Sunday, December 13, 2009

Kipi kinachoitangaza Tanzania?

Elimu ya msingi, wanafunzi 50% hawakufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu. Jiji la Dar Es Salaam ni chafu. Uzalishaji katika kilimo bado ni wa chini. Miundo mbinu ni ya ubabaishaji. Umeme si wa uhakika. Maji ni kwa mgao. Michezo- Mpira wa mguu timu ya Taifa haijafanikiwa kupata ushindi na kutwaa kikombe kwa muda mrefu. Madini ndo tunaambulia athari za kuharibika kwa mazingira pamojan na wananchi kupata vilema badala ya kuwa matajari. Hivi Tanzania ukiondoa amani na usalama tuna lipi la kujivunia. Hata usafi tu ni issue! Mwe!

Kuwasimamisha MAJEMBE ni kupunguza kasi ya mabadiliko

Kwa kawaida binadamu hapendi mabadiliko. Hasa mabadiliko HASI. Hivi karibuni uongozi wa JIJI la Dar Es Salaam waliamua kuwatumia MAJEMBE Auction Mart kudhibiti hali mbaya ya usafiri hapa jijini wakisaidina na Traffic Police. Zoezi hilo halikudumu kwa muda mrefu baada ya wamiliki wa mabus kutishia kugoma (hasa kwa njia ya TABATA waligoma). Hatimaye kuufanya uongozi wa mkoa wa Dar Es Salaam kusitisha zoezi hilo. Jamani tusiogope mabadiliko tuyafanyie kazi na tutazoea tu. Kwa kawaida binadamu hapendelei mabadiliko HASI.

HONGERA JKT

Kama kuna jeshi lililoonyesha ukakamavu wa hali ya juu na kushangiliwa na maelfu ya wananchi waliokuwepo uwanja wa UHURU tarehe 9 Desemba wakati wa kusherehekea miaka 48 ya UHURU ni JKT. Walipendeza kwa sare, ukakamavu na kuwajibika pamoja na kufurahisha. HONGERA SANA JKT

Mawaziri kupanda waingia uwanjani kwa mabus miaka 48 ya UHURU

Nilikuwepo uwanja wa UHURU kwenye sherehe za miaka 48 ya Uhuru. Kwanza nikiri kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuhudhuria sherehe za uhuru katika uwanja wa UHURU. Pamoja na viburudisho vya ngoma za kitamaduni kutoka hapa nyumbani na nchini Uganda (Kikundi cha NDERE) na gwaride la vikosi vya majeshi ya polisi,jwtz, magereza,jkt + Halaiki ya wanafunzi. Kipya ni Mawaziri, Mabalozi, Wakurugenzi kuingia uwanjani na mabus ya kukodi. Naambiwa magari yao waliyaacha KARIMJEE! Hivi hili waandishi hawakuliona?

Tuesday, November 24, 2009

Maalim Seif na Karume kukubaliana kuachana na uhasama ni uamuzi wa kihistoria

Jambo la msingi katika maisha ni kuondoa tofauti inayoleta misuguano katika jamii inayosababisha kudumaa kwa maendeleo. Msuguano uliokuwepo kati ya vyama vikuu vya siasa visiwani Zanzibar (CCM na CUF) umeleta athari kubwa katika jamii. Baya zaidi watu wamepoteza uhai kwa msuguano huu tena raia wa kawaida kabisa huku wakiwaacha viongozi wakuu wa vyama wakidunda!

Kitendo cha viongozi wa vyama hivyo huko Zanzibar kukubaliana kuachana na uhasama na kuijenga Zanzibar ni kitendo cha AFYA. Nawapongeza sana.

Falsafa ya 'Zee la Nyeti'

Kama anaandika lugha ya kihuni, kama vile mtoto wa mijini. Lakini ndivyo mwandishi Henry Mdimu (Zee la Nyeti) anavyofikisha ujumbe wake kwa jamii kupitia gazeti la Mwananchi kila Jumamosi katika kurasa za starehe.

Blog hii imevutiwa sana na makala hizo na leo imebidi kuwafahamisha wasomaji wake ni vizuri ukalipata gazeti la Mwananchi la kila Jumamosi uweze kusoma falsafa ya Zee la Nyeti. Makala za Mdimu zina ujumbe mzito hasa kwa vijana. Lugha anayoitumia kufikisha ujumbe ni ile wanayoitumia vijana kwa hiyo haichoshi. Kwa mfano Jumamosi iliyopita kulikwa na kichwa cha habari kinachosmea 'Ngoma haipigwi kwa nyundo'.....hivi watu mkisikia mdundo wa ngoma mnafikiri ngoma huwa inapigwa kwa nyundo? Vijifimbo viwili tu, au samtaimz mkono wako tu...

