Tuesday, August 26, 2014

Ajali na riziki hapohapo

Lori hili la mafuta lilianguka Kimara hivi karibuni. Kwa kuwa llilikuwa limebeba mafuta ya kula, wananchi walihangaika kusomba mafuta hayo. Angalia umati unavyoshughulika, kila mmoja kwa nafasi na uwezo wake. Najiuliza, wateja wa mafuta haya ni akina nani? Kwa  vyovyote vile ni mama ntilie na familia za kipato cha chini. Hata hivyo kuna wengine huenda waliweka katika vifungashio vipya na kuuza madukani.Kwa hiyo inawezekana kabisa wengi wetu tumepata kutumia mafuta haya bila kufahamu. Kweli ajili na riziki hapohapo!

No comments: