Monday, September 30, 2013

Vipimo ni vya aina nyingi u sahihi je?

Kila aina ya kipimo kina matumizi yake. Lakini  nina mashaka kama wadau wanafahamu jinsi vinavyotumika.Anayefahamu ni mpimaji. Kwa mfano hata mimi wakati mwingine huwa nachanganywa na hicho kipimo chenye rangi nyekundu. Uzito (jiwe) scale (ruler) vyote hutumika kwa pamoja. Kwa kweli hapa ni rahisi kuibiwa hasa kwa wakulima wetu. Ni vyema wadau wakaelimishwa.

T-shirts kutoka Tanzania

T-shirt kutoka Tanzania, ni nzuri na ujumbe unaeleweka.Hivi ni kwanini Watanzania hatupendi chetu. Penda chako hata kama ni kibaya.

Mkaa kutoka maganda ya Karanga

Je tunazo karanga za kutosha za kukidhi mahitaji ya mkaa kutoka maganda ya karanga? Watafiti nipeni jibu. Pichani  mkaa wa karanga ukiwa juu ya meza kwenye maonyesho ya wakulima kitaifa yaliyofanyika Dodoma viwanja vya Nzuguni 2013.

Phillips ya kulia 'feki'

Mtaalamu wa kutambua bidhaa feki sokoni hasa za viwandani amebainisha kuwa hiyo bulb ya energy server iliyoko kulia ni feki lakini zote ni Phillips

Ufuta aina ya Lindi 02 hutoa magunia 15 ya kilo 100 kwa hekta

Siajabu kwa mkulima kuvuna magunia 15 ya ufuta yenye kilo 100 kila gunia kwa hekta. Hii inawezekana kwa kulima ufuta aina ya Lindi 02 ambayo hukomaa kati ya siku 100-110 tangu iote.Aina hii ya ufuta ina asilimia 55 ya mafuta. Hii ni habari njema kutoka kwa watafiti wa Kilimo kutoka kituo cha Utafiti Naliendele,Mtwara.

Machungwa matamu

Tanzania imebahatika kuwa na hali ya hewa inayoweza kustawisha mazao mbalimbali yakiwemo machungwa. Pichani vijana wa kisemvule wakijishughulisha na biashara ya machungwa kwenye kituo cha mabus hapo kijijini.

Maji bwelele Kisemvule

Wakati wengine wana shida kubwa ya maji, wananchi wa kijiji cha Kisemvule wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani nchini Tanzania maji si tatizo ukichimba kidogo unapata maji ya kutosha tena siyo ya chumvi.Hii pengine ndiyo sababu ya wawekezaji wa viwanda kupenda eneo hili na hivi sasa kuna viwanda vingi kikiwemo cha sementi ambacho kinatumia maji mengi.

Wanawake watafiti wa Kilimo


 Ishika Mshaguley na Vidah Mahava ni Watafiti wa Kilimo wanawake kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. Hapa wako kwenye kikao kazi cha Kupelemba na Kutathmini shughuli za Utafiti wakiwa kwenye sekretarieti ya Kikao hicho.Kila mmoja wao ana kidadavuzi mpakato!


Waumini wakiwa katika sherehe ya Mt. Visent wa Paulo Parokia ya Vikindu




Fr. Jinu akifanya mawasiliano

Mmoja wa Mapdri wa Parokia ya Vikindu, Fr.Jinu Joseph akifanya mawasiliano kwa kutumia simu yake ya mkononi huku masista wa Carmel wakifuatilia kwa makini matukio ya sherehe ya Mt.Vinsenti wa Paulo iliyofanyika tarehe 29/9/2013 kwenye viwanja vya parokia ya Vikindu.

Mkereketwa wa St.Vincent de Paul Vikindu

Mtoto huyu anapendwa na wazazi wake. Wazazi ni waumini wa Kanisa Katoliki St.Vincent De Paul, Vikindu wamemnunulia T-shirt nzuri ya Mt.Vinsenti wa Paulo.Ona alivyofurahi!

Wanakwaya wa Mt.Veronica kigango cha Kariakoo

Hii ndiyo kwaya ya Mt.Veronica kigango cha Kariakoo, Jimbo kuu la Dar Es Salaam waliokuja kuwapa shavu  marafiki zao wa Kwaya ya Mt.Vinsenti wa Paulo wakizindua Album yao ya Video "Inanibidi Nikeshe" iliyozinduliwa  tarehe 29/09/2013

Je, umeshawahi kumuona Ngongoti?

Kigango cha Malela Parokia ya Vikindu walileta Ngongoti kusherehesha sikukuu ya Somo wa Kanisa Mt.Visenti wa Paulo tarehe 29/9/2013.

Hawa ni Mapadri wa St.Vincent de Paul, Vikindu, Tanzania

Fr.Mathayo (Left) and Jinu Joseph-Vikindu Roman Catholic Priests

Album ya Video-Inanibidi Nikishe yazinduliwa

Jana tarehe 29/9/2013 Kwaya ya Mt.Vinsenti wa Paulo, Vikindu ilizindua album yake ya kwanza ya Video inayojulikana kwa jina la "Inanibidi nikeshe." Uzinduzi ulikuwa wa kufana sana. Pichani mgeni rasmi Bw. Peter Vava akizindua ALBUM hiyo.

