Saturday, September 6, 2008

Sabodo kaandika, Makwaiya "kalonga" simu za viganjani tunaibiwa

Mmoja wa matajiri wakubwa hapa Tanzania - Mzee Sabodo imembidi kulipia ukurasa mzima kwenye gazeti la "Daily News" wiki ya jana ili kulalamika jinsi watanzania tunavyoibiwa kijanja na makampuni ya simu za viganjani kwa gharama kubwa za huduma hiyo. Hakulalamika hivi hivi alikuja na mahesabu kuwa kwa sasa inasemekana kuna wateja milioni 15 wa simu za viganjani. Hebu fikiria iwapo kila mteja atutumia sh-50 tu kwa siku ni shilingi ngapi makampuni hayo yanavuna burebure tu. Kwa wiki, mwezi na mwaka je? Alihitimisha kwa kusema hii pengine ni skandali kubwa zaidi kuliko EPA au RICHMOND.

Jana Ijumaa, katika Gazeti hilo hilo la "DailY News" Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa siku nyingi hapa nchini. Bw. Makwaia Kuhenga katika "Mraba" wake amejadili kwa kina aliyoandika Sabodo.

Hili si geni, blog hii iliwahi kumsikia Mbunge Ndesamburo akibainisha hili kwenye moja ya vikao vya Bunge kule Dodoma. Lakini Watanzania bado! Kweli simu za mkononi zina manufaa yake. Lakini tuangalie gharama yake. Kuna baadhi ya watu gharama ya simu kwa siku ni kubwa kuliko fedha anayoacha nyumbani kwa matumizi!

No comments: