale aliponieleza kuwa anamwaga chumvi pembeni ya jiko ili chakula kiwe kitamu! Huyu ndiye Malangoza mtaalamu wa maakuli -Morogoro.

Kuna wazungu na Africana pia


Ndiyo kwenye familia yetu kuna sisi weusi na wenzetu weupe lakini sote tumetoka kibanda kimoja Africana! Pichani Banzi na mtoto wa mjomba Beatus nyumbani Morogoro.

Mkude wa Morogoro


Huyu ni ndugu 'mtoto' wangu anaitwa Mkude. Kwa kuzingatia taratibu za mila za Kiluguru mimi ni Baba Mkude. Lakini mimi ni Banzi au Jaka, Zinga na dada zangu wanaitwa akina Kimbiki ni watoto wa Wambiki. Watoto wangu wanastahili kuitwa akina Mkude, Mizambwa, Mdoti, Midahuli.. (wanaume) na ikiwa mwanamke anaitwa Mwenda au Mlamwenda. Kwa hiyo huyo ni ndugu yangu na ni mtoto wangu. Morogoro akina Mkude,Banzi, Mloka, Mwenda, Mbiki,Mbena, Luanda, Mtonga tukiwa nyumbani tunatumia jina la kwanza kutotofautisha!

Familia ya Morogoro


Familia yangu ni kubwa sana. Hapa ni Morogoro- Kola, nyumbani kwa Babu yangu-Unaowaona ni dada zangu na wadogo zangu watoto wa wajomba zangu. Tulikuwa kwenye 40 ya mama mdogo na dada.

Wednesday, June 29, 2011

Morogoro inapendeza

Hapa ni Morogoro pale Kola karibu na makaburi njia ya kwenda nyumbani Matombo.

Wednesday, June 22, 2011

Trekta letu

Sijatembelea maonyesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea hapa jijini katika viwanja vya Mnazi Mmoja. Lakini kitu kilichonivutia ni kusoma ndani ya blog ya Mjengwa kuwa kuna trekta lililobuniwa na Mtanzania ambalo lina uwezo wa kulima ekari 5 kwa siku. Linaweza kusaga nafaka na pia kutoa nishati ya umeme. Haya ni maendeleo makubwa katika nyanza ya sayansi na Teknolojia. Trekta hili lilibuniwa na CARMATEC-Arusha mwaka 2008 na Dr. Patric Jonathan

KATRIN kujengewa uwezo


Kituo cha Utafiti - KATRIN kilichopo Ifakara mkoani Morogoro kinatazamiwa kuwa Kituo Mahiri cha Utafiti wa Mpunga (RRCoE)katika Afrika Mashariki na Kati chini ya Programu ya Kuendeleza Tija katika kilimo Afrika (EAAPP).Picha ya juu Mratibu wa Mradi wa Kituo Mahiri Bw. Nkori Kibanda akitoa maelezo ya jinsi mradi huo unavyotekelezwa na mahitaji ya kujengewa uwezo hasa kwa watumishi ili waweze kufanya kazi zao kwa ufasaha na hatimaye kufanikisha lengo.

Utafiti wa Mifugo Uyole - Mbeya


Dkt. Pilika Mwakilembe akifanunua jambo ofisini kwake Uyole,alipotembelewa na Banzi wa Moro hivi karibuni.

ASA-Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Tayari Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) wameshaandaa. Mkataba wa Huduma kwa Mteja. Ndani ya Mkataba imewekwa bayana huduma zitolewazo na Wakala hii na jinsi huduma anavyopaswa kuhudumiwa. Lengo ni kutoa huduma za mbegu zenye ubora wa hali ya juu ili kuweza kuongeza tija katika kilimo.

Dakawa-Kituo cha usambazaji wa Teknolojia


Kituo kipya cha usambazaji wa teknolojia za kilimo kimejengwa Dakawa-Morogoro kwa msaada wa Serikali ya China kimefunguliwa mwaka huu na Rais wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete

SARO- Nyumbani kwake Cholima-Dakawa


Moja ya vituo vya Utafiti wa Kilimo kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro. Kituo hiki kilizinduliwa mwaka 1985 na Rais wa awamu ya Kwanza Mhe. Julius K.Nyerere. Kimejengwa kwa ushirikiano na wa Jamhuri ya Korea Kaskazini. Shughuli zake kuu ni utafiti wa mpunga. Aina ya mbegu ya mpunga SARO nyumbani kwake ni hapa.

Ni madaraja



Ukisafiri kwa kutumia gari kutoka Mikumi kwenda Ifakara kitu kimoja ambacho ni dhahiri kukiona ni madaraja. Mojawapo ni hilo hapo juu la Mikumi ambapo reli inapita juu na hili la kulia la Ruaha.

Friday, June 17, 2011

Chini ya Daraja la Umoja

Ukitembelea kijiji cha Mtamba swala-Nanyumbu na kuliona daraja la Msumbiji utashangaa sana.Pichani- Mshana,Kadeng'uka na Banzi chiniya daraja la Umoja.

Mgahawa wa Kituo cha mabus-Masasi

Huu ni mgahawa maarufu Masasi.Hapa nilipata chapati moja,na supu ya kuku wa kienyeji!

Zawadi kutoka Msumbiji

Kweli imetengezwa Msumbiji!

Nangurukuru

Hapa ndipo panaitwa Nangurukuru ni maarufu kwasamakiwakukaanga. Ni kituo maarufu sana wakati unaelekea Lindi kupitia barabara ya Kilwa. Kiko njia panda ya kwenda Kilwa Masoko. Angalizo usikurupukekununua samaki wakukaanga hovyo hovyo hapa na kubugia. Mimi yalinikuta!

Nyama choma na supu ya mbuzi ok!


Endapo utafiti wa kupata aina bora za mbuzi utafanikiwa,tutaongeza uzalishaji wa mbuzi na kufaidi matunda yake kama hivi.