Wednesday, April 18, 2012

Adha ya Traffic jam-Barabara ya Kilwa


Kwa wale tunaotumia barabara ya Kilwa tumeanza kuonja adha ya 'Traffic jam' hasa nyakati za asubuhi. Kinachosababisha ni barabara mbovu.

Duka la viatu vya Bata


Wazee wetu bado wanaamini kuwa viatu vyenye jina la biashara 'Bata' ni imara. Kampuni ya viatu ya Bata ni ya Kenya. Jijini Dar wana maduka yanayouza bidhaa hizo. Pichani moja ya maduka katika ya jiji la Dar Es Salaam.

Thursday, April 12, 2012

Tukubali Dar chafu


Siku ya jana mvua kubwa ilinyesha jijini Dar. Nilishuhudia mafuriko katika mto Kizinga. Baadhi ya maeneo ya Tandika nyumba zilibomoka.Uchafu ulijitokeza waziwazi kwenye mitaa ya Tandika, Temeke na Mbagala. Mifereji imeziba maji hayatiririki kwenye mitaro iliyojengwa. Kila aina ya uchafu ulisambaa kirahisi kabisa. Mifuko ya plastiki, chupa, matambara, miwa, matunda, matairi chakavu na vingi vingi. Ni uchafu ambao umekuweko kwenye mitaa yetu kwa siku nyingi bila kushughulikiwa. Nina imani kuwa kuna kampuni za usafi zinazolipwa na jiji au Manispaa husika. Hizi zinafanya kazi gani je zinapata malipo bila kazi? Manispaa kwanini zimeshindwa kusimamia usafi? Mbona Moshi wameweza. Hakika ukifika Moshi utadhani ndiyo makao makuu ya Tanzania kwa jinsi maeneo yalivyo safi. Moshi kila mmoja ni askari wa usafi. Tukubali Dar Chafu!

Tuesday, April 3, 2012

Mawasiliano na Banzi wa Moro


Kuanzia sasa unaweza kuwasiliana na Banzi wa Moro kwa kutumia email addresses zifuatazo:- banzi.john@yahoo.com;jlsbanzi@gmail.com

kuna wasomaji wangu wengi walikuwa wakiuliza mbona siwajibu wakinitumia msg kwa email ya jbanzi@hotmail Ndugu zangu hii ilishibiwa na wajanja siku nyingi kwa hiyo nilikuwa siitumii lakini ilikuwa inaonekana kwenye blog yangu ingawa mimi nilikuwa natumia hiyo ya gmail.Leo nimempata mtaalamu wa IT hapa Mananga Centre na kunirekebishia mamboos.Vitu sasa safi kabisaa.Byebye hotmail.Na pole sana aliyeningilia hata kama hajui Kiswahili habari ndiyo hiyo!

Nauli za mabus Tanzania hizi hapa

Bango linaonyesha taarifa ya nauli za mabus kutoka Dar Es Salaam kwenda mikoani.(Nashindwa kufahamu kama Abood Bus ni kawaida,luxury au semi luxury).Jamani, Mkuranga nayo ni mkoani kama ilivyo Kibaha mbona haipo bangoni. (Picha kwa hisani ya Michuzi Blog).

Heshimu lugha ya mwenzako

Hebu soma bango hilo pichani. Bango hili ni moja ya mabango mengi yaliyotundikwa chuoni Mananga, Swaziland.Tafsiri kutoka Kiswati kwenda kiingereza inaeleweka.Je? Bango hilo lingeruhusiwa kutundikwa Tanzania?(Picha kwa hisani ya Leonard Mabuga, masomoni Mananga, Swaziland)

Mambo ya mpakani

Si mpakani mwa Swaziland wala Msumbiji ubadilishaji wa fedha kwa magendo unaendelea waziwazi. Hao wanaoenekana pichani wote wanafanya biashara ya kubadilisha fedha.

Squarters za Maputo

Maputo ni jiji kubwa ukilinganisha na Mbabane, Swaziland lakini unapoanza kuingia jijini Maputo ukitokea Swaziland habari ndiyo hiyo!

Jinsia inazingatiwa chuoni Mananga

Wimbi la kujiendeleza kitaalamu haliangalii jinsi ya mtu. Hapa chuoni Mananga idadi ya wanachuo ukizingatia jinsi ni asilimia 50 wanawake na asilimia 50 wanaume. Wanawake wana nafasi sawa na wanaume na kwa hakika wanawake wanapewa kipaumbele zaidi. Hata waajiri wameshaliona hilo ndiyo maana hali ni kama nilivyoieleza.

Msafiri Kafiri!

Msafiri kafiri.Ndiyo methali tuliyoizoea nyumbani Tanzania. Nikiwa Maputo Msumbiji hivi karibuni nilithibitisha uhalisia wa methali hiyo. Tukitokea Swaziland (nyumbani kwetu) tulijiandaa kwa vitafunnwa na vinywaji. Tulipofika Maputo tulipata kifungua ndani ya gari letu tulilosafiria. Mimi nilipata kipande cha kuku sehemu ambayo huwa siipendi!Tuko ugenini, safarini-Kweli Msafiri Kafiri.

Madafu- Maputo kama Dar!

Madafu bwelele jijini Maputo, Msumbiji. Vijana hao (nje ya uzio) walipotuona walitukimbilia na mkokoteni wao wakitaka kutuuzia madafu lakini kwa kuwa lugha gongana tulishindwa kunywa maji ya dafu ( Wao Wareno sisi Waingereza!).Kwa hiyo hata bei ya dafu jijini Maputo siijui!

Monday, April 2, 2012

Kila mlo - Juice

Kuna Juice za aina nyingi kutoka matunda mbalimbali.Hapa Mananga kila mlo lazima upate juice.Kuna juice ya maembe, mapera,machungwa,passion fruit....Unajua mimi napenda juice gani? (Hiyo yenye rangi nyekundu!)

Inawezekana

Essau Banda (katikati) ni Mhasibu - Benki Kuu Malawi na pia ni Mchungaji(Pastor).Tupo naye Swaziland hapa chuoni Mananga. Juzi tulisafiri naye kwenda Maputo Msumbiji. Kabla ya kuanza safari yetu tuliomba mmoja wetu aombe kwa sala ili Mungu aibariki safari yetu. Banda alijitokeza na kuomba sala fupi na nzuri.Kwenye bus nilikaa karibu naye pembeni yake kulikuwa na kitabu. Nilimuomba kukisoma ndipo nipogundua kuwa Banda ni mchungaji baada ya kusoma ukurasa wa kwanza ulioandikwa Pastor Essau Banda! Ona, Banda hajawahi kujionyesha kuwa ni mchungaji au mlokole. Na pia sikutegemea kuwa na mchungaji akisoma mambo ya dunia hapa Mananga, kumbe yote inawezekana!

Sunday, April 1, 2012

Na hapa ni Lomahasha border post ya Swaziland

Lomahasha kituo cha uhamiaji cha Swaziland.

Mpakani Namaacha-Msumbiji

Jana tarehe 31/03/2012, Mwenyekiti wa 'Africana Group' akiwa mpakani mwa Msumbiji na Swaziland.

Shamba la Miwa la Simunye-Swaziland


Shamba la miwa la Simunye nchini Swaziland

Bus linapovuta trailer la mizigo

Lori kufungwa trailer ni kitu cha kawaida nchini Tanzania lakini kwa bus hasa la abiria sijaona. Jana tarehe 31/3/2012 akiwa ziarani jijini Maputo nchini Msumbiji,Banzi wa Moro alishuhudia bus hili likivuta trailer lenye mizigo ya abiria.Usalama wa mizigo ya abiria!(sina jibu)

Ushuru wa barabara-Maputo

Unapoingia au kutoka Msumbiji kwa gari ni lazima ulipie ushuru.Pichani gari yetu ikisubiri kulipia ushuru jana tarehe 31/3/2012

Siyo photoshop

Leonard ndani ya Maputo akitokea Swaziland.Utamtaka!

Sina la kuwadanganya April 1

Banzi wa Moro Kando ya mti wa Yanga,Simunye-Swaziland!