Tuesday, January 28, 2014

Yapo mahindi rangi nyeusi

Wengi tumezoea mahindi rangi nyeupe au manjano. Lakini ya rangi nyeusi yapo pia.

Aina nyingi za karoti

Kuna karoti za aina nyingi; nyeupe, njano,kijani,nyekundu........

Kuna aina nyingi za bilinganya

Kuna aina nyingi za bilinganya ambazo wengi hatuzifahamu na hatujazila.

Adha ya ujenzi wa barabara ya mabus yaendayo kasi DAR

Mpaka itakapokuwa imekamilika. Ujenzi wa barabara ya mabus yaendayo kasi jijini Dar utakuwa umewatesa wengi na kwa kweli wachumi tunaweza kukokotoa gharama ya matumizi ya mafuta na kuchelewa kazini wakati wote wa ujenzi wa barabara hiyo/hizo. Tutashangaa!

Mbegu ya mpunga TXD 306 a.k.a SARO 5

Mbegu ya mpunga TXD 306  iliyozalishwa na watafiti wa kilimo Tanzania maarufu kwa jina maarufu la SARO 5 kwenye maonyesho ya kilimo kitaifa huko Dodoma ikipigiwa debe.

A man's life in 3 pictures


Ukiwa umetalakiwa unakuwa kama umenyonyolewa manyoya! Tafakari.

Wednesday, January 22, 2014

Vipando vya mahindi

Maonyesho ya vipando vya mahindi  kwenye maonyesho ya kilimo Kitaifa viwanja vya Nzuguni, Dodoma mwaka 2013

Zana za Kilimo

Miaka 10 iliyopita Taifa imefanya jitahada za makusudi ya kuongeza zana za kilimo nchini kwa kuboresha sera na kuwafanya wakulima kuweza kutumia zana mbalimbali za kilimo kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kuleta tija katika kilimo.

Chezea korosho wewe!

Korosho kujitangaza hata kwenye kanga.

Wakili yupi unayemfahamu katika picha hii?

Mimi namfahamu George Mandepo tu!

Kwetu pazuri!

Inawezekana picha hii haina uhalisia. Lakini kuna baadhi yetu tunaomiliki magari ya kifahari lakini hatuna makazi mazuri huko tunakofanyia kazi wale kule vijijini tulikotoka.Tubadilike.(Picha kwa hisani ya fb- George Mandepo)

Gari la shule linapokwama

Si wamelipa ada.Asukume nani?  (Picha kwa hisani ya George Mandepo)

Wako pamoja

Wako pamoja tokea mwaka 1962. Ni ubunifu mkubwa hongera sana

Mahindi mabichi

Biashara ya mahindi mabichi imeenea sehemu nyingi za nchi. Watu wengi hupenda kula mahindi mabichi yaliyochomwa

Enzi hizo

Enzi hizo tulichapa barua kwa typewrite. Na kutumia simu za mezani.

Madhara ya mvua Iringa

Mvua zinaendelea kunyesha sehemu nyingi za nchi hii kwa sasa. Pichani ni mafuriko yaliyotokea huko Iringa kutokana na mvua iliyonyesha tarehe 7 Januari 2014

Matangazo mengine bwana!

Inawezekana usielewe ujumbe wa tangazo hili

Kibanda cha mamalishe

Inasadikiwa kuwa hiki ni kibanda cha mamalishe. Tusicheke. Inabidimmiliki aweze kushauriwa ili aweze kuboresha kibanda hiki kwa lengo la kuvuitia wateja na kulinda afya zao. (picha kwa hisani ya Bw. George Mandepo)

Chai maharage bado zipo Zanzibar

Usafiri wa mjini kisiwani Zanzibar  kwa kutumia magari yajulikanayo 'chai maharage"  bado unatumika. Hebu angalia jinsi watalii walivyofurahi!

Hajali onyo lililotolewa

Mwenzetu huyu anaonekana kutojali onyo. Pengine hafahamu lugha za kiingereza na kiswahili!