Monday, July 13, 2015

Alinena kwa lugha za kimataifa


Hii ilikuwa Arusha mwaka huu

Tunasubiri ya Dodoma mwaka huu pia

Anacharaza kinanda


   Ningependa kucharaza kinanda kama anavyofanya huyu.

Altare nyumbani kwa Nkwera

Jumuiya ya Mt.Joseph Mfanyakazi ilipoazimisha  siku ya somo wa Jumuiya tarehe 2/5/2015. Wanajumuiya walikusanyika nyumbani kwa Mwl. Angriberth Nkwera na kusali pamoja. Altare ya Mungu inapohamia nyumbani kwake ni jambo la kumshukuru Mungu.

Tunaandaa database ya uwekezaji katika sekta ya kilimo

Kwa kushirikiana na Bill and Melinda Foundation na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika pamoja na wale wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi wakiwa katika mafunzo ya kuandaa database hiyo.

Hii ni familia yangu


Ndiyo. Hii yote ni familia yangu. Ni siku mtoto wetu Frt. Linto alipokuja kutuaga pale nyumbani Kisemvule. Frt. Linto anatoka India, lakini kwa takribani mwaka mmoja alikuwa parokiani kwetu Vikindu  kwa uchungaji. Alipopewa vazi la kuwa Frateri yeye alituomba mimi na mke wangu (Nancy) kuwakilisha wazazi wake ambao wasingeweza kuwepo siku hiyo. Kwa hiyo Linto ni mmoja wa familia yangu. Kwa sasa Ftr. Linto yuko Uganda kwa muda baadaye ataelekea Nairobi kwa masomo ya Teolojia.Pichani pia wanaonekana  waseminari ambao walikuwepo kwa mwaka mmoja parokiani kwetu wakianza mafunzo ya useminari kwa sasa wako Uganda.

Ilibidi kuweka kumbukumbu na watoto hawa




Junior na Herieth wa Buguruni ni watoto marafiki. Nilipowatembelea nyumbani kwao nilifurahishwa jinsi walivyokuwa wakishirikiana. Wanacheza pamoja na kula pamoja. Junior ni Mluguru na Herieth ni Mchagga. Ushirikiano waliounyesha ni dalili nzuri kuwa hata wazazi wao wanashirikiana. Hii ndiyo Tanzania umoja unajengwa toka tukiwa wadogo. Nami niliona ni heri nikapiga picha ya kumbukumbu pamoja nao.

Junior na Herieth wa Buguruni-Maghorofani





Junior na Herieth wanaishi kwenye jengo moja lililopo Buguruni -Maghorofani. Hawa wanatoka familia tofauti. Junior ni mpwa wangu anatoka Morogoro-Matombo na rafikiye Herieth ni Mchagga wa kutoka Rombo-Kilimanjaro. Nilipomtania uncle Junior kama tutapeleka "mahali Uchaggani" alikuwa na aibu na kubaki kucheka tu.

Africana Group kwa Christian Mkoba




Africana Group ni kundi la familia linaloundwa na ukoo wa Wambiki na watoto wao kwa asilimia kubwa. Kundi hili lipo jijini Dar Es Salaam. Lengo Kuu la kundi hili ni kudumisha uhusiano wa kifamilia uliokuwepo tangu zamani kwa bibi na babu zetu ambao makazi yao ni Morogoro, Matombo, Nige-Kariakoo. Kila mwezi hukutana mara moja nyumbani kwa mwanakikundi. Mwezi Juni Africana Group ilikutana nyumbani kwa ndugu yao Bw. Christian Paul Mkoba huko Kisemvule,wilayani Mkuranga, Pwani. Wakati mkutano unaendelea wajumbe wanaendelea na chakula pamoja na vinywaji walivyoandaliwa na mwenyeji wao.

Tunapokea zawadi kutoka kwa watoto wetu

Mwezi Juni 15,2015. Bw na Bibi Victor Shayo walifunga pingu za maisha ndani ya Kanisa la Mt. Vinsenti wa Paulo, Vikindu. Familia hiyo ilituchagua mimi na mke wangu kuwa wazazi wao wa kiroho katika maandalizi yote ya ndoa hiyo hadi walipofunga ndoa. Hapa wanatukabidhi zawadi yao baada ya kutukaribisha kwao wanakoishi (Vikindu). Asanteni sana. Tunawatakia ndoa yenye furaha.

Wamechagua mahali sahihi kupiga picha



Ni Maria Banzi na mdogo wake Nancy Maulidi Mbawala wakiwa nyumbani kwao Kisemvule!

Mount Meru Hotel-Arusha




Mount Meru Hotel - Arusha imerudi katika viwango vyake. Mazingira safi na huduma za kuridhisha. Usisite kufanya shughuli yako hapo au kukodi chumba hotelini hapo pamoja na familia yako kwa lengo la kutalii kwenye mbuga zetu za taifa.

Wadau wa Mbegu za mazao Tanzania


Watafiti kutoka Mikocheni

Baadhi ya watafiti nguli wa kituo cha utafiti wa kilimo Mikocheni wakifuatilia kwa makini hotuba ya Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika wakati wa uzinduzi wa taarifa ya kimataifa ya mwaka 2014 kuhusu baiteknolojia uliyozinduliwa kwenye viwanja vya makao makuu ya Wizara hiyo jijini Dar E s Salaam mwezi Juni 2015. Kituo cha Mikocheni ndiko kuliko maabara ya kisasa ya utafiti wa baiteknolojia katika kilimo.