Thursday, January 2, 2014

Karibu mwaka 2014- Moro Oyee!

Mwaka 2013 ulikuwa na changamoto nyingi kwa Banzi wa Moro. Misiba mingi. Nimepoteza mjomba mdogo wangu na ndugu wengine. Hata hivyo kulikuwa wakati wa furaha pia. Harusi nyingi, watoto wamezaliwa na shughuli nyingi tu za kikazi. Namshukuru Mungu kwa kufanikiwa kuingiza posts 602 ambapo mwaka 2012  niliingiza posts 573.




Hata nikiwa mbali na Moro nakumbuka Moro Oyee.....
Nawashukuru wadau wa Banzi wa Moro, wengi wamepitia Blog yangu mwaka 2013 lakini ni wachache sana waliotoa comments. Nawaomba mwaka huu mchangie zaidi katika matukio mbalimbali yatakayoonekana kwenye Blog hii.Kwa kuanza  mwaka huu nawaletea waburudishaji wa Mji Kasoro Bahari (Moro) wakikumbushia enzi za  Marehemu Mbaraka Mwinshehe, Salumu Abdallah na wanamuziki wengine mahiri wazamani wa Morogoro.

No comments: