Thursday, June 14, 2012
Jeneza la Dr. P.Mluge langoni mwa Kanisa
Tumempoteza Dr. Gregory Paul Constanci Mluge
Tuesday, June 5, 2012
Wamepokea Sakramenti ya NDOA
Takribani ni mwaka mmoja sasa tangu Bw na Bi Cleophas wapokee Sakaramenti ya Ndoa Parokiani Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Vijana wengi wanaogopa kufunga ndoa kwa kutaka makuu. Nilishuhudia ndoa hii isiyokuwa na makeke wala vitimbi. Tulikula, tulikunywa na kucheza.Wanandoa wanaendelea na maisha yao bila mfarakano. Hongereni sana.
Kituo cha Mabasi Kivukoni-DAR
Majani ya Kaskasi
Kwenye maonesho ya NaneNane (Siku ya Wakulima)mwaka jana (2011) wakulima wa kutoka Kibungo JUU wilaya ya Morogoro Vijijini kwenye banda lao walionyesha matumizi bora ya ardhi.Moja ya teknolojia waliyoionyesha inayotumika kuhifadhi ardhi ni upandaji wa mmea unaoitwa kaskasi au kwa lugha ya Kiluguru 'usoti' (pichani) kuzuia mmomonyoko wa ardhi milimani. Licha ya kuhifadhi ardhi, kaskasi hutumika kuezeka nyumba.
Mambo ya Teknolojia
Monday, June 4, 2012
Traffic Police mmemuona huyu?
Ni hatari kwa watoto hawa
Hii inahatarisha maisha.Wanafunzi wengi na vijana hupenda kudandia magari ili wapate kitu kinachoitwa 'lift' lakini gharama yake mara nyingi ni kuhatarisha maisha. Angalia picha hizi ambazo zimenyakwa na Banzi wa Moro kuanzia kituo cha Kongowe hadi Mbagala Rangi 3 jijini DAR ES SALAAM
Ndani ya lori
wanajiandaa kushuka chini

Wanapanda
Matokeo ya kutomuaga mkeo
Friday, June 1, 2012
Wanamwita 'Mwabeshi'
Huyu anaitwa Shabani. Lakini hapa kijijini kwetu Kisemvule ni maarufu sana kwa jina la 'Mwabeshi' likiwa na maana ni mtu kutoka Ethiopia! Kwa maelezo yake mwenyewe ni kwamba, jina hilo amelipata hapo Kisemvule kwa kuwa alikuwa anafanya kazi kwa mtu aliyefananishwa na waethiopia lakini kumbe alikuwa ni mchangayiko wa damu ya kihindi na watu kutoka Tabora. Shabani kazi yake ni biashara ndogondogo hasa matunda kwa kuzingatia msimu kuna wakati anauza embe, kuna wakati mwingine machungwa. Hapa alikuwa anauza mahindi ya kuchoma. Huyo ndiye Shabani 'Mwabeshi' ameoa na ana watoto watatu
Nyumba hadi nyumba
Ndivyo inavyofanya kazi Jumuiya Ndogondogo za Kikristu. Hapa ni nyumbani kwa Mzee Mgaya wa Soweto-Vikindu. Jumuiya Ndogondogo zinaimarisha upendo, kutambuana na pia hutumika kulieneza Neno la Mungu.Jumuiya Ndogondogo ikitumiwa vizuri huleta maendeleo.
Alama za kiwanja
Unaponunua viwanja vizsivyopimwa ni vizuri kuweka alama za kudumu na zinazoeleweka ili kuepusha mgangano wa mipaka ya viwanja hapo baadaye
Na hii ndiyo misemo ya Waluguru
1. 'Bita ako si miyage' - Si vizuri kuacha mtu akafanya kitu kivyake vyake
2. 'Chikwili ng'awingagwa na Seko'- Huwezi kumfukuza mnyama anayeitwa 'Chikwili' huku ukiwa unacheka
3. 'Chimbulumbulu kokwila mti gwagumanyile'- Mnyama anayeitwa Chimbulumbulu hupanda mti anaoufahamu.
Tafakari kuhusu semi hizi za Kiluguru!
Miundo Mbinu ya Umwagiliaji
Kuendesha kilimo cha umwagiliaji inahitaji miundo mbinu ya uhakika
Banio la Umwagiliaji liloloko mto wa Ruaha- Ruaha Mbuyuni, Kilolo.
Banio la umwagiliaji maji kijiji cha ItimbaMfereji wa umwagiliaji unaotunzwa vizuriBaada ya kuvuna mahindi, shamba limepandwa maharage (Kijijini Itimba, Utengule-Mbeya vijijini). Hii inawezekana kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Hapa ni Umalila-Mbeya
Isangati Agricultural Development Organization (IADO) kijijini Santilya, Umalila, Mbeya Vijijini. AIDO ni Shirika lisilo la Kiserikali (NGO) linalofanya kazi katika wilaya ya Mbeya Vijijini. AIDO wamewezeshwa na ASDP kupitia DADPs katika kuleta mageuzi ya kilimo wilayani Mbeya. Baadhi ya Miradi ya Kilimo inayosimamiwa na IADO ni:- Upandaji wa Miche Bora ya Kahawa, Ufugaji wa Ng'ombe wa Maziwa, Ufugaji bora wa Nguruwe, Uboreshaji wa Kuku wa Asili, Ufugaji wa samaki. Aidha IADO hutoa mafunzo ya Utawala Bora yanayowawezesha wanavijiji kufuatilia matumizi ya fedha za umma ngazi ya kijiji.Uboreshaji wa kuku wa asili
Nje ya Ofisi ya IADO
Tunapata taarifa ya IADO kutoka kwa uongozi wa shirika.Ukaguzi wa banda la machinjio kijijini Santilya, Mbeya vijijini.
Subscribe to:
Posts (Atom)

