Friday, November 23, 2007

TANESCO MPAKA MPANDISHE BEI?

Moja shirika la umma linalotoa huduma hapa Tanzania ambalo linawakera wananchi basi ni TANESCO. TANESCO haijapata kusifiwa hata mara moja. Na sikumbuki kama TANESCO imeshawahi kutangaza faida. Kila wakati wao wanajiendesha kwa hasara na kila wakati wananchi wananung'unika na huduma zao.

Kuingiza umeme ndani ya nyumba utasumbuana na TANESCO! Kulipia bills ni matatizo hasa wanaotumia mita kila wakatia mita zao zinasoma zaidi ya matumizi. Sasa wamekuja na jipya wanataka kuongeza malipo zaidi kwa kuingiza umeme ndani ya nyumba au kiwanda pamoja na malipo zaidi kwa matumizi ya umeme. Hebu tufikiri kweli mwananchi wa kawaida anaweza kulipia Tshs 500,000/= ili apate umeme nyumbani kwake. Sote tunafahamu jinsi umeme ulivyo muhimu kwa maendeleo yetu. Kwa mwendo huu wa TANESCO tutafika? TANESCO hamfanyi vizuri mapaka mpandishe bei?

No comments: