Thursday, September 25, 2008

Nchi za SADC na Upashanaji Habari katika Kilimo

Wataalamu 22 kutoka nchi 14 zilizo katika umoja wa SADC wanaendelea na warsha ya kujadili jinsi ya kutumia nyenzo ya Habari na Mawasiliano katika kuboresha uzalishaji katika Sekta ya Kilimo. Wataalamu hao wanaangalia ni wadau gani wanaohitaji habari za kilimo, wanazitumiaje habari hizo, zinapatikanaje, mikakati gani itumike kuhakikisha kuwa mfumo unakuwepo wa kutumia habari na mawasiliano ili utumike katika kuwasaidia watunga sera na watoa maamuzi katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika sekta ya kilimo, ni uwezo gani uliopo kwenye masuala ya habari na mawasiliano kwa wadau wa kilimo. Nyenzo na utaalamu upo? Hayo ndiyo mambo yaliyotuleta hapa Gaborone, Botswana kwa muda wa siku tatu. Tanzania inawakilishwa na wataalamu wawili huku jinsia ikizingatiwa. Wataalamu wanatoa hoja zao za nguvu mambo yanachambuliwa na kuwekwa sawa. Hatimaye viongozi wetu tutawaeleza. Cha ajabu katika kundi hili Afrika ya Kusini hawamo licha ya kuwa wanachama wa SADC. Naambiwa aah wao wameshapiGa hatua kubwa kwenye nyanja hii. Nchi zinazoshiriki katika warsha hii ni Tanzania, Zambia, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC),Zimbabwe, Lesotho, Swaziland,Mauritius,Seychelles,Madagascar,Mozambique,Angola,Namibia na wenyeji wetu Botswana.

Wednesday, September 24, 2008

Mashamba katika mchoro wa "Pie Chart" Afrika ya Kusini

Ukiwa angani wakati unatua jijini Johanesburg, Afrika ya Kusini, ukichungulia dirishani utaona maumbo ya kupendeza sana ya mashamba. Hakuna sababu ya kumuuliza mtu, unaona mashamba katika maumbo mbalimbali. Kumbe inawezekana kabisa kuwa na mashamba katika maumbo ya mduara na kutengeneza maumbo ya "Pai" kutegemea na mazao unayozalisha. Kama mkulima analima ngano kwa wingi basi sehemu kubwa ya mchoro inakuwa ni ngano hivyo hivyo kwa mazao yanayolimwa kwa sehemu ndogo na wakati tofauti kiasi cha kutoa picha nzuri ukiwa angani. Hata rangi zinajionyesha waziwazi. Kumbe hata wakulima wanazitumia hesabu za "pai" vizuri. Hapo ndipo walipofikia wasouth kwenye kilimo. Kwa hali hii mwanafunzi ataogopaje hesabu kwani anaona jinsi inavyotumika.

Kweli Botswana ni nchi ya nyama

Unapoingia kwenye ndege ya Air Botswana haipiti hata dakika 10 kabla hujarushiwa kipaketi cha nyama ya kukausha safi kilichofungwa vizuri utafune kwa raha zako huku wakikuuliza ni kinywaji gani unataka ushushie. Botswana hapo wanaanza kutangaza nyama. Jana jioni kwenye chakula cha jioni pale Grand Palm Hotel kulikuwa na nyama zilizotayarishwa kwa njia tofauti na ni nyingi tu. Mchana huu tumepata chakula chetu huku nyama zikiwa nyingi tu tena zimeandaliwa vizuri hata mifupa imekatwa vizuri! Ilibidi nimuulize Mtswana mmoja . "Nyie mnakula nyama sana hampati ugonjwa wa "gaoti"? Yeye alisema tatizo hilo limeanza kujitokeza sasa hasa kwa wanaokunywa pombe! Tanzania tunashindwa hata kuwatayarisha vizuri dagaa kamba "prawns" na kufanya bite kwenye AIR Tanzania?

ATCL mnatuangusha

Niko jijini Gaborone, Botswana tangu jana kuhudhuria warsha kuhusu Menejimenti ya Habari na Mawasiliano katika Utafiti wa Kilimo na Maendeleo. Safari yangu kufika hapa haikuwa nzuri hata kidogo. Kwanza tulichelewa kuondoka Dar kwa masaa 8. Kwasababu hiyo tuliikosa ndege ya kuunganisha toka Johanesburg kwenda Gaborone. Hata hivyo tulifanikiwa kuunganishwa kwenye ndege ya AIR Botswana. Wakati wote tulipokuwa Dar tukisubiri kuundoka tulikuwa tunatangaziwa kuwa tutaondoka saa 5.30, mara saa 7.30 kitu ambacho hakikutokea hadi tulipoondoka saa 8.30. Abiria wapatao watatu ilibidi wavunje safari zao kwani walijua kuwa wasengeweza kuwahi shughuli zao au kupata ndege ya kuunganisha huko waendeko.

