Monday, June 6, 2011

Na huu ni mgahawa

Kuna mahali pa kupata chakula na vinywaji baridi na vikali! Hapa ni Mangaka, Nanyumbu.

OFISI YA DC NA DED NACHINGWEA


Moja ya majengo mazuri ya utawala wilayani. Hapa ndipo yalipo makao makuu ya Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Halmashauri ya Nachingwea.

Ng'itu bus la kwanza


Tulikuwa tunajiuliza kuna nini? Bado hatujakutana na mabus kutoka Dar! Mara hilo Ng'itu, bus la kwanza maeneo ya Namwage.

Katibu wa muda


Katika kuandaa taarifa, ilibidi kuinamia Laptop.

Hakuna kulala tunaandaa taarifa


Ukiwa na Dkt. Mkangwa, hakuna kulala. Unamaliza kazi ya field. Usiku lazima timu ikutane kuandaa taarifa.

Joan Kasuga katikati ya daraja la Umoja

Hili ndilo daraja la umoja linalounganisha Msumbiji na Tanzania.

Mlipeni dada twende zetu

Ndivyo anavyosema Mtafiti Tenga akiwahimiza wanatimu kumlipa dadalishe wa pale Mangaka, Nanyumbu.

Saturday, June 4, 2011

Mnima Field Site

Timu ya Kupelemba ilifika Mnima Livestock Field Site kilichoko Newala. Hapa tuliona mbuzi na kupata supu ya mbuzi. Unakumbuka zile picha? Basi ndo hapa! Ofisi nzuri, samani nzuri za mninga kutoka misheni ya Ndanda.

Chumba changu Tandahimba

Kitanda, TV, Fan,na sofa nililipia Tshs 12,000/- kwa usiku mmoja. Cha kufurahisha sana asubuhi kwenye mgahwa wa karibu ni supu ya kuku wa kienyeji.Tandahimba raha tupu siyo adhabu. Ila tulipokuwa safarini usiku kuelekea Tandahimba watu walikuwa wakipiga kelele- CCM hao!

Marafiki

Kushoto ni John Tenga na kulia ni John Banzi wote ni wekundu wa Msimbazi. Ila kwa bahati mbaya tu kwa kuwa walikuwa field imebidi waweke yellow kidogo!

Shabiki wa Liverpool


Starehe, ushabiki na ukokrochi popote. Banzi wa Moro ilimnasa huyu pale Mangaka,Nanyumbu, wakati tulipopata 'Lunch' mara baada ya kutoka kijiji cha Naharawa.

Karanga bomu


Wakulima kupitia utafiti wanafahamu zipi ni karanga bomu. Mimi na wewe hatujui. Picha juu endapo utachagua fungu la karanga kwa kuangalia ukubwa wa karanga, basi utakuwa umeliwa. Ndani hamna kitu. Mimi nilicheza pata potea pale Naharawa na kuchagua karanga bomu!

Striga-Kiduha


Gugu chawi!Ni hatari kwa mazao ya nafaka hasa mahindi na mtama. Gugu hili tumelikuta kwenye moja ya mashamba ya utafiti kijijini Nangaka, wilaya ya Nanyumbu.

Tunatambulishwa kijijini


Unamfahamu huyo mwenye cap?

Masasi-Mtambaswala



Bus hilo linafanya safari zake kutoka mjini Masasi hadi Mtambaswala kupitia Mangaka. Coaster safi.Mtambaswala ni kijiji kilichopo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.

Anapoibiwa mkulima


Ndiyo mihogo imepangwa vizuri kwenye gari. Ni mihogo mizuri. Nenda kamuulize mkulima amepata shilingi ngapi? Hili lori limetoka wilaya ya Rufiji.

GUEST PERHAPS!


Hii ni guest ya Masasi. Inavutia kwa nje lakini in poor management.Hapa ndipo tulipoingizwa mkenge tuliambiwa kuna internet service kwa wateja free of charge. Air conditioners zipo lakini ziko disconnected, matanki ya maji ya mato yapo lakini disconnected. Chai asubuhi saa 2.00. Malazi kwa siku ni kati ya Tshs 30,000- 40,000/=. Basi hii ni Guest Perhaps! Angalia hiyo computer tuliyoingizwa nayo mkenge.

J.Banzi

Chumba changu Mtwara


Bonge la Master bedroom!

Nimepata mchumba Msumbiji


Tuliweza kuwasiliana vizuri tu kwa lugha ya Kiswahili. Mambo, poa. Ah kumbe ni ni Mmakua tu wa Msumbiji wapo mpakani mwa Msumbiji na Tanzania. Kijiji cha kwanza baada ya kuvuka daraja la Umoja.

Friday, June 3, 2011