Wednesday, January 22, 2014

Mafuta ya ubuyu yanatoka katika mti huu

Huu ni mbuyu.Miaka ya nyuma mti wa mbuyu ulikuwa unaonekana hauna faida yoyote zaidi ya ubuyu. Ukubwa wake hauwezi hata kutoa mbao nzuri, haufai pia hata kuchoma mkaa! Lakini katika miaka ya hivi karibuni hapa  Tanzania, mbuyu umewanufaisha watu wengi. Mafuta ya ubuyu yamekuwa yakiaminika kuwa tiba ya magonjwa mbalimbali hivyo kuwa biashara ya maana. Baadaye ilibainika kuwa mafuta hayo si salama. Hadi hivi sasa taarifa kamili haijatolewa kuhusu mafuta ya ubuyu. Tunasubiri taarifa rasmi.

No comments: