Thursday, May 19, 2016

Tanzania imepania kuongeza uzalishaji wa mpunga

Mpunga ni zao linalostawi vizuri katika sehemu nyingi za nchi yetu hasa ukanda wa pwani na mabonde yanayozunguka maziwa yetu na inakopita mito mikubwa. Wakulima wengi huzalisha wastani wa tani 2 kwa hekta ambapo ni kidogo sana. Utafiti uliokwishafanyika hapa nchini unaonyesha kuwa kwa kutumia teknolojia bora za kilimo cha mpunga, uzalishaji unaweza kufikia tani 8
kwa hekta. Hivi sasa serikali inaboresha kilimo hicho kupitia miradi mbalimbali hasa kwenye skimu za umwagiliaji.

No comments: