Wednesday, January 22, 2014
Kutoka Kongo
Je, bado unaikumbuka ndoa hii ya kihistoria iliyofungwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya mwanaume mmoja kufunga ndoa na wanawake watatu. Jamaa anaonekana kufurahim, wanawake je? Hebu waangalie vizuri.
Mafuta ya ubuyu yanatoka katika mti huu
Huu ni mbuyu.Miaka ya nyuma mti wa mbuyu ulikuwa unaonekana hauna faida yoyote zaidi ya ubuyu. Ukubwa wake hauwezi hata kutoa mbao nzuri, haufai pia hata kuchoma mkaa! Lakini katika miaka ya hivi karibuni hapa Tanzania, mbuyu umewanufaisha watu wengi. Mafuta ya ubuyu yamekuwa yakiaminika kuwa tiba ya magonjwa mbalimbali hivyo kuwa biashara ya maana. Baadaye ilibainika kuwa mafuta hayo si salama. Hadi hivi sasa taarifa kamili haijatolewa kuhusu mafuta ya ubuyu. Tunasubiri taarifa rasmi.
Tuesday, January 21, 2014
Friday, January 10, 2014
Fenesi - sura inatisha manufaa ni makubwa
Ukiliona tunda la fenesi kabla halijakatwa kwa kweli halivutiii. Lina sura ya kutisha lenye nundunundu nyingi lakini likishakatwa ni tamu kulila. Licha ya utamu wake, fenesi lina faida zifuatazo kwa afya zetu.
i. Lina vitamini C ambayo huongeza kinga ya mwili
ii Hupunguza mafua
iii.Husaidia kupunguza maumivu ya kifua na homa
iv. Huupa mwili nguvu kwani yana madini ya wanga na sukari
v.Huondoa sumu mwilini hivyo kuwa na kinga ya saratani k.m. mapafu, midomo, kinywa na tumbo
vi.Tiba ya shinikizo la damu kwani lina madini ya potasium
vii.Hurahisisha mmeng'enyo wa chakula (digestion)
viii. Linasaidia kuzuia kuvimbiwa
ix.Kwa wenye matatizo ya macho husaidia uoni (Kwa mujibu wa Dr. Deepark Kevat wa Shree Hindu Mandal Hospital - Dar Es Salaam)
(Kwa hisani ya gazeti la Mwananchi 10/01/2014- Ijumaa)
i. Lina vitamini C ambayo huongeza kinga ya mwili
ii Hupunguza mafua
iii.Husaidia kupunguza maumivu ya kifua na homa
iv. Huupa mwili nguvu kwani yana madini ya wanga na sukari
v.Huondoa sumu mwilini hivyo kuwa na kinga ya saratani k.m. mapafu, midomo, kinywa na tumbo
vi.Tiba ya shinikizo la damu kwani lina madini ya potasium
vii.Hurahisisha mmeng'enyo wa chakula (digestion)
viii. Linasaidia kuzuia kuvimbiwa
ix.Kwa wenye matatizo ya macho husaidia uoni (Kwa mujibu wa Dr. Deepark Kevat wa Shree Hindu Mandal Hospital - Dar Es Salaam)
(Kwa hisani ya gazeti la Mwananchi 10/01/2014- Ijumaa)
Thursday, January 9, 2014
Nyerere na Karume
Hayati Mwl. J.K.Nyerere (kushoto) na Sheikh Abeid Amani Karume.Waasisi wa Muungano wa Tanganyika na Unguja iliyozaa TANZANIA. Wote walikuwa na nia njema na walifanikiwa. Tunakwenda wapi?
Unapoingia Lindi mjini
Kusini raha barabara ya lami hadi Mtwara. Hapa unaingia Lindi mjini. Hebu tupia jicho bahari ya Hindi.
Friday, January 3, 2014
Lazima utafunga tu
Kama futuru yenyewe ndiyo mazagazaga haya, lazima ufunge!- Picha kwa hisani ya kurasa za fb za Mibavu
Kumbe Mibavu Gungu ni Simba!
Sikujua kuwa rafiki yangu Mibavu Gungu ni Simba damu. Picha hii nimiipata kupitia ukurasa wake wa fb
Mwaka 2014 nimeanza na matunda
Wengi wetu hupenda matunda. Tunaambiwa matunda yana vitamin aina nyingi ambayo huipa miili yetu kinga. Kwenye picha kuna ndizi,mananasi,machungwa, zabibu,peyas na pichis. Tanzania tumebahatika ya kuwa na matunda ya tropiki na matunda ya kutoka sehemu za baridi kama Mgeta mkoani Morogoro, Njombe, Tukuyu, Lushoto na sehemu nyingine. Lakini matunda kama vile ndizi, mananasi na machungwa hupatikana kwa wingi kijijini kwangu Matombo mkoa wa Morogoro. Kilimo cha matunda ni Biashara. Kwenye mazingira yanakostawi matunda tujikite na kilimo hicho na tufuate ushauri kutoka kwa wataalamu tulime kwa faida. Wakulima tubadilike. Fedha ziku shambani.Karibu Morogoro tule matunda!
Thursday, January 2, 2014
Karibu mwaka 2014- Moro Oyee!
Mwaka 2013 ulikuwa na changamoto nyingi kwa Banzi wa Moro. Misiba mingi. Nimepoteza mjomba mdogo wangu na ndugu wengine. Hata hivyo kulikuwa wakati wa furaha pia. Harusi nyingi, watoto wamezaliwa na shughuli nyingi tu za kikazi. Namshukuru Mungu kwa kufanikiwa kuingiza posts 602 ambapo mwaka 2012 niliingiza posts 573.
Nawashukuru wadau wa Banzi wa Moro, wengi wamepitia Blog yangu mwaka 2013 lakini ni wachache sana waliotoa comments. Nawaomba mwaka huu mchangie zaidi katika matukio mbalimbali yatakayoonekana kwenye Blog hii.Kwa kuanza mwaka huu nawaletea waburudishaji wa Mji Kasoro Bahari (Moro) wakikumbushia enzi za Marehemu Mbaraka Mwinshehe, Salumu Abdallah na wanamuziki wengine mahiri wazamani wa Morogoro.
| Hata nikiwa mbali na Moro nakumbuka Moro Oyee..... |
Subscribe to:
Posts (Atom)


