Tarehe 31/10/2009. Mdimu alishuka na makala inayosema 'Ukiona manyoya...ujue keshaliwa' simulizi iliendelea hivi.....alipoingia tu anakutana na viata vya jmaa, saa iko mezani na kama nguo anazozijua hivi?.....ukiona unyayo si unajua kabisa kama kuna mtu kapita? .......Maana afadhali uone unyayo kuna siku utakuta manyoya, na itabidi ukubali...kwamba kuku keshaliwa.

Big Up Henry Blog hii imezikubali makala zako.

Tuesday, November 3, 2009

Vijana wanapaswa kutekeleza kauli mbiu ya KILIMO KWANZA


Ukitembelea katika vijiji vingi hapa nchini hutoshangaa kukuta washiriki wakuu wa kilimo ni wazee. Vijana walio wengi hawajihusishi kabisa na kilimo. Ukiwauliza wanazo sababu nyingi za kutojihusisha na kilimo zilizo nyingi si za msingi. Wakati Taifa linajipanga katika kuitikia kauli mbiu ya KILIMO KWANZA vyema vijana wakaandaliwa ili waifahamu vizuri kauli mbiu hiyo kwa kuwa tayari kwa utekelezaji wake. Kwa hiyo mafunzo mafupi ya uzalishaji wa kilimo yakiandaliwa kwa vijana wetu yatasaidia sana kuboresha uzalishaji wa kilimo. Kilimo kikiachiwa wazee kitakufa.

Tunapoteza shilingi milioni 28 za wakulima kama mchezo


Nimesikitishwa kusoma habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Mtanzania la tarehe 2/11/2009 kuwa kiwanda cha sukari cha Ilovo kilichopo Kilombero kimetelekeza miwa ya wanachama 27 wa Chama cha Wakulima wa Miwa katika bonde la Kiliombero yenye thamanin ya shilingi ya Tanzania milioni 28. Habari hii imenistua kwa kweli, kwa umaskini walionao wakulima wetu kupoteza kiasi hicho cha fedha si jambo dogo hata kidogo. Si fahamu ni sababu zipi zilizopelekea uongozi wa kiwanda hicho kukataa miwa hiyo.

Usichelewe kusajili sim card yako


Makampuni ya simu yanayotoa huduma hapa nchini yanaendelea na zoezi la kusajili simu card kwa wateja wake. Blog hii imeshasajili simu card zake za Zain na Vodacom siku ya Jumapili. Zain hawana mlolongo mrefu wa mambo katika kusajili.Tatizo liko kwa Tigo inabidi usote katika foleni. Vipi Tigo ndo tuseme mnawateja wengi? Mimi siamini hata kidogo, hebu boresheni huduma zenu. Banzi wa Moro bado hajasajili simu card yake ya Tigo.

JK amepania kuinua utafiti nchini


Gazeti la Habari leo la tarehe 2 Novemba 2009 limeandika kuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kutoa Tzs milioni 40 kwa ajili ya utafiti wa tufaa (apples) katika kituo cha Utafiti Uyole, Mbeya.

Ni hivi karibuni nimekuwa nikijiuliza kuwa kwanini biashara ya tufaa inaongezeka katika miji yetu wakati sioni wakulima wanaozalisha matunda haya hapa nchini. Jibu ni kwamba tofaa huagizwa kutoka Afrika ya Kusini.

Tanzania zipo sehemu ambazo tofaa zinaweza kuzalishwa kutokana na hali ya hewa ya maeneo hayo sehemu kama vile Lushoto (Tanga), Mgeta (Morogoro) na Mbeya. Iwapo utafiti wa kina utafanyika na kuweza kupata mbegu zinazoweza kustawishwa katika sehemu hizo kutakuwa hakuna sababu tena ya kuagiza tufaa kutoka nje ya nchi, kwahiyo auamuzi wa Mhe. Rais kutoa fedha hizo za utafiti ni chanzo cha kuanza kuzalisha tufaa bora hapa nchini.

HONGERA SIMBA SPORTS CLUB


Mimi ni shabiki wa Club ya Simba au Wekundu wa Msimbazi. Nawapa hongera nyingi wachezaji, coach na viongozi wa klabu kwa ushirikiano mliouonyesha hadi kufanikiwa kuwashinda wapinzani wetu wa jadi Dar Young Africans kwa goli 1-0 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam. Mgosi nakupa shavu mdogo wangu!