Friday, September 27, 2013

Kumwagiana tindakali ni unyama

Hivi Watanzania tumefikia hatua hii ya kinyama? Mtun kama akikukosea, uungwana ni kumuuliza kwanini amekutendea hivyo. Hakuna haja ya kufanyiana visa kama hivi vya kumwagiana tindikali.Pichani Frateri Richard Haki akimsaidia Padri Anselmo Mwang'amba wa Kanisa Katoliki Zanzibar aliyemwagiwa tindikali hivi karibuni.

Kuku wetu wa asili au wa kienyeji ni watamu!

Kuku wa kienyeji wakitunzwa vizuri wanakuwa katika hali hii na utashangaa kuambiwa kuwa ni kuku wa kienyeji. Hakika kuku wetu wa kienyeji au wa asili ni watamu.Tufuge kuku kwa bidii angalau kuku wa tano wa asili kwa kila nyumba.

Ndizi zinaweza kumtoa lakini mtaji mdogo

Mwanamama huyu mchuuzi wa ndizi anahitaji mtaji mkubwa zaidi aweze kuuza ndizi zake kwa faida na kumsaidia huyo anayemtegemea aliyelala kifuani kwake. Wanawake wa aina hii wako wengi wanajitegemea. Wamekimbiwa na wanaume waliowazalisha lakini sikumoja watafanikiwa.Kuna haja ya Taifa kuwangalia na kuwawezesha akina mama wa aina hii.

Pombe ya asili

Pombe ni pombe tu iwe ni ya asili au ya kutoka wapi. Kikubwa pombe ni kinywaji chochote chenye kilevi.

Kuwawezesha wanawake kuongeza thamani ya mazao

Wanawake hawa wamejifunza jinsi ya kupanga nyanya vizuri ili zisihabribuike tayari kwa kusafirishwa. Nyanya hizi haziwezi kuharibika kirahisi hivi kutunza ubora wake kwa muda mrefu. Ni vyema kuwajengea uwezo wanawake katika kuongeza ubora wa mazao ya kilimo.

Hatujafanya vizuri katika Ufugaji wa samaki wa mabwawa

Tanzania hatujafanya vizuri katika ufugaji wa samaki kwa kupitia mabwawa licha ya fursa zilizopo. Kuna kutajirika kwa kufuga samaki pia ni njia rahisi ya kujipatia lishe.

Furaha ya Power Tiller

Kweli ni furaha ya Power Tiller. Hakuna anayependa kulima kwa mkono. Kilimo cha mkono kinachosha,tija ni ndogo na pia hakivutii vijana. Je, powertillers zilizokuwa gumzo mwaka 2010 zinaendeleaje huko vijijini waliko wakulima?

Unaweza kusema nini kuhusu picha hii?


Tuesday, September 24, 2013

Watawa kwenye sherehe ya Mt. Monica

Jumuiya Ndogondogo ni pamoja na watawa. Pichani watawa wa Parokia ya Vikindu wakiwa kwenye sherehe ya Jumuiya ya Mt. Monica
.

Fr. Mathayo akiendesha Ibada ya Misa Takatifu

Fr. Mathayo akiendesha Ibada ya Misa Takatifu katika Jumuiya ya Mt. Monica ya Parokia ya Mt.Visenti wa Paulo-Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam.

Mashindano ya soka kijijini Kisemvule

Kuna mashindano ya mpira wa soka yanayoendelea kijijini Kisemvule hivi sasa. Mshindi hajapatikana lakini hapa kuna vipaji kwakweli kuna vijana wanaoweza kuuchezea mpira wapendavyo!

Kijana akijaanda kuiba mafuta kutoka kwenye lori la mafuta

Kuna vijana wenye mazoea ya kufuatilia malori yanayosafirisha mafuta kwa lengo la kuyaiba kupitia mifuko ya rambo. Ni hatari kwa uhai wao na pia mafuta wanayoiba mara nyingi ni mabaki ya mafuta kwa hiyo kuna hatari kwa wanaouziwa kutumia mafuta yaliyo chini ya kiwango. Tujihadhari na mafuta ya vidumu.
Hapa ni Mnazi Mmoja jijini Dar Es Salaam, Tanzania karibu kabisa na Peacock Hotel.

Friday, September 20, 2013

Niko kwenye banda la Utafiti -Viwanja vya Nzuguni Dodoma

Hapa niko Dodoma kwenye viwanja vya maonyesho ya Nane Nane Dodoma kwenye banda la Utafiti Mradi wa Kuongeza uzalishaji na Tija katika Kilimo Afrika Mashariki (EAAPP). Mbele yetu ni aina mbalimbali za ngano.

Reaction from Dr. Zacharia Malley

Watafiti wanapokutana kila mtu anajinafasi kutokana na elimu yake, uwezo, ujuzi, maarifa na uzoefu. Mambo yote kwa uwazi kabisa. Hii ndiyo knowledge sharing. Pichani Mkurugenzi wa Utafiti Kilimo, Kanda ya Kati Dr. Zacharia Malley akielezea jambo kwenye kikao kazi cha kutathmini taarifa za 'monitoring na evaluation' kutoka kwenye kanda saba za utafiti nchini kwa mwaka 2013. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Edema mjini Morogoro.
DR.Zacharia Malley - Mkurugenzi wa Kanda Utafiti Kilimo-Nyanda za  Juu Kusini, ARI- Uyole

Mambo ya Edema-Moro

Hizi ni moja ya huduma unazoweza kupata kutoka kumbiza mikutano Edema-Morogoro mkabala na Muslim University, Msamvu. Pichani wadau wakipata supu ya asubuhi baada ya morning session. Edema balaa.

Tuesday, September 17, 2013

Maelezo ya Ubora wa bidhaa

Napata maelezo kutoka kwa mdogo wangu Frank Mdimi-kuhusu ubora wa bidhaa.

NARCO na mikato ya Nyama

Sipendi kula nyama yenye vipande vya magogo. Basi Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) inatumia vifaa vya kisasa kukata nyama.Na kila aina ya nyama ina jina lake. Ukitaka kufahamu nunua nyama kutoka NARCO.

Pendo na Naliendele 92-Mbegu za karanga


Pendo na Naliendele ni aina za karanga.Soma sifa zake ili uweze kulima kilimo cha karanga chenye tija.

Nipo na rafiki yangu wa kijiji cha Makumbusho, Kijitonyama-Dar

Sarah Habib Kondo

Sarah amekuwa Askari kamili baada ya kupata Kipaimara mwishoni mwa mwezi Agosti 2013. Ukisoma St.Mathew wote ni sawa. Angalia vazi la Kipaimara. Simple!

Hongera Sarah kupata sakramenti ya Kipaimara

Ray akimkumbatia nduguye Sarah kwa kupata Sakramenti kwenye Ibada ya Kipaimara iliyofanyika katika Shule ya Sekondari St.Mathew iliyopo katika wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani.

Tupo na Mwanetu Sisty

Kushoto Mama Sisty,kulia Baba Sisty.Furaha ya mtoto kuhitimu kidato cha NNE.

Nimevaa kofia ya Kaka

Maria Banzi kaka yake Sisty akifurahia kofia ya kaka pamoja na rafiki zake.

Maghorofa ya Kariakoo-Dar Es Salaam,Tanzania

Huwezi kuamini kuwa hapa ni Kariakoo jijini Dar Es Salaam.

Furaha ya Kuhitimu- Victory Secondary School

Wanafunzi wa Kidato cha Nne-Victory Secondary School wakiwa pamoja na kufurahia kuhitimu kwao.

Nami nilivaa joho la mwanangu

Nakumbuka sikuvaa joho wakati nilipohitimu elimu yangu ya Sekondari. Tarehe 14/09/2013 nilibahatika kuvaa joho la mwanangu Sisty Banzi. Na hapa najipongeza huku mwanangu Maria akiniangalia.

Nampongeza mwanangu Sisty Banzi


Baada ya miaka minne ya masomo ya Elimu ya Sekondari. Nampongeza mwanangu kwa kumaliza elimu yake ya Sekondari.Sasa anasubiri kufanya mtihani mwezi Novemba 2013.

Mama anampongeza mwana

Sisty Banzi akipongezwa na mama yake kwenye mahafali yaliyofanyika shuleni kwao Victory.

SISTY BANZI-Amehitimu Kidato cha NNE

Mwanangu Sisty Banzi amemaliza miaka yake minne ya Elimu ya Sekondari katika shule ya Sekondari Victory iliyopo-Mwandege, Mkuranga.
Sisty Banzi

Tuesday, September 3, 2013

Kitanda 'Six BY six'

Ukiweza kumudu kununua kitanda kikubwa kama hiki Sita kwa sita basi wewe ni mmoja wa wajanja.Ni kitanda kinachotengezwa na vijana wa JKT kitengo cha Chang'ombe. Mbao imara na godoro safi!

Soseji za samaki kutoka Bukoba

Hapa nilipata bahati ya kula soseji za samaki kwenye banda la soseji za samaki. Mama mjasiriamali wa kutoka Bukoba Mary Karega.Alipohojiwa na kituo cha Televeshini cha ITV changamoto anazozipata kwenye biashara yake alisema kikwazo ni ukiritimba wa kupata idhini ya ubora wa bidhaa kutoka Tanzania Bureau of Standards (TBS)

Samani inayotengenezwa na JKT

Viti na meza ya chakula imetengenezwa na mafundi kutoka Jeshi la Kujenga Taifa kitengo kilichopo Chang'ombe jijini DAR ES SALAAM. Kwanini tunahangaika na vya Mchina? Vilikuwepo kwenye maonyesho ya kilimo huko Dodoma 2013.

Ng'ombe kilo 950

Rampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imeweza kufuga ng'ombe mwenye kilo 950. Ng'ombe huyu alikuwa kivutio kwenye maonyesho ya wakulima ya Taifa yaliyofanyika Dodoma mwezi Agosti 2013.