Kitu ambacho nilikuwa sifahamu ni jinsi unavyoweza kuvuna bamia. Bamia linaweza kuvunwa mara mbili kwa siku, asubuhi na jioni. Kuna mtu ameninong'oneza. Bamia wakati wowote hukua, tena kwa haraka ukichelewa linakomaa na hivyo kuwa gumu na kutofaa kuliwa kama mboga labda kulitunza kwa mbegu.Hivi sasa navuna bamia katika sehemu ndogo niliyolima pale nyumbani kwangu Kisemvule. Kweli kilimo cha bamia ni kama ufugaji wa kuku wa mayai.
Tuesday, June 21, 2016
Thursday, May 19, 2016
Tanzania imepania kuongeza uzalishaji wa mpunga
Mpunga ni zao linalostawi vizuri katika sehemu nyingi za nchi yetu hasa ukanda wa pwani na mabonde yanayozunguka maziwa yetu na inakopita mito mikubwa. Wakulima wengi huzalisha wastani wa tani 2 kwa hekta ambapo ni kidogo sana. Utafiti uliokwishafanyika hapa nchini unaonyesha kuwa kwa kutumia teknolojia bora za kilimo cha mpunga, uzalishaji unaweza kufikia tani 8
kwa hekta. Hivi sasa serikali inaboresha kilimo hicho kupitia miradi mbalimbali hasa kwenye skimu za umwagiliaji.
kwa hekta. Hivi sasa serikali inaboresha kilimo hicho kupitia miradi mbalimbali hasa kwenye skimu za umwagiliaji.
Ni changamoto
Wapenzi wa Banzi wa Moro nimerudi kuwajuza.
Inapotokea kuwa na njia mbalimbali za kupeana habari na msambazaji habari ni huyohuyo ni changamoto kwa kweli. Kuingia kwa facebook na whatsapp kwa kweli kumeimomonyoa blog yangu. Inakuwa vigumu kupost kwenye blog. Naweza kupost kutoka whatsapp kwenda facebook tukio hilohilo lakini siwezi kufanya hivyo kwenda kwenye blog. Uzuri wa whatsapp na facebook ni rahisi kupata feedback hivyo kukufanya kuandika na kupost. Hata hivyo nimerudi, nitaanza kuning'iniza kadri ninavyoweza nipatapo wasaa.
Dereva Mwandamizi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Ndg.Shushu Kondowe akiwasilisha taarifa ya mafunzo kwa mratibu wa mafunzo Bw. John Banzi
Inapotokea kuwa na njia mbalimbali za kupeana habari na msambazaji habari ni huyohuyo ni changamoto kwa kweli. Kuingia kwa facebook na whatsapp kwa kweli kumeimomonyoa blog yangu. Inakuwa vigumu kupost kwenye blog. Naweza kupost kutoka whatsapp kwenda facebook tukio hilohilo lakini siwezi kufanya hivyo kwenda kwenye blog. Uzuri wa whatsapp na facebook ni rahisi kupata feedback hivyo kukufanya kuandika na kupost. Hata hivyo nimerudi, nitaanza kuning'iniza kadri ninavyoweza nipatapo wasaa.
Dereva Mwandamizi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Ndg.Shushu Kondowe akiwasilisha taarifa ya mafunzo kwa mratibu wa mafunzo Bw. John Banzi
Thursday, March 31, 2016
Wednesday, March 2, 2016
Wataalamu wa ERPP ofisini Mvomero
Mradi wa kuongeza uzalishaji wa Mpunga (ERPP) umeshaanza. Mradi huu utatekelezwa katika wilaya tatu za mkoa wa Morogoro (Mvomero,Kilosa na Kilombero). Skimu za umwagiliaji zitahusika nazo ni Kigugu, Mbogo-Kamtonga, Mvumi, Njage na Msolwa. Pichani wataalamu wakielezea jinsi mradi huo utakavyotekelezwa ndani ya ofisi ya Mkurugenzi wa Maendeleo Halamshauri ya Mvomero (Haonekani).
