Thursday, March 20, 2014

Busu la hongera kwa mwana

Mama mkubwa na mdogo wakimpongeza binti yao Mwajuma Pembe wakati wa hafla fupi ya kumfunda iliyofanyika  kijijini Kisemvule hivi karibuni.

Pilau 'original'- matandu yapo

   Hii ndiyo pilau original a.k.a wali mchafu! Kipunga hiki ni kitamu sana

Zawadi ya mwavuli

                     Bi. Mwajuma Pembe akiwa na zawadi yake ya  mwavuli aliyozawadiwa wakati wa harusi yake iliyofanyika nyumbani kwao Kisemvule, wilayani Mkuranga. HONGERA

Wednesday, March 19, 2014

Ajali barabara ya Morogoro

Ajali inapotokea ni hasara tupu kwa gari na biashara. Angalia jinsi mahindi yalivyasambaratika  katika ajali hii.

Alama za barabarani


Alama za barabarani zimesimikwa kando ya barabara ya Tanzania-Zambia. Swali, madereva wanazielewa maana ya alama hizi na kuzitumia?

Dr. Deogratias Lwezaura - Mchumi Mkuu Wizara ya Kilimo

Dr. Deogratias Nshoro Lwezaura  Mchumi  Mkuu kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika

Mapambazuko kuelekea Dar


Safari ya asubuhi kutoka Morogoro kwenda Dar ni mapambazuko

Traffic Police kazini

Mwanamama huyu Askari wa barabarani anaimudu kazi yake?

Betty na Agnes akina mama Watafiti wachumi

Betty Chalamila kushoto na Agness Ndunguru ni watafiti wachumi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika wakiwa kwenye kikao cha kazi cha kuandaa taarifa ya Followup Survey ya mradi wa EAAPP kilichofanyika mjini Morogoro mwezi Machi 2014

Ajali barabara ya Morogoro

Barabara ya Morogoro haikosi ajali. Pichani ni ajali ya magari tanker za mafuta iliyotokea Chalinze hivi karibuni. Moja ya sababu za ajali za mara kwa mara inasemekana ni madereva kusinzia.

Maghorofa ya Chalinze


Julieth na Rosalina



 Tumetoka Morogoro. Bibi Julietha Madenge na mjukuu wake Rosalina.

Monday, March 10, 2014

Makazi ya Wamasai

Haya ni makazi ya Wamasai - Monduli, Tanzania

Hali ya nchi Monduli

Monduli ni sehemu tambarare sana yenye vilima vichache vilivyojitokeza

Ndama ana nyonya

Tukiwa njiani kurudi Arusha sehemu za Monduli nilishuhudia ndama huyu akinyonya.

Mtalii ndani ya kibajaji

Vibajaji ni uasafiri unaopendwa sana na watalii kati ya Mto wa Mbu na Monduli. Pichani mtalii akiwa ndani ya Bajaj.

Shabiki wa Yanga - kutoka mji wa Mto wa Mbu-Manyara

Ushabiki wa mpira wa miguu nchini  Tanzania ni wa timu mbili ni Simba na Yanga. Hapa Mto wa Mbu nilimkuta shabiki huyu wa Dar Young Africans. Kwa mtindo huu Mbeya City wana kibarua kikubwa cha kuwa mabingwa wa Tanzania!

Mfereji msafi -Mto wa Mbu

Moja ya vitu vilivyonivutia nikiwa Mto wa Mbu-Manyara ni kuona mifereji misafi sana na iliyotengenezwa kwa uimara wa hali ya juu. Nikawa nalinganisha na ile mifereji iliyopo jijini Dar Es Salaam. Loh kichefuchefu! Angalia pia jinsi sehemu ya waenda kwa migu na baiskeli ilivyotengwa.

Moja ya Mitaa ya Mto wa Mbu-Manyara

Huu ni mmoja wa mtaa wa Mto wa Mbu mkoani Manayara. Sehemu hii ni ya bonde. Mafuriko yanapotokea ni balaa. Lakini sehemu hii ni maarufu kwa kilimo cha Mpunga na mbogamboga. Hivi sasa kimeanza kuwa maarufu kwa watalii.

Wakulima wa Mto wa Mbu mafunzoni


Mwishoni mwa mwezi Februari 2014 nilikuwa Mto wa Mbu kikazi. Hapa nilitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu mapatano katika manunuzi hasa ya mbegu bora ya mpunga. Pichani niko na wakulima na wadau wengine walioshiriki mafunzo hayo.