|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| Hebu angalia takwimu za ufaulu kwa baadhi ya shule za msingi maarufu Morogoro vijijini-Hali ni tete. Tukae na tuone jinsi ya kujikwamua kutoka kwenye hali hii. Mwaka wa jana pia hali ilikuwa si nzuri. Hata wanafunzi wanaofanya mtihani kwa darasa la saba ni wachache ukilinganisha na shule nyingine. Basi kwa uchache huo nilitegemea kuwa watoto wangefanya vizuri. Wanaweza wasifanye vizuri kwenye somo la kiingereza lakini hesabu Je? | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Friday, November 7, 2014
Ufaulu darasa la saba 2014 - Morogoro Vijijini hali ni tete
Queen wa Mzinga Shule ya Msingi apasua A tupu!
Mwanafunzi Queen Damian Mpangwa wa darasa la saba kutoka shule ya msingi Mzinga-Temeke Vijijini, Mkoa wa Dar Es Salaam anatisha! Amepasua vibaya kwenye matokeo ya darasa la saba 2014. Hebu angalia matokeo yake.
Kiswahili - A
English- A
Maarifa - A
Hisabati- A
Science - A
Wastani - A
Hii ni shule ya kawaida ya umma. Nimeambiwa na mwalimu wa shule hiyo kuwa mwanafunzi huyu anatoka familia ya kipato cha chini na anaishi na mama yake. HONGERA sana Queen umezipaisha shule za umma.
Kiswahili - A
English- A
Maarifa - A
Hisabati- A
Science - A
Wastani - A
Hii ni shule ya kawaida ya umma. Nimeambiwa na mwalimu wa shule hiyo kuwa mwanafunzi huyu anatoka familia ya kipato cha chini na anaishi na mama yake. HONGERA sana Queen umezipaisha shule za umma.
Tusiime yaongoza tena STD VII-DAR 2014
![]() |
| Tusiime students (picha ya maktaba - mtandao) |
Wanafunzi waliofanya mtihani 168
1st Wilaya ya Ilala- shule 101
1st Mkoa wa Dar Es Salaam- 506
8 Kitaifa- 1586
Kweli TUSIIME ni shidaaaaa!
KELVIN K.SIMKOKO-KICHWA CHA MARIAN BOYS SEC
Kelvin K.Simkoko ametunukiwa tuzo ya kufanya vizuri katika taaluma Kidato cha 4 2014 shule ya Marian Boys' Secondary. Hongera Kelvin ongoza hadi utakapopata PhD lakini pia usimsahau MUNGU aliyekuumba na kukupa kipaji hicho si kweli kuwa wengine hawataki kuwa vichwa MUNGU ndiye hupanga haya na kwa bidii yako pia.
Wednesday, November 5, 2014
Mahindi kutoka kwa watafiti wa Selian
Ni kweli zipo aina bora ya mbegu za mahindi zenye uwezo wa kuzaa mahindi mengi na bora. Kituo cha utafiti wa Kilimo Selian kilichopo Arusha kwa muda mrefu kimekuwa kikitafiti aina bora za mbegu za mahindi zinazofaa mazingira ya wakulima wa Kanda ya Kaskazini hapa nchini moja ya mbegu zilizokwisha pendekezwa ni Selian H208 na Situka. Kwa maelezo zaidi wasiliana na kituo cha Utafiti Selian( Contact. Dr. Mafuru (ZD) -0756657316)
Hizi ndizo aina bora za mbegu za mbaazi
Wakulima wengi wa zao la mbaazi hapa nchini hupanda mbazi kwa kutumia mbegu walizonazo. Wnapanda kwa mazoea. Hata ukuwauliza aina ya mbegu hizo pamoja na sifa zake hawajui. Mara nyingi mbegu hizo ni mchanganyiko. Hali hii husababisha uzalishaji duni wa zao la mbaazi. Kituo cha utafiti wa Kilimo Selian kilichopo mkoani Arusha Kanda ya Kaskazini kimefanya utafiti wa muda mrefu wa kilimo cha mbaazi si kwa mbegu tu bali mazingira yanayotakiwa ya kustawisha mbaazi (udongo na hali ya hewa) pamoja na kufanya utafiti wa kichumi kuhusu kilimo cha mbaazi.
Nkem Owoh-Msanii machachari wa Afrika
Kwa wenye mazoea ya kuangalia sinema za Kinegeria, sura hii si ngeni kwenu. Huyu ni Nkem Owoh a.k.a asokofia. Huyu ni mcheza sinema mashuhuri kutoka Nigeria. Amecheza sinema nyingi na kutunikiwa zawadi nyingi nyingi nyingi. Cha kushangaza Nkem kwa taaluma ni Mhandisi. Lakini umaarufu wake haukutokana na uhandisi bali ni kwa sanaa. Mimi na wewe pengine tunafanya kazi ambazo hazitupi umaarufu au kutuongezea kipato. Pengine siyo Mungu alichotuumbia tukifanye hapa duniani.
Subscribe to:
Posts (Atom)




















