Monday, February 2, 2015

Mkulima anayejiamini

Mwaka jana nilibahatika kuongea na wakulima wa mpunga katika skimu ya umwagiliaji ya Kamtonga wilayani Mvomero. Kilichonifurahisha ni kuona wakulima wengi vijana waume kwa wanawake wakijieleza kwa umakini mkubwa jinsi wanavyotumia teknolojia za kisasa za kilimo walizofundishwa kupitia mradi wa EAAPP kwa lengo la kuongeza uzalishaji na tija katika zao la mpunga. Bila kubabaika walisema kuwa mbegu ya mpunga TXD 306 (SARO) ni nzuri kwa uzalishaji ukilinganisha na mbegu nyingi za asili.

No comments: