Friday, November 23, 2007

TANESCO MPAKA MPANDISHE BEI?

Moja shirika la umma linalotoa huduma hapa Tanzania ambalo linawakera wananchi basi ni TANESCO. TANESCO haijapata kusifiwa hata mara moja. Na sikumbuki kama TANESCO imeshawahi kutangaza faida. Kila wakati wao wanajiendesha kwa hasara na kila wakati wananchi wananung'unika na huduma zao.

Kuingiza umeme ndani ya nyumba utasumbuana na TANESCO! Kulipia bills ni matatizo hasa wanaotumia mita kila wakatia mita zao zinasoma zaidi ya matumizi. Sasa wamekuja na jipya wanataka kuongeza malipo zaidi kwa kuingiza umeme ndani ya nyumba au kiwanda pamoja na malipo zaidi kwa matumizi ya umeme. Hebu tufikiri kweli mwananchi wa kawaida anaweza kulipia Tshs 500,000/= ili apate umeme nyumbani kwake. Sote tunafahamu jinsi umeme ulivyo muhimu kwa maendeleo yetu. Kwa mwendo huu wa TANESCO tutafika? TANESCO hamfanyi vizuri mapaka mpandishe bei?

NAKUFAGILIA RAIA MWEMA

Nimeshikilia gazeti jipya "Raia Mwema" Toleo Na 4. Hili ni gazeti makini linalotokana na waandishi makini waliobobea,gazeti linalotoa uchambuzi wa kina. Ndiyo maana nalifagilia. Hebu angalia makala za toleo hili- Chadema, Zitto Kabwe na hadithi ya Keki, Watu weusi tuna akili ndogo?, Ngoma inapotawaliwa na harufu mbaya,Spika Sitta na vazi lake kutoka London!Nani anayeuzima mshumaa wa Serikali? Na nyingine nyingi unaposoma unatafakari, unapata ujumbe. Hili si gazeti la utani utani, la porojo, udaku!


Asante Ulimwengu na timu yako kutuletea Raia Mwema.

VETA MTWARA BORESHENI HUDUMA!

VETA MTWARA ni moja vyuo bora hapa nchini vinavyotoa elimu ya Ufundi. Chuo hiki kimejengwa kwa kufadhiliwa na serikali ya Japan. Chuo kimejengwa kando kando ya bahari ya Hindi sehemu inayojulikana Shangani ambayo ni maarufu sana pale Mtwara.

Chuo hiki kinauwezo wa kuchukua wanafunzi wapatao 1000 kwa wakati mmoja.
VETA Mtwara pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali pia ina vitega uchumi vingi kama huduma za malazi, chakula na kumbi za mikutano.

Pamoja na mazingira mazuri yaliyopo VETA Mtwara, huduma zitolewazo bado ni hafifu hasa kwa upande wa chakula. Wahudumu hawachangamkii wateja na unapotaka huduma unaweza kuambiwa hakuna. Chakula- Hakuna, Kinywaji - Hakuna. Eh basi kwaheri.

Kwa kweli inasikitisha wakati mwenyeji wako anapokutoa na kukupeleka mahali fulani ambapo anategemea kuwa unaweza kupata huduma safi anavunjwa moyo na hizi HAKUNA HAKUNA.

VETA Mtwara ni Taasisi ya kujivunia mjini Mtwara na sitoshangaa kama itakuwa CHUO KIKUU hapo baadaye. Lakini boresheni huduma zenu.