Monday, January 14, 2008

MWAKA 2007 NI HISTORIA, 2008 UTAKUWAJE?

Heri ya mwaka mpya wasomaji wa Blog hii. Mwaka 2007 ulikuwa na mambo mengi vituko vingi, bashasha nyingi, kashkash au mitikasi mingi kama mdogo wangu Kamsopi anavyozoza.
Hata hivyo namshukuru Mungu kwa kunilinda na kunipa afya ya kutosha kuweza kutekeleza majukumu yangu kwa mwaka mzima na kikubwa ni kuniwezesha kupata MKATE wetu wa kila siku mimi na familia yangu kama tunavyoomba siku zote.

Kweli nimekuwa mvivu sana kuandika kwenye blog yangu kwa kipindi cha mwaka 2007. Pengine hii ndiyo ile hali tuliyonayo waswahili wengi, nitafanya kesho, kesho, hadi mwaka unakatika. Baadaye miaka 60 inafika tayari umeshafungwa goli la lala salama. Ulikuwa na mipango ya kujenga nyumba 3. Moja Dar, nyingine Morogoro mjini na nyingine kijijini Matombo lakini unashtuka umejenga nyumba 0 hayo yamewakuta wengi tu.

Jamani eeh, sasa mimi naahidi kupunguza uvivu angalau makala za mwaka huu ziongezeke. Lengo MAKALA 100. Mmenipata? Eeh ndiyo hivyo tena lazima kuwa na malengo, vinginevyo nI uswahili uswahili tu. Na utanipimaje? Siyo UTANITAMBUAJE ya Beny Mwaitege. Chati siyo huyo mwalafyale?

Karibu mgeni wetu 2008. Sijui ulikotoka, lakini karibu duniani. Hapa umeyakuta na utayaona mengi. Tuvumilie mgeni wetu. Lengo la mwaka huu nimeshalitaja hapo juu. Tushirikiane na naomba mnipatie maoni yenu wasomaji wangu ili nami nipate moyo wa kuandika!

"HAPPY NEW YEAR"

1 comment:

Belo said...

Kweli 2007 ulikuwa mvivu blog ilianza 2006 na uliandika makala 16
2007 ukaandika tena makala 16
2008 hakuna kulala ukilala ntakuamsha
HAPPY NEW YEAR