Friday, November 8, 2013
Huyu ndiye Betty Missokia wa Haki-Elimu
Bi.Elizabeth Missokia (Kulia) CEO wa Haki -Elimu akiongea na waandashi wa habari hivi karibuni (picha kwa hisani ya gazati la mwananchi).
Thursday, November 7, 2013
Mtambo mpya bandarini Dar Es Salaam
Mtambo mpya wa kupakua na kupakia mizigo umetua bandarini Dar. (Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi)
Mwanamama mchoma mihogo Arusha
Mwanamama Victoria Emmanuel akiwa amembeba mwanae akichoma mihogo na ndizi jijini Arusha.
Hakuna shughuli ya mwanaume tu kila mtu anaweza kufanya shughuli yoyote ukiwa na nia. Tukijishughulisha riziki inapatikana!
Hakuna shughuli ya mwanaume tu kila mtu anaweza kufanya shughuli yoyote ukiwa na nia. Tukijishughulisha riziki inapatikana!
Wadada wamekabidhiwa bendera
Wachezaji wa timu ya Taifa ya wanawake U-20 (The Tanzanite) wamekabidhiwa bendera na kuondoka jana kuelekea nchini Msumbiji. Tunawatakia ushindi 9picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi)
Kilimanjaro beer mali ya Tanzania
Fikiria kijua cha saa sita. Halafu unapewa kituliza kiu cha Kilmanjaro beer iliyo baridi. Sijui utajisikiaje! Hii ni mali ya Tanzania. Beer safi - Premium Lager - sasa imetoa chupa mpya ya ml 375 kwa bei ya Tshs 1600. Hongera Tanzania Breweries. Banzi wa Moro ndo kinywaji chake. Angalau vibia 2 kwa siku!
Korosho utazipenda tu!
Kama hujawahi kutafuna korosho basi picha hii ni kishawishi tosha za kuanza kula korosho halafu utaniambia. Mikoa yote ya pwani nchini Tanzania inazalisha korosho lakini mikoa ya kusini (Mtwara na Lindi ) ni maarufu zaidi. Na huku ndiko kiliko kituo cha Utafiti Naliendele ambako wako watafiti waliobobea na utafiti wa korosho. Sasa wamekuwa gumzo barani gumzo jinsi wanavyolipandisha chati zao la korosho.
Korosho kutoka kituo cha Utafiti Naliendele
Korosho safi tamu zinavutia kutoka kituo cha Utafiti Naliendele, Mtwara.Watafiti wa zao la korosho walipo kwenye kituo cha Utafiti Naliendele mkoani Mtwara wamefika mbali zaidi, si tu wanatafiti mbegu bora, kinga ya magonjwa na wadudu, rutuba ya udongo. Sasa wamefikia mlaji hiyo ndiyo moja ya bidhaa zao kutoka korosho wanazotafiti. Hii ni mali ya Watanzania. Watanzania tuchangamkie kilimo cha korosho fedha iingie mifukoni mwetu.
Tuesday, November 5, 2013
Ha mboga ya maboga
Mboga ya maboga imeshachumwa kutoka shambani. Iko kwenye maandalizi ya kupikwa katika kibanda cha mamalishe kijijini Mvumi, Kilosa, Morogoro.
Satelitte Dish kijijini Mvumi
Mambo mazuri vijijini. Ukizungumzia Messi wote wameshamuona kupitia Luninga. Haya ndiyo maendeleo kwa mazingira haya walimu, mabwanashamba, waganga, wahandisi na wataalamu wengine watapenda kuishi vijijini.
NGO ya kuhamasisha usafi
Vijijini kuna Asasi zisizo za Kiserikali nyingi (NGO) kama hiyo inayohamsisha watu kunawa mikono sabuni kabla ya kula
Huduma ya mawasiliano inapatikana Mvumi
Kijijini Mvumi, Kilosa, Morogo-huduma ya mawasiliano kwa mitandao ya Vodacom na Tigo inapatikana.Pia unaweza kutoa na kutuma pesa kama inavyoonekana pichani. Maendeleo vijijini!
Vifaa vya mamalishe wa Mvumi
Hivi ndivyo vifaa vya mamalishe wa Mvumi. Kuna mchele, mafuta, ndoo za maji, jiko la mkaa na simu ya mawasiliano sakafuni!
Ndani ya Bus safarini Mvumi kwa mazishi
Tukiwa na mwili wa marehemu Lawrence Mbunda safarini kwa mazishi kuelekea Mvumi, Kilosa Morogoro kwa mazishi.
Diwani John Waziri na matango
Diwani John Waziri wa Halmashauri ya mjini wa Morogoro akichagua matango kijijini Mvumi, Kilosa, Morogoro alipokwenda kwa mazishi ya marehemu Lawrence Mbunda, tarehe 3/11/2013
Subscribe to:
Posts (Atom)