Saturday, October 24, 2009

Hawakujiandikisha kwasababu mambo ni yaleyale


Uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mtaa na vijiji unatarajiwa kufanyika kesho. Wananchi wengi inasemekana kuwa hawakujiandikisha. Ni kweli, Banzi wa Moro katika pitapita yake mjini na vijijini amegundua kuwa watu wamekata tamaa na uongozi wa vijiji na mitaa kwani kasi ya maendeleo hasa huko vijijini ni kidogo sana. Mambo ni yale yale. Viongozi wanaomba nafasi hizo kwa manufaa yao binafsi na wala si ya wananchi. Utasikia ah nikipata nafasi hii baada ya muda wangu wa uongozi kumalizika lazima ninunue 'daladala.'Hivi ndiyo lengo kweli la kugombania uongozi ? Wakati wa kampeni nimeshuhudia vibweka vingi kwa vyama vyote wakishindana kwa rusha roho! Hivi kweli kuna lolote hapa? Ndo maana wengi hawajajiandikisha! (Picha kwa hisani ya gazeti la mwananchi tarehe 24 Oktoba 2009)

Tuesday, October 13, 2009

Mchicha upo wanunuzi je?


Vijana hawa wameamua kuuza mazao ya kilimo hasa mbogamboga. Lakini, wanunuzi wako wapi? Ona mchicha umeanza kunyauka!

Mbuzi wanauzwa


Kama utatembelea 'Kiembe Mbuzi'- Vingunguti na kukuta mbuzi wa aina hii wanauzwa sidhani kama utasita kununua na sifikirii kwamba utampata kwa bei poa. Je, mbuzi wa aina hii wanaweza kupatikana hapa nchini? Fika katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo ya Taifa - Mpwapwa utapata jibu na utaanza kufuga na kuuza mbuzi.

Mtafiti wa Kilimo inaijua Bodi ya Utendaji ya FARA na sekretariati yake?


Kama umeshafika Accra Ghana na kama wewe ni mtafiti wa kilimo lazima utakuwa umefika kwenye makao makuu ya FARA (Forum for Agricultural Research in Africa)- Ni mkono wa kiufundi wa AU katika masuala ya uendelezaji Kilimo na Uchumi wa vijijini katika Bara la Afrika. Pichani ni Bodi ya Utendaji na Sekretariati ya FARA.

Hana uhakika wa soko


Mwangalie msichana huyu anatembeza mboga kwa wateja. Tatizo ni moja je atauza? Upatikanaji wa soko la uhakika kwa mazao ya kilimo ni tatizo linalorudisha nyuma maendeleo ya kilimo barani Afrika na kusababisha wakulima wasipokee kwa urahisi teknolojia bora za uzalishaji.

Vichwa vya Kilimo Afrika


Afrika hatujapiga hatua kubwa katika kilimo. Uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara bado ni mdogo sana. Mazao yatokanayo na mifugo nayo ni haba na duni. Matokeo yake njaa inapiga hodi kwenye bara hili. Hata viwanda vinavyohitaji mali ghafi kutokana na kilimo havitoshelezwi. Hata hivyo kuna vichwa vinavyokuna ubongo kuhakikisha kuwa Afrika inapata teknolojia bora zitakazosaidia kuinua uzalishaji katika kilimo. Angalia vichwa hivyo katika picha.

Mafuta kwenye mahindi tumekwisha!


Wakati wananchi wetu wanahangaika kupata mlo. Wenzetu wako 'busy' kupata mafuta yakuendeshea mitambo kutoka mimea kama vile mahindi. Hii maana yake nini hasa? Chakula kwao kinatosheleza ila wana wasiwasi wa nishati! Upuuzi mtupu. Hivi kweli unaweza kuendesha gari kama una njaa? Watanzania lazima tuangalie suala la nishati na chakula kwa uangalifu mkubwa na kutoa kipaumbele kinachostahili tuwe makini na sera ztu vinginevyo tumekwisha.

Saturday, October 10, 2009

Raphael Benitez wa Liverpool


Mmoja wa makocha wanaojiamini katika Ligi Kuu ya Uingereza ni Raphael Benitez wa Liverpool. Hebu angalia mbwembwe za Benitez pichani. Lakini Banzi wa Moro anaipenda sana timu ya Liverpool kwa sababu gani? Wachezaji wake wanajituma sana hasa Stephen Gerald - The Captain. Lakini zaidi ya hilo nyuzi zao kama wekundu wa Msimbazi!

Hakika Makamu wa Rais ni mfano wa kuigwa


Hivi karibuni nimekuwa nikifuatilia habari za Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Ali Mohamed Shein kwa karibu sana. Katika safari zake karibu zote iwe za kikazi au binafsi ndani na nje ya nchi yeye huambatana na mkewe Mama Mwanamwema Shein. Tarehe 8/10/2009 alifika katika kituo cha Shule ya Msingi Oysterbay, Dar Es Salaam kwa kusudi la kujiandikisha katika Daftari la wapiga kura, hebu check kushoto kwake ameambatana na nani? (Pichani kwa hisani ya gazeti la Majira).