Thursday, December 31, 2009
KWAHERI 2009 KARIBU 2010
Pamoja na changamoto nyingi zilizojitokeza kwa mwaka 2009. Namshukuru Mungu mwaka 2009 ulikuwa wa mafanikio kwangu. Nawashukuru wote walionisadia kufikia malengo yangu. Nawashukuru wote waliopata fursa ya kupitia blog hii. Shukurani za pekee zimwendee Prosper Bello aliyekuwa wa kwanza kufuatilia blog hii na kutoa maoni yake. Namshukuru pia mfuatiliaji wa pili aliyejitokeza mwaka huu ambaye ameonekana kuwa mfuatiliaji mzuri wa Banzi wa Moro (Haja taja jina). Ingawa nimeshindwa kufikia lengo la kuning'iniza vitu 365 lakini 250 nazo si haba nimevunja rekodi ya mwaka jana. Endapo Mungu akinijalia nikaweza kumiliki camera yangu mwenyewe naahidi kuwaletea vitu vizuri mwaka 2010. HAPPY NEW YEAR.
NAMSHUKURU MUNGU NIMEWEZA KUNING'INIZA MENGI KWENYE BANZI WA MORO

Pamoja na majukumu mengi na mapya niliyokuwa nayo mwaka 2009 lakini namshukuru Mungu nimeweza kuning'iniza mengi katika blog hii. Kuna wakati nilining'iniza chache sana hasa mwezi Novemba 7 tu. Sababu ni nyingi- mtandao kugoma, na kutingwa na shughuli za ofisi pamoja na misiba haya yalionifanya nishindwe kutuma mambo mtandaoni. Namshukuru Mungu
MWAKA 2009 NILIIKOSA XMASS YA MATOMBO
Nilipanga kwenda kijijini Matombo Morogoro kwa likizo ya muda mfupi kusherekea sikukuu ya XMASS mwaka huu ilishindikana kutokana na majukumu ya hapa kazini. Pengine hiki ni moja ya kitu nilichokikosa mwaka huu
Kila kifo ni cha ghafula-Sheikh Yahya
Mapema leo asubuhi nilikuwa nikitazama kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC. Mmoja wa wageni waliokaribishwa katika kipindi hicho ni Mnajimu wa siku nyingi Afrika Mashariki na Kati Sheikh Yahya ambaye hivi karibuni utabiri wake uliodai kuwa atakayegombea nafasi ya Rais katika uchaguzi wa mwakani kumpinga Rais wa sasa Mhe. Jakaya Kikwete atakufa ghafla. Akionyesha uhodari wa kujenga na kutetea utabiri wake na hoja hiyo alisema kuwa wanadamu tusiogope kifo kwani kinapotokea kina faida na hasara. Kwa mfano ni pale tu mzazi anapofariki ndipo watoto wanapopata fursa ya kurithi mali za mzazi.
Samaki mkunje angali mbichi
TUTOKE HUKU
Simu inapotumika na mkulima kutika kupanga bei ya mazao shambani

Mwisho huu wa mwaka nawaletea picha iliyoshinda kwenye mashindano yaliyoendeshwa na jarida la kimataifa liitwalo 'Farming Matters.' Picha hii ni ya wakulima wa Phillipines maarufu kwa zao la mpunga. Mkulima anaweza kuwasiliana na mfanyabiashara kwa kutumia simu ya kiganjani kabla ya mavuno hivyo kuepukana na walanguzi kwani kwa kupitia simu majadiliano kuhusu bei hufanyika.
KAWAWA AMETUACHA
Tuesday, December 29, 2009
Mifereji ya barabara ya Kilwa isilipuliwe
Kuna zoezi linalokwenda kwa kasi la kujenga mifereji kwenye barabara ya Kilwa. Naambiwa kuwa hilo lilikuwa ni agizo la Mhe. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyeagiza mamlaka husika kushughulikia mifereji hiyo haraka iwezekanavyo kuepusha hatari ya kuharibika barabara mpya iliyojengwa. Ninachoona mimi ni kuwa mifereji hiyo inajengwa haraka lakini si kwa kiwango kinachotakiwa. Ni kweli wajenzi ni wazawa. Lakini uzawa isiwe 'issue' ya kulipua kazi. Kwa maana nimeshaona baadhi ya maeneo mifereji imeshaanza kuchimbika kutokana na mvua hizi zinazonyeesha.
Dawasco bomba linavuja kituo cha Msikiti-Kilwa Road
Leo asubuhi wakati nikija kazini karibu kabisa ya kituo cha Msikiti mara baada ya kumaliza makaburi ya Mbagala Mission tulikuta maji ya kitiririka barabarani yakiashiria kuvuja kwa bomba. Hatari ni kwamba hali hiyo isipodhibitiwa haraka maji yatachimba barabara na hivyo magari kukwepa shimo hilo hatimaye kusababisha msongamano wa magari pengine hata ajali ndiyo maana nawakumbusha DAWASCO wafanye hima kurekebisha hali hiyo.
Garage za mtaa wa Mkumba-Wailes ni uchafu
Jana jioni wakati nikitoka kazini nilibahatika kupitia mtaa wa Mkumba uliopo Wailes-Temeke na kuona magari mabovu pande zote za barabara hiyo. Nilipojaribu kuuliza ni kwanini kuwepo kwa hali hiyo? Nikajibiwa aah mzee usishangae hizo ni garage za mitaani.
Hivi kweli watendaji wa Temeke mmerizika na hali hiyo? Jiji hili bado kunakuwa na garage za mitaani? Aah ondoeni uchafu huo haipendezi hata kidogo.
Hivi kweli watendaji wa Temeke mmerizika na hali hiyo? Jiji hili bado kunakuwa na garage za mitaani? Aah ondoeni uchafu huo haipendezi hata kidogo.
Monday, December 28, 2009
Yanga Imara bado
RUZUKU IPIMWE KWA UZALISHAJI

Yapata miaka mitatu sasa tangu serikali ianze utaratibu wa kutoa ruzuku ya pembejeo hasa mbolea kwa wakulima hapa nchini. Ruzuku hii hutolewa kwa mfumo wa vocha. Mfumo huu wa ruzuku kwa kutumia vocha unakuwaje hasa. Hapa kichafanyika ni kwa serikali kugharamia asilimia fulani ya gharama za pembejeo kwa mfumo wa vocha hivyo kumpunguzia makali ya uzalishaji mkulima. Mfumo huu ulipoanza ulikumbana na matatizo mengi kila mwaka maboresho yamekuwa yakifanywa ili ruzuku iweze kutoa matokeo yanayokusudiwa. Mimi naamini kuwa matokeo mazuri yatapatikana kwa kuongezeka uzalishaji na kuleta tija kwa wakulima.
SIKUKUU NI YA WATOTO
Thursday, December 24, 2009
KHERI NA BARAKA ZA X-MASS NA MWAKA MPYA
Friday, December 18, 2009
Ni kweli mazingira ya dhiki hayatakuza elimu

Wakati nakaribia kutoka ofisini siku ya Ijumaa. Kwa haraka nilipata kusoma kichwa cha habari kisemacho "Mazingira ya dhiki hayatakuza elimu" makala iliyoandikwa kwenye gazeti la Rai 17-23 2009. Kichwa cha habari hii kimenivutia kusoma makala hii iliyoandikwa na Masumbuko Nesphory. Serikali haitaki lawama na walimu nao hawataki kulaumiwa. "Tuache siasa tuache porojo katika elimu. Tusilaumiane tuwajibike." Anamaliza mwandishi wa makala hii. Mwandishi ameandika mengi kwa pande zote mbili. Ni kweli mazingira ya sasa ya kutoa elimu kwa shule za umma hayaridhishi. Tafuta gazeti hili na soma makala hiyo. Picha kushoto kwa hisani ya gazeti la Rai
Naambiwa hiki ni kijiji cha China

Miaka takribani ishirini iliyopita China ilikuwa ikidharaulika sana. Labda ilikuwa ikiogopwa kwa wingi wa watu wake na umahiri wao kwenye vita. Lakini nchi za magharibi iliiponda sana hasa kutokana na siasa yake Ujamaa.
Lakini sasa ni tishio. Waamerika wanaigwaya China. Kitu gani ambacho China hawawezi kukifanya. China wamebakia kuwa wajamaa huku wakiboresha maisha ya wananchi wao. Hebu angalia picha kushoto kwako, hicho ni kijiji mojawapo kilichopo China. Wanapanga na kutekeleza haya ndiyo maendeleo tunayotaka. Ubepari sawa lakini kwa faida ya nani? Ubepari huku tunashindwa kuzibua mitaro ya maji machafu? Ubepari huku tukishindwa kupaka rangi hata majengo ya umma?Ubepari wakati makao makuu ya nchi umeme kwa mgao?
Ziara za mafunzo kwa wakulima

Moja ya urithi alioucha marehemu mama yangu ni doti ya Khanga iliyoandikwa "Tembea Uone" Ni kweli mimi mwenyewe nimetembea na kuona mengi na kujifunza mengi na kuacha mengi.
Tunapotaka wakulima wajifunze teknolojia mpya moja ya mbinu zinazotumika ni kuwapatia ziara za mafunzo. Bado tunaamini kuwa "Tembea uone." Kwenye ziara hizi wakulima huona na kujifunza haraka. Wanaweza kujifunza jinsi ya kufuga kuku kutoka kwa wakulima wenzao kwa mazingira yanayofanana na ya kwao, jinsi ya kulima aina fulani ya zao kama vile nyanya, vitunguu n.k. kwa ufanisi zaidi. Wanajifunza pia jinsi wakulima wanavyoweza kujenga nyumba nzuri kwa kutumia raslimali walizonazo. Wanaweza kujifunza pia kumbe hata mkulima wa embe anaweza kumiliki gari!
Ukiona huwezi kusahau kwa urahisi. Nahitimisha kwa kusema kuwa ziara za mafunzo kwa wakulima ni muhimu. Pichani wakulima wakiwa katika ziara ya mafunzo wakionyeshwa namna ya kuchota maji kwa ajili ya umwagiliaji toka kwenye kisima nyumbani kwake huko Ibumila Njombe.
Ungefuga kuku wa kienyeji

Sikukuu ya X-MASS na mwaka mpya inakaribia. Ni wazi kuwa bei ya nyama itaongezeka hata mara mbili. Familia nyingi hazitoweza kumudu kula nyama. Nyama ya kuku ndo usiombe kabisa nafikiri X-mass hii kuku atauzwa kuanzia shilingi 10,000 hadi 20,000/- Lakini mwananchi naomba nikuulize utashindwa kweli kufuga kuku wawili au watatu kwenye kibanda kidogo kwa mfumon huria? Mimi naamini ungefuga kuku wa kienyeji usingetaabika na kitoweo wakati wa sherehe hizi zinazokaribia tubadilike tuanze kufuga sasa kwa ajili ya Pasaka na Idd-Elftri ya mwakani.
Subscribe to:
Posts (Atom)