Wazungu wawili (mtu na mkewe) tuliosafiri ndege moja ambao walikuwa ni watalii kutoka Afrika ya Kusini hawakusita kusema kuwa walipokuwa Tanzania mambo yalikuwa mazuri sana walisifu vivutio vyetu vya utalii (Bara na visiwani) ni vizuri sana na kusema Watanzania ni wakarimu sana na ni wa amani. Tatizo ni kwenye usafiri wa ndege kwani wakati wakiwa nchini kulikuwa na uchelelewaji wa ndege kuondoka kila waliposafiri na hasa ATCL. Ndugu zangu ATCL kweli mnatuangusha. Tatizo ninaloliona mimi ni menejimenti kuto kutoa uamuzi sahihi kwa wakati unaofaa. Halafu pale Airport kuna wafanyakazi wengi tu wanazagaa zagaa sijui na wa Swissport kazi yao ni nini?

Sunday, September 21, 2008

Samaki uhai wa akina mama wa Mkuranga

Kila siku asubuhi asilimia 40 ya wasafiri kutoka Mkuranga kwenda jijini Dar ni wanawake. Wengi wa wanawake hawa hubeba ndoo za plastiki. Hii inaashiria nini? Ndoo hizo hutumika kubeba samaki wanaowanunua kutoka soka la samaki Kigamboni. Wanawake hawa ni mahili sana. Hujua kukimbilia mabasi, huamka mapema asubuhi na hutunza fedha zao sehemu ambayo itakuwa vigumu kwa vibaka kuiba! Jem biashara ya samaki inalipa? Anajibu mama mmoja. Inalipa baba ikiwa unamtaji mzuri. Pia inategemea soko kule Kigamboni. Kweli akina mama hawa wameweza kufanya mengi kupitia biashara ya samaki kama vile kusomesha watoto. Aidha huwasaidia akina baba kuboresha bajeti ya nyumbani!

Wednesday, September 17, 2008

HIVI TUNAELEWA NYIMBO ZINAZOIMBWA KWA LUGHA YA KIINGEREZA?

Adamu Lusekelo ni Mwandishi Mwandamizi hapa nchini. Mimi binafsi ninamfahamu. Jinsi anavyoandika ndivyo alivyo. Soma Mraba wake wa LIGHTTOUCH kila Jumapili kwenye gazeti la "Sunday News" utapata ujumbe kama utamwelewa unachokiandika. Anaandika kwa lugha nyepesi na ya kuvutia yenye mzaha lakini..... Hiyo ndiyo maana ya LIGHTTOUCH - pengine niseme ni "kuuma na kupuliza." Jumapili hii alikuja na kichwa cha habari " The Nasty generation gap!" (MPASUKO KWA VIZAZI ---tafsiri yangu). Alipoandika kuwa vijana walikuwa wanafurahia nyimbo iliyokuwa ikiimbwa ya " Do me ! Do me !" huku wakiirudia rudia. Nabaki nikijiuliza, je vijana hawa wanajua maana ya nyimbo zinazoimbwa kwa kiingereza? Maana wasanii huwa hawaimbi kwa lugha Nyepesi. Wastafsiri "Do me" kwa tafsiri nyepesi. Kwa kawaida wasanii hutumia lugha za mafumbo. Msikilize Juma Nature, Ali Kiba, Nyoshi El Sadat, Muhidin Gurumo. Utafahamu nini ninachozungumza. Nyimbo hiyo kwa tafsiri sahihi ni MATUSI! Niwaambieni.

Madereva Taxi wa uwanja wa ndege Dar acheni hizo

Kila Jumapili sikosi kumsoma Tony Zakaria kwenye Sunday News katika mraba wake unaojulikna kwa jina la "FIRINGLINE." Tarehe 14 September Tony alilamika jinsi tunavyoshindwa kutumia fura tuliyonayo ya utalii kuongeza pato la Taifa. Lakini alinifurahisha zaidi kwenye para moja alipoandika kuwa Madereva taxi waliopo uwanja wa Taifa wao wanaongalia jinsi gani ya kumtoza mteja fedha nyingi kutoka Uwanja wa ndege hadi anakokwenda. Kweli, ni kitu cha kawaida kabisa kuambiwa kutoka uwanja wa ndege hadi Mbagala/Kawe/Mwenge ni shilingi 40,000. Hivi kweli kwa bei hizi hata hao watalii wanaweza kulipa kweli. Tunapotoka tukiamini kuwa kila mtalii ni tajiri na yuko tayari kulipia kiasi chochote kwa huduma yoyote. Madereva taxi acheni hizo. Tuboreshe huduma zetu tutapata haki zetu.

Sera nzuri utekelezaji hafifu

Watanzania, na wasio watanzania, wasomi na wasio wasomi niolibahatika kuzungumza nao wanasema, Watanzania ni wazuri katika kuandaa sera lakini utekelezaji wa kile kilichoandaliwa una walakini mkubwa. Sekta zote zina sera nzuri iwe utalii, kilimo, viwanda, afya .... lakini kwanini hatuendelei? Je, sera zilizopo zinafuatwa? Nani wa kutekeleza sera hizo? Tatizo hilo tutalitatuaje. Tufikiri sote. Natumie maoni yako.

