Tuesday, October 3, 2017

Masista wanafunzi (Novisti) wa Shirika la  Carmel,Vikindu, Jimbo Kuu la Dar Es Salaam wakicheza ngoma siku ya mahafali ya wanafunzi wa darasa la saba wa  shule ya Msingi ya Carmel ya Vikindu.

Shukrani iliyoniliza

Ilikuwa zaidi ya shukrani. Pale Dada Slyvia Daulinge, mtoto kitinda mimba wa Bw & Bi. Nestory Daulinge alipotoa shukrani kwa wote waliomhangaikia marehemu Baba yao Mzee Nestory Daulinge hadi kuzikwa kwake. Ilituliza wengi hata kama ni kimyakimya. Hii ilikuwa kabla ya mazishi tarehe 5 Septemba 2017 kule Matombo, Morogoro

Hapa ndipo alipopumzika Mzee Nestory Augustino Daulinge

Dada watatu kutoka Kushoto Slyvia Daulinge,Edditruda Daulinge na Restituta Daulinge wakiwa na mtoto wao baada ya tendo la kumzika baba yao Mzee Nestory Augustino Daulinge tarehe 5 Septemba 2017 nyumbani Matombo, Morogoro.
Wamasai wanapendeza wakiwa na vazi lao la asili wakimlaki Rais wetu Mhe. John Pombe Magufuli. Hivi mchakato wakuwa na vazi la taifa imefikia wapi? Tusiangalie rangi, tutakwama.Tuangalie design.

Tuesday, August 15, 2017

Huyu ndiye Haruna Niyonzima-Fundi

Haruna Niyonzima-Fundi amekwenda kucheza mpira Simba Sports Club. Asante Niyonzima.Hakika umeanza kuonyesha vitu vyako.

Mluguru katikati ya Wazungu

Fr. Kunambi Gega akiwa amezingirwa na wazungu huko Italia

Dafu la kwanza nyumbani Kisemvule Mkuranga


Kisemvule nyumbani kwetu raha sana. Ona mke wangu na mwanetu Sisty wakikata kiu kwa maji ya dafu. Hii ilikuwa mwaka 2012 tulipoanza kuonjam dafu la kwanza kwa minazi tuliyoipanda.

Prof. Ndalichako na maendeleo ya Elimu Mkuranga

Jiwe la Msingi la moja ya majengo ya Shule ya Sekondari Nasibugani iliyopo wilayani Mkuranga likiwekwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof. Joyce Nadilichako. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Sanga na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga  Mhe.Abdalah Ulega.Shule ya Nasibugani sasa ni mpaka kidato cha sita. Hakika, wakati viwanda vinazidi kujengwa wilayani Mkuranga, elimu  lazima iboreshwe kwani viwanda vinahitaji wataalamu.

Wednesday, September 28, 2016

Hili ni group langu nililosoma nalo nchini Urusi

Hili ni group langu la masomo nilipokuwa nchini Urusi kwa masomo yangu.Katika Group hili nawakumbuka wachache kwa majina hasa hao waafrika kutoka kushoto Mamadu (Mali) Mohamed Barrie (Sierra Leone), Mansary (Sierra Leone) na Alex Konte (Siera Leone). Mimi niko mkono wa kushoto wa Mamadu. Hapa ilikuwa ni Crimea, Simferopol mwaka 1989. Nadhani wa kwanza kushoto ni Kutryova na kushoto kwangu ni Svetlana.

Huyu ndiye Ibrahim Ajibu wa Simba

Ibrahim Ajibu wa Simba Sports Club (Nyekundu) akiruka kiunzi wakati wa mpamboa wa klabu yake na AFC-Leopards kutoka Kenya-Tarehe 8/8/2016 katika uwanja wa Taifa, Dar Es Salam. Leopards ilala 4-0. Ni katika kuadhimisha miaka 80 tangu kuanzishwa kwa klabu ya Simba ninayoipenda mimi!

Bright Angels-High School ziara ya mafunzo-Mafia

Wanafunzi wa Bright Angels High School iliyopo wilayani Mkuranga, Mkoa wa Pwani wakiwa katika ziara ya mafunzo huko Mafia wakiangalia mabwawa ya kutengeneza chumvi.

Miaka 80 ya Simba Sports Club nilikuwepo uwanjani

Nilikuwepo uwanjani pamoja na mashabiki lukuki wa Simba nikimshuhudia mnyama akimrarua AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 kwenye uwanja wa Taifa, Jijini Dar Es Salaam. Wote tukiimba kila mtu 'Mavugooo'. Mchezaji huyu wa Kimataifa kutoka Burundi,  Laudit Mavugo alitupia bao katika mechi yake ya kwanza akiichezea SSC. Ilikuwa raha sana. Nimeweka kumbukumbu ya kuhudhuria mechi ndani ya uwanja wa Taifa wakati Simba inatimiza miaka 80 tangu ianzishwe.

Thursday, September 22, 2016

Milima ya Nyingwa-Matombo-Morogoro

Hii ni milima ya Nyingwa, Matombo-Morogoro

Matombo-Lanzi

Mandhari mazuri ya kijiji cha Lanzi,Kibungo, Matombo, Morogoro. Angalia mgahawa kando ya barabara. Kwetu kuzuri.

Hii ndiyo Kamati ya Harusi

Ukisikia kamati ndiyo hii. Hongera!

Maharusi wamechagua kibanda wazi

Hawa ni wadogo zetu Waluguru kutoka Matombo Kiswira waliofunga ndoa hivi karibuni. MC alikuwa Richie Paschal. Kwa mujibu wa Richie harusi ilifana sana.