Padri Abdoni Antipas Nzegesela akisoma Injili
Padri Abdoni Antipas Nzegesela ni Paroko wa Parokia ya Ilonga iliyoko Kilosa- Kanisa Katoliki jimbo la Morogoro. Pichani anaonekana akisoma Injili ndani ya Kanisa Katoliki Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Ndiye aliyefungisha ndoa ya Bw. Macarios Banzi na Bi. Martina Jeremias siku ya tarehe 6/02/2016
Bango bora la Shule ya Msingi Kisemvule
Huenda likawa bango bora kabisa kwa shule za msingi za wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani. Ni shule ya msingi Kisemvule. Kila kitu kiko wazi.Huu ni ubunifu wa mwalimu mku wa shule hiyo ambaye amehamishiwa hapo shule hivi karibuni. Nilipouliza gharama ni Tshs 150,000/= na kiasi kikubwa cha fedha kimetolewa na Serikali ya Kijiji cha Kisemvule. Hongera Mwenyekiti na Kamati yako ya Kijiji. Kujitangaza ni maendeleo pia!
Skimu ya umwagiliaji ya Msolwa kuboreshwa
Wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi wakikagua skimu ya umwagiliaji ya Msolwa iliyoko wilayani Kilombero mkoa wa Morogoro ambayo kupitia Mradi mpya wa " Expanded Rice Production Project" ulioanza kutekelezwa mwaka 2015/16 ni moja ya skimu zilizo kwenye mpango wa kuziboresha ili ziweze kuongeza uzalishaji wa mpunga nchini.
Samaki-Faida inayoweza kupatikana kwenye skimu za umwagiliaji
Hivi karibuni nilitembelea skimu ya umwagiliaji ya kijiji cha Msolwa kilichoko wilaya ya Kilombero mkoa wa Morogoro. Nilishangaa kuwaona watoto hawa wakivua samaki kwenye skimu hiyo. Hii ina maana kuwa kwenye skimu za umwagiliaji, wakulima wanaweza kutenga sehemu na kuwa na mabwawa ya kufuga samaki na kujipatia kitoweo pamoja na mapato kwa kuuza samaki hao.
Saturday, February 27, 2016
Sh2-Mdundo bila umeme
Wote hawa wanafurahi mdundo wa ngoma ya Kiluguru iitwayo shilingi 2. Hii ngoma ilitumbuiza siku ya harusi ya Bw na Bibi Macarios Banzi. Kikundi hiki ni cha watu sita na kila mmoja hupiga,huimba na kucheza. Kwa kawaida hupiga ngoma kwa muda mrefu na hubadilisha midundo mumo kwa mumo. Unacheza upendavyo. Hiyo ndiyo shilingi 2 mdundo bila umeme wala amplifier!
Harusi ya Macarios Banzi- Watu walicheza sana
Harusi ya Macarios- Kila mmoja aliyekuwa ukumbuni alicheza jinsi alivyogusa kuna wale waliogswa na ngoma ya asili ya shilingi 2 kuna sisi vijana wazamani tulioguswa na old is gold na vijana walicheza bongo flava na kwaito. Woo kwa kweli hapakukalika. Hebu check picha ya chini kabisa mimi mambatsa mu moko pamoja na Mr.Mkude tukiyarudi magoma!
Meza moja na marafiki zangu wa Tosamaganga
Picha ya Juu. Tangu mwaka 1978 hadi leo, kutoka Tosamaganga hadi Dar miaka zaidi ya 36 sasa. Banzi, George Mnyitafu (Ngi) na Chris Kalanje (aliyevalia miwani) kushoto kwake Mrs.George. Walisafiri hadi Vikindu kunipa tough na kumpongeza dogo Macarios kwa kufunga ndoa. . Pembeni yao na marafiki wapya maisha mapya Vikindu. Asanteni sana.
Subscribe to:
Posts (Atom)