Saturday, September 6, 2008

Sabodo kaandika, Makwaiya "kalonga" simu za viganjani tunaibiwa

Mmoja wa matajiri wakubwa hapa Tanzania - Mzee Sabodo imembidi kulipia ukurasa mzima kwenye gazeti la "Daily News" wiki ya jana ili kulalamika jinsi watanzania tunavyoibiwa kijanja na makampuni ya simu za viganjani kwa gharama kubwa za huduma hiyo. Hakulalamika hivi hivi alikuja na mahesabu kuwa kwa sasa inasemekana kuna wateja milioni 15 wa simu za viganjani. Hebu fikiria iwapo kila mteja atutumia sh-50 tu kwa siku ni shilingi ngapi makampuni hayo yanavuna burebure tu. Kwa wiki, mwezi na mwaka je? Alihitimisha kwa kusema hii pengine ni skandali kubwa zaidi kuliko EPA au RICHMOND.

Jana Ijumaa, katika Gazeti hilo hilo la "DailY News" Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa siku nyingi hapa nchini. Bw. Makwaia Kuhenga katika "Mraba" wake amejadili kwa kina aliyoandika Sabodo.

Hili si geni, blog hii iliwahi kumsikia Mbunge Ndesamburo akibainisha hili kwenye moja ya vikao vya Bunge kule Dodoma. Lakini Watanzania bado! Kweli simu za mkononi zina manufaa yake. Lakini tuangalie gharama yake. Kuna baadhi ya watu gharama ya simu kwa siku ni kubwa kuliko fedha anayoacha nyumbani kwa matumizi!

Wednesday, September 3, 2008

LUGALUGA WAANZA KUJITAYARISHA KWA KILIMO

Ushirika wa Kilimo na Maosko ujulikanao kwa jina la Lugaluga lenye makao yake makuu katika Manispaa ya Morogoro hivi sasa imeanza kutayarisha mashamba yao tayari kwa msimu wa kilimo 2008/9. Kwa mujibu wa Katibu wa Ushirika huop Bw. John Waziri. Ushirika huo una eneo la shamba lipatalo ekari 16,000 katika kijiji cha Kimambira wilayani Mvomero.

Ushirika huo wenye wanachama wapatao mia moja umepanga kulima ekari 2000 za mpunga kwa mwaka 2008/9.Tayari mipango ya kuwakopesha matrekta wanachama wa Lugaluga uko kwenye hatua za mwisho. Kupatikana kwa matrekta hayo yasiyopungua matano kutawawezesha washirika hao kutayarisha mashamba yao mapema tofauti ilivyokuwa mwaka jana ambapo matrekta yalichelewa kuanza kazi shambani.

Akiongea na blog hii Bw. John Waziri amesema kuwa wanapata ushirikiano mzuri kutoka kwa viongozi wa ngazi zote mkoani Morogoro wakiwemo Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Saidi Kalembo na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Bi Hawa Ngulume cha kutia moyo ni kwamba wameshatembelea eneo la shamba hilo kubwa.

Blog hii ilipata nafasi ya kufika kimambila na kuona shamba hilo na kushuhudia jinsi wananchama walivyokuwa na ari ya kujikita kwenye uzalishaji wa kilimo.

Mashamba ya Kimambila yakiboreshewa miundo mbinu (hasa barabara za kufika shambani,maji na umeme. Na iwapo wakulima watapata zana za kilimo kama vile matrekta na kupata fursa ya kupata pembejeo za kilimo (mbolea, mbegu na viuatilifu) kwa wakati wakati unaofaa.Kuandaa mtandao wa kilimo cha umwagiliaji. Yanaweza kuzalisha chakula cha kutosha na kuchangia katika adhima ya kuufanya mkoa wa Morogoro kuwa ghala ya chakula ya Taifa.

MKULLO KACHEKA KWENYE ATM

Siyo siri mtu wangu, kama zali vile, nilikuwa nimechacha ile mbaya. Hata mwanangu Mary alikuwa analitambua hilo kwani zawadi ilikuwa hakuna tena. Maana si unajua, kama alivyosema bosi wetu wa TUCTA kuwa mshahara ni "mbolea" ya wafanyakazi. Mbolea hiyo ilichelewa kutufikia si ya "kupandia" wala "kukuzia"! Ikawa malumbano kati ya "TUCTA" na Ma Ghasia na Mzee Mkullo wa "Treasury"? Si ndo ikwa ahadi, ahadi na huku "TUCTA" ikisisitiza kuwa kama hiyo mbolea haitatolewa wafanyakazi wataingia barabarani? Basi kama zali mwanangu leo asubuhi kuweka vitu kwenye ATM mbolea waaa!