Monday, November 17, 2014

Neema Kirway-Mahali ukumbini









Baadhi ya vitu vya mahali vilitolewa ukumbini siku ya kumuaga Bi. Neema Timothy Kirway. Inawezekana hii ni mila ya utamaduni wa Wairaq. Babu, Bibi, Mama na Baba, wajomba,baba wadogo, mama wadogo,shangazi na wadogo zake Neema walipata mgao wao.Kwa kweli ilipendeza sana. Jamani eeh tuuenzi utamadani wetu.

Neema Kirway akiingia ndani ya ukumbi wa Best Choice

Bi Neema Timothy Kirway aliingia ndani ya ukumbi wa Best Choice - Tabata Aroma namna hii akisindikizwa na kaka yake. Siku hizi imekuwa ni style ya aina yake kwa mabinti waagwa  kusindikizwa na ndugu zao wa kiume.

Send off ya Neema Kirway ndani ya Best Choice Hall


Walipendeza kwa mavazi yao ya heshima na pia walijimwaga uwanjani kwa nyimbo za utukufu wa Mungu. Hivi ndivyo ilivyokuwa siku ya Sendoff ya Neema Timothy Kirway siku ya Ijumaa tarehe 14/11/2014 ndani ya ukumbi wa Best Choice jijini Dar.

Biashara ni kujitangaza


Vipeperushi hivi nilivikuta ndani ya ukumbi wa Best Choice uliopo Tabata Aroma. Ni kampuni ya Happiness ikijitangaza kwa huduma za Cake, nguo za maharusi na mambo mengine. Nami sina sababu ya kutomrusha kwenye Banzi wa Moro. Biashara ni matangazo.

Wednesday, November 12, 2014

King Mswati III wa Swaziland

Siyo kama hana suti, bali anadumisha utmaduni wa nchi yake ya Swaziland.Huyu ni Mfalme Mswati wa III wa Swaziland. Mfalme huyu hata akipokea wageni mashuhuri ofisini kwake utamkuta katika mavazi hayo. Lakini pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi ya Swaziland wakati mwingine hutilia combat!

Tido Muhando-Mwandishi nguli

             Huyu ndiye Mwandishi wa habari wa Kimataifa Dunstan Tido Mhando. Mwandishi mahiri    na     mtangazaji pia. Enzi zake alipokuwa Radio Tanzania alikuwa akitangaza vizuri sana kipindi cha michezo na hasa matangazo ya moja kwa moja ya soka. Alipokuwa BBC alikuwa akitupasha habari kemkem kutoka Bara la Afrika. Amefanya mahojiano na marais mashuhuri wa Bara la Afrika akiwemo Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere, Hayati Laurent Kabila aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Rais Paul Kagame na Rais Yoweri Mseveni. Katika mahojiano yake na Hayati Laurent Kabila ilibainika kuwa alikuwa shabiki mkuwa wa klabu ya Soka Simba ya jijini Dar, Tanzania.

Kilimo cha bia

Kilimo cha bia. Shamba limeandaliwa vizuri. Variety ya mbegu (bia) inaonekana na spacing inaonekana vizuri tu tena zimepandwa kwa mstari. Zitavunwa lini? Hatujui na matarajio ya mavuno kwa hektari ni bia ngapi. Kweli duniani kuna mambo kila mtu anafikiri nini na ni kipi ni kipaumbele chake. Mtu kufikiri kupanda bia ili azivune nyingi basi upeo wa juu kabisa wa kufikiri. Picha hii nimeipata kwenye mtandao wa fb kuna wengi waliotoa maoni yao kuhusu picha hii wengine walibaki kutoa sentensi za kushangaa na wengine walidai pengine ndio zitakuwa kali zaidi!

Monday, November 10, 2014

'Togwa limeingia nzi'

Mdudu nzi kwa asilimia kubwa hapendwi na wanadamu. Mbwiga wa Mbwiguke wa Clouds huwa anasema kuwa 'Togwa limeingia nzi.' Ninavyoelewa mimi togwa ni kinywaji baridi cha asili hasa kwa watu wa Pwani  ni tamu kwa sababu huongezwa sukari kwa maana hiyo lisipotunzwa vizuri mdudu nzi hunyemelea na kwa kuwa nzi ni mdudu mchafu, anapoingia kwenye togwa basi hulichafua na kuwa halifai tena kwa kunywa. Utafakari usemi huu.

MC Mwakajumba

Huyu ndiye MC Mwakajumba (Mwenye microphone) aliyesherehesha reception ya Bibi na Bw. Mpoki Mbetwa ndani ya Ukumbi wa Marantha-Msimbazi jijini Dar  tarehe 08 Novemba 2014

Bw & Bibi Mpokigwa Mbetwa



Tutakuwa tukilishana hivi daima. Sisi ni mwili mmoja ndivyo ilivyokuwa wakati Bibi & Bw Mpoki Mbetwa walipokuwa wakilishana keki ya upendo siku ya harusi yao tarehe 8 Novemba 2014

Violet keki kwa wakwe

Nitawahudumia hivi. Ndivyo Violet anavyosema wakati alipokabidhi keki kwa familia ya Mbetwa siku ya tarehe 8 Novemba 2014 kwenye ukumbi wa Marantha-Msimbazi, Dar.

Ndivyo Mpoki na Violet walivyoingia Marantha Hall






Mwenyekiti Pilla na keki ya Kamati

Mwenyeki wa Kamati  Bw. Phillip Pilla akifurahi keki ya Kamati ya Maandalizi ya Harusi ya Bw  & Bi Mpoki Mbetwa siku ya tarehe 8/11/2014

Keki ya Kamati

Hii ndiyo keki ya Kamati aliyokabidhiwa mwenyekiti wetu Bw. Phillip Pilla wa Kamati ya Maandalizi ya harusi ya Bw & Bibi Mpoki Mbetwa.

Mpoki-Ukarimu kwa wakwe


Kutoa keki kwa wakwe ni kuonyesha ukarimu wakati wote na kuwahakikishia wakwe kuwa uko tayari kuwakaribisha nyumbani kwako wakati wowote na kuwa chakula kipo kwani chakula ni UHAI.

Keki ya ukweli

Yes, hii keki si ya kitapeli ni keki ya ukweli. Nilipoila imeivaa lainii kama pamba! Keki ya Bw & Bi.Mpoki Mbetwa.

Special kwa Bw & Bibi Mpoki Mbetwa


Wasindikiza maharusi waliingia hivi


Wasindikizaji maharusi waliwaingiza Bw & Bi Mpoki Mbetwa ndani ya Marantha Hall-Msimbazi jijini Dar siku ya tarehe 8 Novemba 2014  katika style hii. Check wanavyojimwaga!

Wakwe ukumbini



Tuliwapokea ndani ya ukumbi wa Marantha-Msimbazi wakwe zetu kutoka Iringa kusheherekea harusi ya Bw Mpoki Mbetwa na mtoto wao Violet siku ya tarehe 8 Novemba 2014

Huwezi kuwakataza watoto wa familia

Watanzania tumekuwa na tabia mbaya ya kuandika kwenye kadi kuwa watoto hawaruhusiwi kwenye hafla za harusi na sendoffs. Lakini huwezi kuwakataza watoto wa familia. Watajifunzaje kushughulikia matukio haya muhimu wakati tunawakataza? Pichani watoto wa Familia ya Mbetwa wakiwa ukumbini siku ya harusi ya baba yao mdogo Mpoki. Angalia jinsi wanavyoburudika na soda!