Friday, November 8, 2013

Huyu ndiye Betty Missokia wa Haki-Elimu

Bi.Elizabeth Missokia (Kulia) CEO wa Haki -Elimu akiongea na waandashi wa habari hivi karibuni (picha kwa hisani ya gazati la mwananchi).

Hakika 100% Moro

Morogoro mji kasoro bahari! Maarufu kwa soka, muziki,kilimo na utalii!

Thursday, November 7, 2013

Mtambo mpya bandarini Dar Es Salaam

Mtambo mpya wa kupakua na kupakia mizigo umetua bandarini Dar.  (Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi)

Mwanamama mchoma mihogo Arusha

Mwanamama  Victoria Emmanuel akiwa amembeba mwanae akichoma mihogo na ndizi jijini Arusha.
Hakuna shughuli ya mwanaume tu kila mtu anaweza kufanya shughuli yoyote ukiwa na nia. Tukijishughulisha riziki inapatikana!

Wadada wamekabidhiwa bendera

Wachezaji wa timu ya Taifa ya wanawake U-20 (The Tanzanite) wamekabidhiwa bendera na kuondoka jana kuelekea nchini Msumbiji. Tunawatakia ushindi 9picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi)

Kilimanjaro beer mali ya Tanzania

Fikiria kijua cha saa sita. Halafu unapewa kituliza kiu cha Kilmanjaro beer iliyo baridi. Sijui utajisikiaje! Hii ni mali ya Tanzania. Beer safi - Premium Lager - sasa imetoa chupa mpya ya ml 375 kwa bei ya Tshs 1600. Hongera Tanzania Breweries. Banzi wa Moro ndo kinywaji chake. Angalau vibia  2 kwa siku!

Korosho utazipenda tu!

Kama hujawahi kutafuna korosho basi picha hii ni kishawishi tosha za kuanza kula korosho halafu utaniambia. Mikoa yote ya pwani nchini Tanzania inazalisha korosho lakini mikoa ya kusini (Mtwara na Lindi ) ni maarufu zaidi. Na huku ndiko kiliko kituo cha Utafiti Naliendele  ambako wako watafiti waliobobea na utafiti wa korosho. Sasa wamekuwa gumzo  barani gumzo jinsi wanavyolipandisha chati zao la korosho.

Korosho kutoka kituo cha Utafiti Naliendele


Korosho safi tamu zinavutia kutoka kituo cha Utafiti Naliendele, Mtwara.Watafiti wa zao la korosho walipo kwenye kituo cha Utafiti  Naliendele mkoani Mtwara  wamefika mbali zaidi, si tu wanatafiti mbegu bora, kinga ya magonjwa na wadudu, rutuba ya udongo. Sasa wamefikia mlaji hiyo ndiyo moja ya bidhaa zao kutoka korosho wanazotafiti. Hii ni mali ya Watanzania. Watanzania tuchangamkie kilimo cha korosho fedha iingie mifukoni mwetu.

Tuesday, November 5, 2013

Ha mboga ya maboga

Mboga ya maboga imeshachumwa kutoka shambani. Iko kwenye maandalizi ya kupikwa katika kibanda cha mamalishe kijijini  Mvumi, Kilosa, Morogoro.

Satelitte Dish kijijini Mvumi

    Mambo mazuri  vijijini. Ukizungumzia  Messi wote wameshamuona kupitia Luninga. Haya ndiyo maendeleo kwa mazingira haya walimu, mabwanashamba, waganga, wahandisi na wataalamu wengine watapenda kuishi vijijini.

NGO ya kuhamasisha usafi

    Vijijini  kuna Asasi zisizo za Kiserikali nyingi (NGO) kama hiyo inayohamsisha watu kunawa mikono       sabuni kabla ya kula

Kibanda cha kujiremba- Mvumi

Hiki ni kibanda cha kutengeneza nywele kwa akina baba kijijini Mvumi, Kilosa, Morogoro

Nyumba bora mazingira safi kijijini Mvumi

    Nyumba bora mazingira safi na ya kupendeza kijijini Mvumi,Kilosa-Morogoro

Huduma ya mawasiliano inapatikana Mvumi

Kijijini Mvumi, Kilosa, Morogo-huduma ya mawasiliano kwa mitandao ya Vodacom na Tigo  inapatikana.Pia unaweza kutoa  na kutuma pesa kama inavyoonekana pichani. Maendeleo vijijini!

Vifaa vya mamalishe wa Mvumi

Hivi ndivyo vifaa vya mamalishe  wa Mvumi. Kuna mchele, mafuta, ndoo za maji, jiko la mkaa na simu ya mawasiliano sakafuni!

Duka la nyama (Butcher) kijijini Mvumi

Maisha mazuri popote. Hata kijijini Mvumi, wilayani Kilosa kuna duka la nyama zuri.

Ndani ya Bus safarini Mvumi kwa mazishi

Tukiwa na mwili wa marehemu Lawrence Mbunda  safarini kwa mazishi kuelekea Mvumi, Kilosa Morogoro kwa mazishi.

Diwani John Waziri na matango

Diwani John Waziri wa Halmashauri ya mjini wa Morogoro akichagua matango kijijini Mvumi, Kilosa, Morogoro alipokwenda kwa mazishi ya marehemu Lawrence Mbunda, tarehe 3/11/2013

Kibanda cha mamalishe Mvumi

Kibanda cha mamalishe kinachoendelea kujengwa kijijini Mvumi, Kilosa, Morogoro.

Mapumziko ndani ya kibanda cha mamalishe

Dada zangu waliokwenda msibani Mvumi walijipumzisha ndani ya kibanda cha Mamalishe.