
Ukitembelea katika vijiji vingi hapa nchini hutoshangaa kukuta washiriki wakuu wa kilimo ni wazee. Vijana walio wengi hawajihusishi kabisa na kilimo. Ukiwauliza wanazo sababu nyingi za kutojihusisha na kilimo zilizo nyingi si za msingi. Wakati Taifa linajipanga katika kuitikia kauli mbiu ya KILIMO KWANZA vyema vijana wakaandaliwa ili waifahamu vizuri kauli mbiu hiyo kwa kuwa tayari kwa utekelezaji wake. Kwa hiyo mafunzo mafupi ya uzalishaji wa kilimo yakiandaliwa kwa vijana wetu yatasaidia sana kuboresha uzalishaji wa kilimo. Kilimo kikiachiwa wazee kitakufa.






