Friday, January 25, 2008

AMEUNGUZWA NA KURUKIA DALADALA

Siku ya Jumanne wiki hii, pale Mbagala Rangi 3 lilitokea tukio la ajabu.

Kuna kibaka alibambwa, akapigwa na kuchomwa moto.Lakini kwa maajabu ya mwenyezi Mungu, moto ulipozimika aliweza kunyanyuka na kutembea.

Asubuhi hiyo ya Jumanne nilimshuhudia mtuhumiwa huyo akitembea kama sanamu vile! Huku wananchi wakimzonga na kumzomea. Ee bwana eeh, alikuwa kama mzuka vile, maana ngozi ilianza kubanduka na kuonyesha ile rangi ya ndani nyeupee! Huwezi kutazama mara mbili nakwambia. Damu ilikuwa inamtirirka kichwani hadi mdomoni, nakwambia hata kama alikuwa ndugu yako usingeweza kumtambua. Nguo zilionekana ni matambaratambara na amevikwa upati kuhifadhi sehemu nyeti. Alhamdulilah!. Lakini cha kushangaza, kipande cha baba kile kwa ghafla na bila kutarajia aliweza kudandia daladala ya Ubungo huku akituacha hoi .

Habari nilizozipata baadaye ni kwamba kibaka huyo alimalizwa na wananchi wenye hasira hadi kufa!

Vibaka acheni ukwapukwapu mtapoteza maisha hivi hivi. Wananchi wema wamechoka na vitendo vyenu. Nguvu mnazo zitumieni kwa kufanya kazi halali.

No comments: