Wednesday, September 17, 2008

Madereva Taxi wa uwanja wa ndege Dar acheni hizo

Kila Jumapili sikosi kumsoma Tony Zakaria kwenye Sunday News katika mraba wake unaojulikna kwa jina la "FIRINGLINE." Tarehe 14 September Tony alilamika jinsi tunavyoshindwa kutumia fura tuliyonayo ya utalii kuongeza pato la Taifa. Lakini alinifurahisha zaidi kwenye para moja alipoandika kuwa Madereva taxi waliopo uwanja wa Taifa wao wanaongalia jinsi gani ya kumtoza mteja fedha nyingi kutoka Uwanja wa ndege hadi anakokwenda. Kweli, ni kitu cha kawaida kabisa kuambiwa kutoka uwanja wa ndege hadi Mbagala/Kawe/Mwenge ni shilingi 40,000. Hivi kweli kwa bei hizi hata hao watalii wanaweza kulipa kweli. Tunapotoka tukiamini kuwa kila mtalii ni tajiri na yuko tayari kulipia kiasi chochote kwa huduma yoyote. Madereva taxi acheni hizo. Tuboreshe huduma zetu tutapata haki zetu.

No comments: